Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nimshukuru Mheshimiwa Rais kuwa na imani na mimi. Vilevile ndugu zangu wa Jimbo la Musoma Vijijini ambao waliamua niwe mwakilishi wao mzuri, tumeanza kujenga uchumi kwa kasi kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba ya Mheshimiwa Rais ni agizo na Wizara ya Nishati na Madini imeanza kutekeleza kwa vitendo. Niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa michango mizuri na wengi ambao wamechangia watakubaliana name kwamba wengine nimeanza kutatua kero zao. Kwa hiyo, wengi wanaomba umeme. Nawathibitishia Watanzania kwamba unakuja umeme mwingi, wa uhakika na wa bei nafuu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wachimbaji wadogo wanatafuta maeneo, na watapewa na vilevile ruzuku itaendelea kupatikana. Tulianza na dola 50,000, tumefika dola 100,000 na tunataka tupate wachimbaji wadogo wanaoweza hata kufika kwenye ruzuku ya dola 1,000,000 au 5,000,000 hivi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, agizo la Mheshimiwa Rais, ni suala la kuondoa umaskini ambao unaendana na kujenga uchumi imara. Ni lazima uchumi wetu ukue kwa zaidi ya asilimia 10 na kufanya hivyo ni kila Mtanzania atumie umeme mwingi, aliyepo shambani na aliyeko kwenye viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa hivi wastani wa matumizi ya umeme wetu, kila mtu hapa, hata tuliokaa humu ni unit 9 kwa mwezi. Kazi niliyopewa ni kuwatoa kwenye unit 9 kwa mwezi, kwenda kwenye unit 250 kwa mwezi. Hiyo ndiyo inayoitwa nchi ya kipato cha kati. Tukifanya hivyo, uchumi utakua kwa zaidi ya asilimia10 kutoka asilimia 7 za sasa hivi. Tukiendelea na asilimia 7 na asilimia 8 umasikini hautatoka.
Kwa hiyo, Wizara ya Nishati na Madini inataka ilete umeme mwingi. Tuna vijiji 15,809; asilimia 33 tu ya vijiji hivi ndiyo vyenye umeme. Kwa miaka miwili inayokuja, ni lazima tufike angalau asilimia angalau 67, theluthi mbili ya vijiji hivyo vipate umeme. Sasa hivi ni asilimia 40 ya Watanzania wote wanaopata umeme. Tukitaka kuingia nchi ya kipato cha kati, ikifika mwaka 2025 angalau asilimia 75 ya Watanzania na ikifika mwaka 2030 kwa sababu Tanzania ndiyo iliwakilisha Afrika kwenye mambo ya nishati duniani, ni lazima tuwe zaidi ya asilimia 90 ya Watanzania wanaotumia umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutafanyaje sasa? Ni kutumia ni vyanzo vyote vya umeme ambavyo tunavyo. Kwa sasa hivi gesi ni karibu asilimia 50, maji asilimia 35 na umeme wa mafuta karibu asilimia 15. Ni lazima tuachane na umeme wa mafuta, uwe umekaa pale kama tahadhari yetu tu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutazalisha umeme mwingi kutokana na gesi asilia, makaa ya mawe na maji. Halafu ndiyo tunakuja nishati jadidifu yaani jua, upepo na mengineyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni kwasababu hesabu hizi lazima ziendane na muda. Leo hii Watanzania tuko milioni 53.5; tutakavyokuwa tunapiga kura mwaka 2020 tutakuwa karibu milioni 65; na tutakapofika mwaka 2025, tukiwa nchi isiyokuwa na maskini na mtu anaamua anachotaka kula, kama mimi napenda muhogo basi tutakuwa karibu watu milioni 80 na uchumi hapa ndugu yangu inabidi Pato la Taifa liwe zaidi ya shilingi bilioni 240 mwaka 2025. Kwa hiyo, niwahakikishie Watanzania umeme wa uhakikia ni lazima. Ahsante. (Makofi)