Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nachukua nafasi hii kukushukuru kwa kuniweka kwenye orodha ya leo ya kuchangia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naunga mkono kwa asilimia mia moja hoja ya Waziri. Nachukua nafasi hii vile vile kupongeza jitihada zinazoendelea kufanywa na Rais, Mheshimiwa Dkt. Magufuli katika kupambana na kuhakikisha nchi yetu inakuwa kwenye mstari sahihi. Desperate times desperate measures. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu ni ndogo tu, ni namna Wizara ya Biashara inaweza ika-sensitize, ikashirikiana na mikoa yote, ni namna gani ya kuweza kusaidia na kunyanyua informal sector katika nchi yetu. Sekta ambayo siyo rasmi kama mama lishe, bodaboda, machinga, welders na vinyozi. Informal sector kwenye nchi jirani hapa, hawa bodaboda, machinga, matatu, welders, mama lishe, vinyozi huchangia dola bilioni nne kwenye pato la Serikali. Pesa hizi kufanya shughuli zao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitakupa mfano kwa Mkoa wa Dar es Salaam tuna wafanyabiashara wa informal sector sio chini ya milioni mbili. Fanya kila mmoja analipa shilingi mia tatu tu kama ada ya ushuru kwa siku mamlaka zinazohusika zitapata milioni mia sita kwa siku, kwa mwezi ni shilingi bilioni 18, kwa mwaka shilingi bilioni 216. Kama kuna programu ya kuhakikisha wanawekwa katika mazingira mazuri tunapata shilingi bilioni 432 kwa kipindi cha miaka miwili tu kwenye informal sector kwenye Mkoa wa Dar es Salaam. Pesa hizi zinakuwa ringfenced, zinalindwa, wanaanzishiwa majengo mapya ya kisasa na kufanya biashara katika mazingira mazuri. Pesa hizi zinaweza zikatumika kuanzisha benki ya wafanyabiashara wadogo wadogo, pesa hizi zinaweza kutumika wafanyabiashara hawa hawa wadogo ambao ndiyo shareholders wakaji-involve kwenye masuala ya biashara ya kilimo. Ethiopia wameweka programu ya kuwafanya vijana kupenda kilimo. Wamechukua vijana 10,000 miaka minne iliyopita, wamewaonesha kilimo cha kisasa na sasa hivi wanafanya kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sekta isiyokuwa rasmi ikiwezeshwa nchini mwetu, ni dhahabu na ni goldmine katika mikoa yote ya Tanzania. Nataka kujua kuna networking gani inayofanywa katika Wizara ya Nishati, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Biashara? Wizara hizi tatu lazima ziwe pamoja kama alivyosema Mheshimiwa Serukamba lazima, tuwe na raw materials na vitu vyote vitapatikana kwa networking ya Wizara hizi tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Serikali ijaribu kutazama sekta isiyo rasmi ambayo tunaiona ni bugudha, tunaiona ni sekta ya kufukuzana nao mitaani, tunaiona kama ni sekta ambayo ni parasite wakati sekta hii ikisimamiwa vizuri inaweza ikatoa mchango mkubwa sana kwenye Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, zao la alizeti mwaka huu nchi nzima kila mkoa uliolima alizeti wamepata bumper harvest lakini wanakatishwa tamaa na mafuta yanayoagizwa nchi za nje. Naomba Serikali ijaribu kudhibiti tunyanyue watu wetu, tuzuie product kutoka nje na tuweze kuwasaidia katika agro-industries. Soko la mafuta ya chakula linapatikana DRC, Rwanda, Burundi na katika region yote hii ya East Africa na ni soko kubwa sana ambalo litawanyanyua hawa wakulima. Kwa hiyo, naiomba Serikali na Waziri wa Biashara yuko hapa ajaribu kutazama masuala haya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba sana Serikali mjaribu kutazama namna gani mtanyanyua informal sector. Mjaribu kutazama namna gani one stop center ya kuleta wawekezaji nchini mwetu itarahisisha uwekezaji kwa kuangalia policies na sheria ambazo zitawavutia.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maneno haya machache, mimi sina mengi, mara nyingi nachangia kidogo kuwaachia nafasi watu wengine, nashukuru sana na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.