Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipongeze hotuba nzuri ya Waziri wa Elimu. Kwa ufupi naomba nichangie yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, uandaaji wa Walimu. Tunaomba Wizara isimamie vyuo vya Walimu kwa karibu kwani vyuo vingi ubora umepungua sana:-
(i) Maabara za sayansi hakuna katika baadhi ya vyuo, kufanya Walimu kukosa umahiri wa ufundishaji; na
(ii) Walimu wa Hesabu. Ubora wa Walimu wa hesabu umepungua na kufanya output kuwa hafifu. Nashauri programu maalum ya hamasa kwa Walimu wa hesabu Kitaifa na kutoa zawadi maalum kwa wakufunzi wa hesabu. Hesabu ni tatizo kubwa kwa watoto wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa VETA. Tunaomba kuleta maombi ya kujengewa Chuo cha VETA katika Wilaya ya Buhigwe kwani ni Sera ya Wizara yako ya kujenga Chuo cha VETA kila Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa Nyumba za Walimu/Madarasa. Kwa kuwa, bajeti ya Wizara ya Elimu na TAMISEMI ni ndogo, kwa nini Wizara ya Elimu isishirikiane na Social Security Fund (Mifuko) ili iwasaidie kujenga na Serikali kuwalipa yearly?
Mheshimiwa Mwenyekiti, TCU na Bodi ya Mikopo. Nashauri Wizara isiishie tu kufukuza, naomba uchunguzi uende mbele zaidi kwani inaonekana rushwa ipo kubwa kwenye sekta hizi mbili; maamuzi ya kubadili Secretaries ni muhimu sana, nao wanaweza kuwa ni chanzo cha rushwa. Bodi ya Mikopo wapewe malengo makubwa ya kukusanya mapato kuliko kuachwa kama ilivyo sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri zaidi:-
(1) Fanya ziara za kushtukiza katika taasisi zako.
(2) Komesha siasa mashuleni.
(3) Toa zawadi kwa vyuo bora kwa vigezo vya Wizara.
(4) Toa zawadi kwa wanaofaulu hesabu.