Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Aloyce Andrew Kwezi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ALOYCE A. KWEZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba nichukue nafasi hii kwanza kumpongeza Waziri kwa uteuzi, Naibu Waziri nakupongeza watumishi wote wa Wizara hiyo ya Menejiment ya Utumishi wa Umma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie kwa kuangalia wananchi na watumishi walioko katika jimbo langu, Jimbo la Kaliua, pale tuna watumishi karibu 2,800; wamenituma watumishi hawa, natambua pamoja na watumishi wengine kwenye utumishi wetu kwenye nchi hii ya Tanzania wanaitaji kulipwa fedha zao kwa maana ya madai, madai haya mara ya mwisho imelipwa mwaka 2016; mwaka 2017 uhakiki umefanyika wa madai ya likizo, madai ya matibabu, madai ya uhamisho, madai ya mafunzo watumishi hawa hawajawahi kulipwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tumefanya uhakiki nchi nzima, lakini kulipa hatujawahi kuwalipa. Ninamuomba Mheshimiwa Waziri ahakikishe watumishi hawa tuwarudishie morali yao ya kufanya kazi kwa kuhakikisha wamelipwa maslahi yao. (Makofi)

Niomba niongelee malimbikizo ya mishahara, hapa napo kuna changamoto kubwa sana, mtu amepanda daraja mwaka 2012, mwaka 2014 mchahara ukabadilika anadai malimbikizo, sasa miaka hii yote malimbikizo bado hajalipwa, shida ni nini? Watumishi hawa tunawavunja mioyo, watumishi wamefanya kazi kubwa sana za kubadilisha maendeleo makubwa sana kwenye nchi yetu, hata kwenye jimbo langu bado wanaendelea kujenga hospitali, madarasa wanasimamia wanafundisha watoto wetu, lakini kwa kweli morali ya watumishi inashuka.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia watumishi hawa hata increment mara ya mwisho ni mwaka 2014 kupata increment, walikuwa wanapata kila Julai wanapata increment kwenye mshahara kunaongezeka fedha kidogo, wanaweza kukopa, sasa matokeo yake kule kwenye utumishi sasa hivi mimi naona kama hadhi ya watumishi wa umma imeshuka kidogo. Imeshuka kwa sababu watumishi wanakopa kuliko kiwango, napengine tumewadhibiti kupitia mfumo wa Lawson wa utumishi ambao upo kwamba wanakopa one third, lakini wanakwenda kukopa kwenye wakopeshaji bubu.

Mheshimiwa Naibu Spika, wanakabidhi saa nyingine mpaka kadi zao benki, sasa tunakwendaje? Mimi nilikuwa namuomba Mheshimiwa Waziri waangalie sekta ya utumishi waiboreshi ipasavyo, na pengine kwa wale wastaafu sasa, hapa napo kuna shida, mstaafu anastaafu anadai malimbikizo hajalipwa, lakini kinachoumiza sana wastaafu unapostaafu unafatilia michango yako unakuta Wizara ya Fedha namuomba sana kaka yangu Mheshimiwa Mwingulu Nchemba watumishi unakuta hatukuchangia ipasavyo na ninyi pale mnachelewesha pelekeni zile fedha za wastaafu kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, wastaafu hao waweze kulipwa fedha zao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wewe umestaafu umefikisha miaka 60, umefikisha miaka 55 unakuta kuna gap kubwa sana huku nyuma, una miaka miwili kwamba hukuchangia, fedha yako haijaenda, anaanza kuzunguka huyu mzee, utumishi wa umma anatakiwa aone furaha ya kulitendea kazi Taifa lake, lakini hapa bado lipo shida. Niombe nashukuru sana wakati wanawasilisha TAMISEMI hapa wakaongea kwamba tunaenda kuziangalia RS zile Sekretari za Mikoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi namshauri Waziri wa Utumishi, shida iko hivi pale kwenye RS ili twende na utendaji mzuri watumishi wengine wa RS wamekuwa ni ma-junior hawajafikia kwenye senior post, hawajafikia kuwa waandamizi. Sasa mtu ajafikia kuwa mwandamizi kwenye Halmashauri kuna watu wana miaka zaidi ya kumi na tano, Maafisa Mipango, Maafisa Utumishi, Wakuu wa Idara, wenye sifa za kutosha kupanda kwenda RS, tumewaacha wale pemeni, tunaangalia RS mtumishi ana miaka miwili, anakuja kuongoza, ana mwongoza Afisa Mipango mwenye miaka 15. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yaani kuna muda tulikuwa tunaona vichekesho kwa sababu wewe inabidi kumshauri sasa kwamba ndugu yangu hiki hapa kipo moja, mbili, tatu. Sasa ni nini hiyo succession plan iko wapi, maana yake mfumo wa kurithishana madaraka wale ambao wako competent kwenye level ya Halmashauri wapande kwenda Mikoani wale ma-senior. Sasa sisi tunaacha huku tunampa mtu wa miaka miwili anamwongoza mwenye miaka 20 yule kule ana Ph.D ana Masters, anafanya kazi vizuri, kwa nini tusichukuane yule tukapandisha wale ambao wanaanza at least ajifunze? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na hili linafanana, shida ambayo ilitukuta kwa Hayati ndio succession plan yenyewe hiyo, mama yupo competent kachukua nafasi pale, shida iko wapi? Kwa nini huku bado kuna gap? Kwa hiyo, nilikuwa nashauri tuangalie vizuri eneo hilo ili tuweze kwenda pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine kikubwa zaidi ni kuboresha vitendea kazi, tunawasaidia Waratibu wa Elimu wa Kata pikipiki, tunasahau Watendaji wa Kata, Maafisa Tarafa. Sasa kwenye kata mkubwa wa kata ni Afisa Mtendaji wa Kata, sasa Afisa Mtendaji wa Kata pembeni hakuna ka- incentive kokote kwake, tumeangalia yaani chini yake kule kuna mtu anapata posho ya madaraka, sasa kwa nini na wenyewe tusiwaangalie ili twende vizuri?

Mheshimiwa Naibu Spika, upungufu kwenye sekta ya utumishi, nataka nichangie sehemu moja mahususi kweli kweli. Maana ukiangali Maafisa Kilimo wachache, hata kwenye jimbo langu ni hivyo hivyo, ukiangalia manesi wachache, ukiangalia sijui nini wachache. Lakini hebu twende kwenye human resource allocation tupange watumishi wetu vizuri, centers zina watumishi wamezidi. Centers kubwa zinawatumishi wamezidi, miji zimezidi, manispaa zimezidi, sijui wapi imezidii, kule unakuta mwalimu wawili, watatu. Ukiangalia sehemu fulani hakuna uwiano wako 40/50 sasa tunasaidia Taifa au tunakwendaje kwenye mfumo huo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nafikiria tuwapange kwanza vizuri hao, lakini tuajiri watumishi wa kutosha kwenye sekta zetu. Afisa Ugani mmoja ana control kata mbili tunategemea kweli kilimo kiinuke hapa? Bado itakuwa ni changamoto. Utumishi niwashauri kingine, ikama zinaidhinishwa kila mwaka za kuajiri, tuna miaka hatujaajiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga hoja mkono, ahsante sana. (Makofi)