Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuchangia hotuba muhimu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Kabla ya kuchangia naomba ku-declare interest mimi kabla ya kuwa Mbunge nilikuwa mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa miaka kumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimefanya kazi na Mheshimiwa Simbachawene, nimefanya kazi na Mheshimiwa Mwigulu na Mheshimiwa Masauni. Kwa hiyo, baadhi ya development ambazo nitazichangia hapa ni jitihada ambazo zimeanza siku nyingi naamini wataendelea kuzifanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, sasa nitachangia maeneo matatu kutokana na muda. Eneo la kwanza, nitachangia kuhusu makazi na nyumba za askari; eneo la pili, nitachangia kuhusu Jeshi la Polisi na Jeshi la Zima Moto na Uokoaji; na eneo la tatu, kwa mapana nitachangia kuhusu vitambulisho vya Taifa.

Mheshimiwa Spika, sasa katika upande wa makazi na nyumba za askari, Wabunge wengi wamechangia hiyo concern kuhusu kuboresha nyumba za makazi. Kwa kweli kwa mfano mimi kwenye jimbo langu la Igunga, tuna nyumba zimejengwa mwaka 1993 mimi nilikuwa darasa la kwanza, mpaka leo hazijawahi kufanyiwa maboresho. Kwa hiyo kama Wizara ijaribu kuangalia kuja na package ambayo itasaidia kuanza kuboresha nyumba za askari.

Mheshimiwa Spika, katika hilo nina wazo ambalo naweza kulitoa. Kwa mfano tunaangalia tunapopata fedha ya barabara tunapotoa kwenye mafuta, sasa kuna faini na tozo mbalimbali ambazo zinatoka kwenye taasisi za Wizara ya Mambo ya Ndani, inaweza Wizara ikajenga hoja Serikalini na ikaja hapa ikipitishwa na tukakubaliana, katika tozo na faini mbalimbali angalau kila asilimia kumi basi ikaingizwa kwenye Mfuko Maalum kwa ajili ya kuboresha nyumba za makazi ya askari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, itakapotoka hii fedha itakuwa na Mfuko Maalum halafu itaenda kufanya kazi kwa mfumo wa force account kupitia hata Jeshi la Magereza kwa maana itatusaidia sana kuboresha nyumba za askari na kujenga nyumba mpya.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, ni kwenye suala la Jeshi la Zima Moto na Uokoaji, kama alivyosema Waziri wamepanga kununua magari mawili lazima pia wawe na wilaya za kimkakati. Kwa mfano Wilaya yetu ya Igunga, pale bomba la mafuta kutoka Uganda linapita na litakuwa na kituo kikubwa cha koki, sasa wilaya ina ofisi ya zima moto lakini haina gari la zimamoto. Kwa hiyo tunaomba Waziri maeneo kama haya ambayo ni ya kimkakati kwa sababu lile bomba ni kubwa, ni la gharama kubwa, ikitokea eruption ya moto bila kuwepo na gari pale tutatafutana na tutauwa wananchi wengi. Kwa hiyo maeneo kama haya, yawe ya kimkakati kwa Wizara ili waweze kuyapa kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, suala lingine katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ni suala la motisha kwa wafanyakazi. Wale wafanyakzi wanafanya kazi wakati mwingine katika mazingira magumu ya kuokoa watu kwenye moto, kwenye majanga, kwenye maji. Sasa unashangaa, inabidi Wizara waweke mfumo mzuri pia wa motisha itakayowasaidia hawa watumishi wa jeshi la zimamoto wote kwa ujumla. Tusiwe tunasubiri kwamba mtu amefanya wonderfully deeds, kaokoa mtoto au kafanya nini, ikishaanza kusambaa kwenye ma-group ya WhatsApp ndio anatafutwa awe awarded. Kwa hiyo naomba tubadilishe huo mfumo hili tuweze kuwapa motisha askari wetu.

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu ambalo napenda kulichangia kwa upana kidogo ni suala la vitambulisho vya Taifa. Kwa kweli wakati design ya National ID inafanyika, NIDA imeanzishwa mwaka 2008, moja ya jambo kubwa ambalo lilikuwa ni lengo lake, ukiacha la kiusalama, ni kuhakikisha inatusaidia kutambua walipa kodi wa nchi hii, taxpayer identification. Kwa kipindi kile walipa kodi walikuwa milioni mbili lakini walikuwa wanatakiwa kuwa milioni 14, sasa kama Wizara ifanye tathmini hili limetusaidia vipi katika kuongeza walipa kodi mpaka sasa hivi.


Mheshimiwa Spika, kuna suala la kuzalisha vitambulisho, lazima itoke kwenye hili suala la namba, twende tukazalishe ili watu wengi waweze kutambulika. Sasa hivi katika moja ya vitu ambavyo inakwenda ni digital economy. Watu wanalipa kwa kutumia kadi, hizi kazi za vitambulisho vya Taifa, hata katika design yake ni kwamba baadaye tunasema tutumie kama e- wallet ambayo maana yake ni kwamba, malipo haya yanayofanyika katika huduma mbalimbali, mtu anaenda na kitambulisho cha Taifa na ile namba yake ya utambulisho, analipa anatoa kadi inachanga malipo yanafanyika. Tukifikia hivyo, Serikali itapata kodi lakini tutakuwa tumebadilisha pia mfumo wa kutembea na pochi kubwa hiizi mifukoni zenye hela nyingi.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ningependa kumshauri Waziri na Wizara wasaidie, NIDA wakati inafanyiwa design na sasa hivi ilipo, nyaraka nyingi zimekuwa za kipindi kile NIDA bado ina watumishi zaidi ya 100. Sasa hivi NIDA ina-oparate nchi nzima, ina ofisi nchi nzima na ndio maana ugumu unakuja kufanya kazi, mtumishi wa NIDA aliyepo Kongwa akihitaji kununua kalamu, lazima awasilisane na Makao Makuu Dar es Salaam, ni ngumu sana kufanya kazi na kutoa matokeo. (Makofi)


Mheshimiwa Spika, naomba wabadilishe, kwenye majeshi mengine yaliyoko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani, wanaona namna tunavyo-oparate kupitia Makamanda wa Mikoa, sasa na NIDA tubadilishe ili mamlaka katika wale Maafisa wa NIDA wa Mikoa wawepe nguvu ya kuweza kusimamia maafisa walioko katika maeneo yao. Sio mtumishi anahitaji pini ya kubana fomu ya usajili, anatakiwa aombe Dar es Salaam ndio ipelekwe kule Wilayani. Hilo waliangalie sana.

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo ni la muhimu, naomba Mheshimiwa Waziri akalifanyie kazi kulikuwa na mikataba miwili, naomba waiangalie vizuri, ambayo baadaye itawasadia. Kulikuwa na mkataba wa ujenzi wa ofisi za NIDA nchi nzima, walijenga awamu ya kwanza, wanatakiwa kwenda awamu ya pili wakaangalie wamefikia wapi. Mkataba mwingine wa muhimu...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)