Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Madini

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Madini

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwanza kabisa naomba kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji wake mzuri lakini kwa namna ambavyo anaendelea kuonesha weledi katika Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye maeneo mawili, eneo la kwanza ni la mikataba kuwekwa wazi, wote tunajua umuhimu wa mikataba kuwekwa wazi moja ya advantage kubwa ambayo tutaipata ni kutengeneza trust kati ya wananchi na Serikali, lakini advantage ya pili ambayo tutaipata kama tukiwa mikataba wazi ni investars watajenga trust na Serikali na kuepusha migogoro baina yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, advantage nyingine ambayo ni muhimu sana taasisi mbalimbali kama haki rasilimali na nyingine vyombo vya habari, watafiti watatoa mchango mkubwa sana kushauri Serikali namna bora ya kuingia mikataba hii kwasababu watakuwa wanauwezo wa kufanya ulinganifu wa mikataba mbalimbali. (Makofi)

Mheshimimiwa Naibu Spika, jambo moja ambalo Serikali liweke akili ni rasilimali za nchi yetu ya Tanzania, ni rasilimali za wananchi wa Tanzania Serikali ni wasimamizi tu, ukiangalia kwenye Sheria ya Extractive Industry Transparency and Accountability Act ya Mwaka 2015 sheria inaeleza very clearly inataka mikataba iwekwe wazi. Nataka niihoji Serikali leo kupitia kiti chako pia ni kwa nini Serikali mpaka siku ya leo toka mwaka 2015 ukiangalia mwaka 2016, 2017, 2018 mpaka hivi ninavyozungumza hapa hakuna mkataba hata mmoja ambao umekwisha kuwekwa wazi wa kwenye sekta ya uziduaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tusiogope kuweka mikataba wazi, nchi zimekwishafanya hivyo, Ghana wameweka mikataba wazi, Chad wameweka mikataba wazi, Mongolio wameweka wazi Ukraine wameweka mikataba wazi nchi nyingi nikisema nizitaje hapa nitamaliza muda wangu sisi tunafeli wapi? Kwa nini tunashindwa kuweka mikataba yetu wazi! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-wind up atuambie ni lini Taifa letu Nchi yetu itaanza rasmi kutekeleza sheria ambayo tuliitunga wenyewe ya kuweka mikataba wazi, asipofanya hivyo na kama hataeleza na sitaridhishwa nitashika shilingi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nielekee kwenye TEIT bado tunaendelea kuziba mianya inaonyesha uwazi, tumekataa kuweka mikataba wazi tumejiondoa kwenye OGP Open Government partinership tulibakiza TEIT kama kiashiria pekee cha afadhali at-least kutuonyesha mwanga nini kinaendelea kwenye rasilimali zetu. Lakini nasikitika kukuambia kwamba, TEITtoka mwaka 2018 mwaka wa fedha 2018/2019 hawajapewa hata shilingi tano, mwaka wa fedha 1920 awajapewa hata shilingi tano mwaka 2021 awajapewa hata shilingi tano wanafanyaje kazi hawa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna pesa ambayo imetoka kutoka world bank bilioni 1.75, nafikiri ndio hii ambayo Wizara inatazama inakwenda TEIT, lakini wanatakiwa wajue kwamba fedha hii imetengwa na world bank purposely kwa ajili ya mradi wa EGPS, na hii ni extra-resource ni lazima Serikali itenge fedha kwa ajili ya TEIT ili TEIT iweze kujiendesha yenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niipongeze sana TEIT inafanya kazi kubwa sana pamoja na kutokuwana fedha nimepitia ripoti za TEIT 10 toka mwaka 2009 mpaka mwaka 2019, kuna mambo yanasikitisha kwelikweli, TEIT wamelipoti wanasema hivi, kuna risiti za malipo kutoka makampuni ya madini kwenda Serikalini, hazionekani na wanasema zaidi ya fedha bilioni 90 za kitanzania hazina maelezo ziko wapi na vielelezo havipo hizi sio taarifa za Jesca Kishoa ni taarifa kutoka TEIT. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, CAG alipewa kazi maalum ya kuchunguza ripoti ya saba na ya nane kuangalia fedha hizo zimekwenda wapi, nataka nikujulishe leo kwenye Bunge lako Tukufu ripoti hiyo toka CAG ameifanyia kazi imefichwa makwapani hatujaiona na hatujui hiko wapi. Nina jedwali linaonesha fedha ambazo TEIT imeweka wazi ambazo zinaonesha kuna discrapper za hali ya juu sana kwenye ripoti ya kwanza ya TEIT wanaonyesha kuna fedha ambazo risiti zake zina maelezo yake hayaeleweki milioni 24 zaidi ya bilioni 24 ripoti ya pili inaonesha zaidi ya bilioni tano hazina maelezo na risiti zake haziko wazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ripoti ya tatu inaonyesha zaidi bilioni 10 ripoti ya nne zaidi ya bilioni 2 ripoti ya tano zaidi ya bilioni nane ripoti ya sita zaidi ya bilioni 2 ripoti ya saba zaidi ya bilioni 27 ripoti ya nane zaidi ya bilioni 30 ripoti ya tisa zaidi ya bilioni 1, ripoti ya kumi zaidi ya bilioni 3. Takribani zaidi ya bilioni 90 hazina maelezo yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishauri Serikali kuna kila sababu ya kutunga sheria ya kumpa mamlaka CAG aweze kuwa na mamlaka ya kukagua pesa zinazotoka kwenye makampuni na pesa zinazolipwa Serikalini. Lakini pia ipo haja kupitia kiti chako kama itakupendeza uitake Serikali ripoti ambayo CAG aliipitisha ripoti ya saba na ya nane ambayo aliikagua akairudisha wizarani iletwe hapa Bungeni Wabunge tuihoji na tuipitie kwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naushauri wangu wa mwisho kwa Serikali kama itapendeza hebu ipeni mamlaka STAMICO ipeni nguvu kama ambavyo mmeipa nguvu TPDC, ili STAMICO kama itakuwa ina uwezo wakuwa na shares iweze kusajili shares zake kwenye soko la mitaji automatically hesabu zitakazokuwa zinaingia zitakuwa zinaonekana kwasababu ukishaingia kwenye soko la mitaji, ukishapeleka shares zako huko automatically wewe hesabu zako zinakuwa wazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru sana. Ahsante. (Makofi)