Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Madini

Hon. Salim Alaudin Hasham

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Madini

MHE. SALIM A. HASHAM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Bunge lako Tukufu japo ametumia jina langu Salimu Almas jina la biashara jina langu kamili naitwa Salimu Alaudin Hasham Mbunge wa Jimbo la Ulanga.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa niniiponge Wizara kwa kazi kubwa waliofanya kwa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya madini mpaka hii leo kuonekana sisi pia wachimbaji wadogo ni watu ambao tunachangia katika pato la Taifa. Lakini kuna vitu vichache ambavyo napenda kuvichangia kwenye Wizara ya Madini ili kuviweka sawa inawezekana ikachangia pato zaidi kwenye upande wa madini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, natokea kwenye upande wa madini ya vito na nimekulia kwenye madini ya vito cha kwanza kabisa naomba nichangie katika upande wa value addition. Kwenye upande wa value addition, Tanzania tuna madini ya aina nyingi sana na Tanzania inaachangia duniani kwa asilimia karibu 30 kwenye madini ambayo yanaingia kwenye soko la dunia.

Lakini niseme ukweli kabisa kwamba Serikali bado hatujajipanga vizuri kwenye upande wa value addition na hii nitatoa mifano michache kutokana na ufinyu wa muda mfano mkubwa kabisa tuna madini aina ya safaya ambazo zinachimbwa Tanga na ambayo yanachimbwa Tunduru kwenye Jimbo la ndugu yangu Hassani. (Makofi)

Mheshimimiwa Naibu Spika, madini yale yamewekwa kwenye utaratibu kwamba mwongozo unasema madini yale yasafirishwe kuanzia gramu mbili kushuka chini ndio yasafirishwe yakiwa ghafi. Kwa maana hiyo kwamba madini ya juu hayawezi kusafishwa lakini kinachotokea ni kwamba kwenye upande wa safaya madini ya safaya ili yaweze kuongeza thamani lazima yafanyiwe treatment kwa maana yachomwe na utaalamu ule bado haujaingia kwenye nchi yetu kabisa huko Thailand peke yake na hawajawahi kuugawa utaalamu ule kwenye nchi zingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana hiyo Serikali itakuwa imeamua kuuwa biashara ya madini aina ya safaya, vinginevyo wangeruhusu yale madini mengine yaweze kusafirishwa madini ya vito yasafirishwe yakiwa ghafi ina maana labda kuna uwezekano ingesaidia utoroshaji wa madini katika sekta ya madini. Ninayo mifano mingi lakini kutokana na ufinyu wa muda kwa sababu nina vitu vingi vya kuchangia naomba niendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna upande wa ma-valuer kiukweli Serikali ina ma-valuer wachache sana kwa upande wa Tanzania katika idadi ambayo tulionayo katika takwimu inaonyesha tuna ma-valuer 18 peke yake ambao hawatoshi lakini naamini kabisa Serikali inapambana kuongeza ma-valuer lakini pia ma-valuer wetu wengi awana uzoefu mkubwa wa kufanya valuation ya madini tuliyo nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini naamini kipindi ambacho wanaendelea kufanya kazi watapata uzoefu ili kujihakikishia kazi ambayo wanaifanya. Lakini pia kuna maneno yanasemekana kwamba ma-valuer wetu ndiko mapato yanakopotelea jibu nasema sio kweli kabisa na inawezekana ma-valuer hawa wanawapatia faida zaidi Serikali kuliko wafanyabiashara kwasababu mara nyingi Serikali kuliko wafanya biashara kwasababu mara nyingi wakikosea wanakosea kwenye kuongeza thamani ya madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kodi utakayolipa itakuwa ni kubwa zaidi naomba Serikali ijikite zaidi kuangalia madini yanapotelea wapi lakini sio mapato yanakopotelea naamini kabisa madini yakifika kwa ma-valuer Serikali haina kinachopoteza. Kwa hiyo, ijikite kwenye kuangalia madini yanatoroshwa vipi lakini si yanapotea kutokana na wanaofanya valuation.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa lingine naomba nichangie na hii itakuwa ni special case Mheshimiwa Waziri unisaidie kidogo kwenye upande wa Jimbo langu kuna kampuni mbili ambazo zinataka kuja kufanya miradi mikubwa ya madini ya kinyo yaani graphite. Kampuni zile ni Tanzagraphite na ingine inaitwa Mahenge - resource. Mwaka 2017 walifanya uthamini juu ya kuwalipa fidia wana Kijiji wa Ipango, lakini mpaka mwaka 2019 uthamini ule ulikuwa ume-expire kwa maana hiyo kampuni ya Tanzagraphite ilipaswa kuwalipa posho ya usumbufu wananchi wa Ipango kulingana na kucheleweshwa na kusitishwa shughuli zao za maendeleo na waliandikiwa barua walihimizwa kwamba wafungue akaunti ili waweze kulipwa posho hizo lakini mpaka leo hawakuweza kufanya kitu kama hicho.

Mheshimiwa Naibu Spika, na bado watu wale wamesitishwa kabisa kufanya shughuli za maendeleo kwa hiyo nilikuwa naomba kupata muhafaka wa kampuni ile nini kinaendelea na nipate muafaka mzuri nione jinsi gani ya kuwajibu na katika sehemu ambayo nilipata changamoto kipindi nafanya kampeni zangu Mheshimiwa Waziri, nilifika niliwakuta wananchi wale wamekaa chini badala ya kunishangilia. Matokeo yake ikabidi nibadilishe mkutano kwa kikao kama cha familia ili waweze kunielewa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kuna kampuni nyingine ya Mahenge resource ambayo pia imeshafanya uthamini, tunaomba pia uhalali wa kampuni ile na uhakiki wa kampuni ile kwamba ipo tayari kuja kufanya kazi katika vijiji vyetu kwasababu isije na wenyewe wakatokea ikawa kama yenyewe ni Tanzagraphite ambako wananchi wale pia wamesitishwa zaidi ya vijiji vinne havifanyi shughuli za maendeleo.

Mheshimia Naibu Spika, naomba nizungumzie kwenye value of chain kwenye upande wa madini kuna mchimbaji, kuna broker na kuna dealer, ukiweka hawa watu ukiwakusanya pamoja lazima mmoja wapo… broker ni mtu ambaye ana mtaji mdogo mwezangu na mimi au la hana mtaji kabisa. Obvious mchimbaji yule hawezi kufanya kazi na broker akachagua kufanya kazi na dealer, kwasababu wana-cash, maana yake utakuwa umemuuwa yule broker hawezi kufanya biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wale tunawalazimisha wakate leseni watu wanakadiliwa kodi ya mapato mwisho wa mwaka wanapaswa kulipwa na ndio wengi zaidi ambao wanaunganisha biashara kati ya mchimbaji na dealer. Kwa hiyo, naomba pia Serikali iliangalie hili kwa kina zaidi ione ni jinsi gani inaweza kufanya mabadiliko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nirudi kwenye upande wa GST bado haijafanya vizuri sana kwenye upande wake, ningeomba Serikali iwawezeshe sana GST waende kufanya utafiti katika madini yenye thamani kubwa kama vile kama ya aluminum, copper lithium maganize nickel graphite, silver na mengine mengi lakini pia kuna layer- ath-stone kama ruby spinel na madini mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, GST iende ikafanye utafiti mkubwa ili kuongeza wawekezaji waje kwa wingi kufanya, lakini pia Serikali iwaangalie sana wawekezaji wa ndani kwa sababu wawekezaji wa ndani sasa hivi wana uwezo mkubwa wa kufanya, na iwaangalie kwa jicho la tatu ili waweze kuwasaidia na hasa kwenye upande wa mikopo ya wachimbaji wadogo. Wachimbaji wadogo hatuamini kabisa mabenki pamoja wanashauriwa kwa ajili ya kutukopesha lakini mabenki bado hayatuamini kwa hiyo tungeifanya biashara yetu iwe biashara ambayo inatambulika duniani na watu waaamini kile ambacho tunakifanya naamini Serikali yetu ingeweza kuongeza pato zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)