Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa muda na mimi nichangie hii hoja ya Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora. mimi nitazungumza kwa uchache sana kwa habari ya Utawala Bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, lipo jambo ambalo linafanya tasnia nzima ya Utawala Bora katika nchi yetu iwe na dosari kubwa sana sana. Kuna hizi sheria, hii ya The Anti Money Laundering CAP 423 ya mwaka 2006 ambayo ilifanyiwa marekebisho na Bunge hili mwaka 2019, inajulikana kama Sheria ya Utakatishaji Fedha na hii Sheria ya Economic and Organization Crime Act. ambayo CAP 200 ya mwaka 1984 ambayo pia ilifanyiwa marekebisho na Bunge hili mwaka 2019 pamoja na Sheria ya Ugaidi ambazo zinafahamika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hizi sheria tatu zinaifanya dhana ya utawala bora katika nchi yetu itiliwe maswali sana. Kwa mfano Bunge hili wakati linapitisha sheria hii au kufanyia marekebisho sheria hii na sheria hii kufikia mahali kwamba haina dhamana kabisa, nia ya Bunge ilikuwa nzuri, lakini katika utekelezaji wake imeingia dosari nyingi sana, kuna watu wengi sana wapo ndani, wapo mahabusu maelfu ya watu kwa sababu ya hili suala la utakatishaji fedha, kubambikiziwa na watu wasio waaminifu katika vyombo vyetu vya dola na kwenye nchi yeyote makini jambo hili haliwezi kuachiwa hivi hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unakuta mtu anakwenda kwa mfanyabiashara kukusanya mapato au kudai mapato au malimbikizo ya mapato anakwenda na charge kabisa anamwambia bwana usiponipa fedha kadhaa tayari nina hati hii hapa ninakuwekea money laundering au ninakuwekea economic sabotage kuna watu wengi sana wapo ndani, wapo mahabusu kwa sababu ya matumizi ya mabaya ya hawa watu wasio waaminifu ambao tumewakabidhi kuitekeleza hii sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka leo kwa mujibu wa takwimu kuna watu 1,701 ambao wako mahabusu kwa sababu ya ama kwa ajili ya money laundering au kwa sababu ya economic sabotage na kwa sababu hiyo nilikuwa nafikiri ni muhimu sana, kwakuwa kazi moja wapo ya Bunge letu ni kutunga sheria lakini na kufanyia marekebisho sheria na kufuta baadhi ya sheria, haileti sense kwa nini mpaka leo wale Masheikh 23 wa Uamsho wa Zanzibar wapo ndani mpaka leo mahabusu, leo ni miaka tisa, haileti sense kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, najaribu kuwaza ningekuwa mimi au angekuwa baba yangu, au angekuwa ndugu yangu ambaye mpaka leo miaka tisa yupo ndani, hajahukumiwa bado na haijulikani ana hatia au hana hatia. Itakuwaje baada ya miaka 20 huyu mtu mkagundua hana hatia, atalipwa nini in-exchange na miaka aliyopoteza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi kwa kweli haliingii akilini kwanini hawa Masheikh 23 wa Uamsho wa Zanzibar wapo ndani mpaka leo kwa miaka tisa, lakini haitoshi kuna Masheikh 64 huko Arusha ambao nao wapo ndani kwa sababu ya hizi hizi Sheria za Ugaidi ambazo hazina dhamana kwa sababu ambazo hatuzielewi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nashangaa kwa nini Masheikh tu wapo ndani kwa ajili ya Sheria za Ugaidi hakuna gaidi mwingine ambaye sio Sheikh?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri husika pamoja na Serikali kwa ujumla tuangalie kwa undani sana namna ya kuli-handle suala hili, kwa sababu sio sahihi Masheikh hawa wakawa ndani kwa muda wa miaka tisa, sisemi kwamba wana hatia au hawana hatia sijadili kosa lao, lakini ninachojadili ni kwamba basi wangehukumiwa basi ikajulikana. Wangehukumiwa wangejua wamebakiza miaka mitatu/miaka minne/miaka mitano/miaka sita. Lakini sasa wapo ndani bila kujua watamaliza lini matatizo yao mimi nilikuwa naomba Wizara pamoja na by-imprecation Waziri wa hii Wizara ni Mheshimiwa Rais, na Mheshimiwa Rais wa nchi ni Rais wa nchi lakini pia ni Waziri wa hii Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naomba jambo hili lifanyiwe kazi, kuna watu wengi sana, rafiki yangu mmoja akanipigia simu akaniambia Askofu kuna watu wamekuja kwangu wananiambia ama niwape milioni 100 ama wanipe money laundering, nikamwambia wape haraka haraka utapata money laundering na utashindwa namna ya kutoka.

Nilikuwa nashauri sana sana kwa ajili ya kuondoa dorasi zinazotokana na kusemwa kwamba Tanzania hatuna utawala bora, tuweze kuziangalia kwa makini hizi sheria, tuzi- revise na naomba sana rafiki yangu Mheshimiwa Mchengerwa ulifanyie kazi hii Masheikh hawa 23 na Masheikh hawa 64 ambao wapo ndani utafute namna ya kufanya, vinginevyo nitakuondolea shilingi kwenye bajeti yako. Ahsante sana. (Makofi)