Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ENG. ISACK A. KAMWELWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia hotuba hii ya Utawala Bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina hazina kubwa sana ya viongozi wetu wastaafu ambao wamepita ngazi za juu, kuanzia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini pamoja na Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunao Marais upande wa Jamhuri ya Muungano, lakini na Zanzibar; tunao Mawaziri Wakuu wastaafu, tunao Makamu wa Rais wastaafu, tunao Ma-chief Secretary wastaafu, lakini pia tunao mpaka Maspika na Naibu Maspika wastaafu. Hawa viongozi wetu ni hazina kubwa sana kwa nchi yetu. Ukienda kule Ulaya wenzetu wana Mabunge ya waliochaguliwa, lakini kuna Bunge ambalo wanaita kwa mfano kama Canada wanaita The House of Queen na Uingereza wanasema The House of Lord. Hili Bunge la pili linakuwa na wale viongozi wastaafu ambao walishatumikia zile nchi na kila muswada unapopitishwa na Bunge la waliochaguliwa hauwezi kupita moja kwa moja, lakini lazima uende ukapate ushauri kwanza kwa wale viongozi wastaafu ambao walishatumika katika zile nchi na kwa kufanya hivyo nchi inakwenda vizuri na utawala bora unakwenda vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa namuomba Mheshimiwa Waziri wa Utumishi, Ndugu yangu Mchengerwa jaribu kuliangalia hili na ikiwezekana kutengeneza mfumo rasmi katika nchi yetu ili tuweze kuwatumia hawa viongozi wetu wastaafu kwa sababu wanayohekima, wana busara nyingi na bado wanauzoefu mkubwa wanaweza wakatushauri hata katika ndani ya Bunge, hilo lilikuwa la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nizungumzie Jimbo langu na nimuombe sasa Mheshimiwa Waziri anisikilize pamoja na Naibu Waziri. Jimbo langu wananchi kwa kutumia Mfuko wa Jimbo pamoja na michango yao walijenga zahanati kumi kwenye hii miaka mitano iliyopita katika hizo zahanati kumi ni zahanati mbili mbili tu ndiyo ambazo zimefunguliwa, zahanati nane bado kwa sababu ya kukosa watumishi. Nimuombe sana Mheshimiwa Waziri kwamba hizi zahanati nane, mtakapo fanya ajira utuletee watumishi ili wananchi waendelee kufaidi jasho lao, wamejenga zahanati wenyewe lakini wanakosa huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu, nataka nizungumzie Shirika letu la Reli na nimpongeze sana Mheshimiwa Rais jana katika hotuba yake amezungumza jinsi gani ambavyo Serikali imekarabati reli ya kutoka Tanga kwenda Kilimanjaro mpaka Arusha na baada ya kukarabati reli hiyo kumekuwa na manufaa makubwa, ajira zimeongezeka, lakini pia mzigo kutoka Tanga wa cement kupeleka Kilimanjaro na Arusha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu train inavuta mabehewa kumi ya cement bei imepungua tofauti na kubeba na lori. Hoja yangu nini, ukarabati ule umefanywa na Watanzania, vijana wetu na waliofanya ngazi ya darasa la saba na kushuka chini. Vijana hawa ile reli ilikuwa imechoka sana wamefanya kazi nzuri, tulikuwa tuna mapendekezo kwamba hawa vijana wangefikiriwa kuajiriwa kama wanavyoajiriwa watu wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mfumo wetu wa ajira una sheria unasema kwamba hauwezi kuajirwa mpaka awe amefika form four, ni form four gani ambaye atakuwa pigilia, ni form six gani ambaye atakubali kufanya ya pigilia, akakae kule kwenye magenge. Nimuombe Mheshimiwa Waziri kama inashindikana basi hiyo sheria ifanyiwe amendment kwa kuletwa hapa Bungeni ili angalau tuweke tu hiyo kwamba ni special tuwaajiri hawa vijana, waendelee kutengeneza ile reli. Kwa sababu tukiacha itaharibika tena kama ilivyokuwa imeharibika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la mwisho, na mimi nizungumzie kidogo suala la utawala bora, lakini kwa kusema nini maana ya nidhamu, nini maana ya heshima, kwa sababu nikichukulia mfano kwenye Halmashauri kumekuwa na tabia ya kuwahamisha watumishi hovyo hovyo kwa matakwa ya mtu mmoja anayeitwa Mkurugenzi, transparent inakosekana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati nipo mtumishi niliwahi kwenda Canada, Montreal, ndiyo nilikokwenda kujifunzia kozi yangu ya leadership, nilichokigundua kule tulipewa semina kama wewe ni Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda, kiwanda kinazalisha vizuri na marketing officer wanafanya kazi vizuri, yule Meneja wa Uzalishaji usimpandishe madaraka, usimpe cheo kwa kumpandisha madaraka ile skill aliyokua anafanya azalishe zaidi. Lakini...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. ENG. ISACK A. KAMWELWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)