Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi na kwa sababu ya muda naomba niende moja kwa moja na nina hoja moja tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Chama cha Mapinduzi traditionally ni Chama cha Wakulima na Wafanyakazi, ndio base yetu; ndio social base ya chama hiki. Na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ni muhimu sana, sana, ikashughulika na wafanyakazi wa nchi hii kama mtaji muhimu wa Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa nataka kuzungumzia jambo ambalo limezungumzwa na Wabunge kwa sehemu; lakini mimi nimeona nililete kwenye Wizara ya Utumishi. Jambo la haki na stahiki za walimu wa Tanzania. Nimeona nizungumzie hawa kwa sababu kwanza, ni karibia asilimia 70 ya watumishi wa umma wa nchi hii ni walimu, lakini ndio watu ambao tumewakabidhi watoto wetu na vijana wetu kwa kuwalea na kuwafundisha kulitengeneza Taifa letu tunakokwenda. Kwa hiyo, ni kundi muhimu kabisa muhimu sana, lakini bahati mbaya Wizara ya Utumishi na Hazina wamekuwa wakitoa nyaraka na taratibu ambazo kwa namna moja ama nyingine zimekuwa hazilitendei haki kundi hili kubwa katika watumishi wa umma wa nchi yetu. Nyaraka hizi na taratibu ambazo zimekuwa zikitumika kwa mfano kwa walimu zimezaa makundi yafuatayo:-

Moja, kuna kundi la walimu ambao walipewa barua za kupandishwa madaraja lakini stahiki zao hazikubadilika mpaka wakastaafu. Kwa hiyo mafao yao ya mwisho yameathirika sana na kundi hili lipo mtaani, kubwa! Wamepewa barua, stahiki zao hazikubadilika na hivyo mafao yao yameathirika kwasababu stahiki zao hazikubadilika.

Kundi la pili, walimu waliopandishwa madaraja kwa barua, lakini hakukuwa na mabadiliko kwenye stahiki zao kwa muda mrefu mpaka wamekutwa na barua zingine za kupandishwa madaraja wakati zile za awali hazikufanyiwa kazi. Kundi hili nalo lipo kubwa katika kada hii ya walimu.

Kundi la tatu, walimu ambao wamepandishwa madaraja au vyeo kwa makaratasi, lakini mpaka leo wamebaki na maandishi ya pesa kwenye makaratasi lakini stahiki zao hazijaguswa.

Kundi la nne na hapo nataka niguse mifano tu, walimu ambao walipandishwa madaraja kwa barua na hii nadhani ilikuwa mwaka 2013. Wakakaa nazo bila ya mabadiliko ya stahiki zao, baada ya muda ukaandikwa waraka ukafuta, kule kupandishwa kwao madaraja na bila sababu ya msingi na mimi nadhani ni baada ya kuona kuna mlimbikizo mkubwa Serikali ikataka kukwepa deni hili ikaandika waraka wa kufuta waraka wake ambao uliwapandisha hawa walimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, haya madaraja na stahiki zao sio hisani ni haki zao. Hivi inavyoendeshwa, inalifanya jambo hili ligeuke kuwa ni hisani kuwapandisha madaraja na kuwapa stahiki zao. Hili jambo si sawa, hatuwatendei haki walimu wa nchi hii. Ni matumaini yangu nimesikia Wizara wanasema kwamba wanapandisha madaraja watu ni karibu 900. Lakini kupandisha huku madaraja kusisahau hawa ambao tayari wameshaathirika kwa sababu ya mfumo mbovu ambao tumeutumia. Nyaraka tunazoziandika kutoka Utumishi, zisigeuke kichaka cha kupora haki za watu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haki ndio itainua Taifa hili, hili kundi ni kubwa sana kulifumbia macho na kuja tu na hoja tu ya kupandisha madaraja peke yake hakutafidia haki ambazo zimepotea za haya makundi na haya ni machache inawezekana yapo mengi sana na jambo hili limezungumzwa hapa. Sasa mapendekezo yangu, naiomba Serikali ikiwezekana iunde Tume Maalum iende ikachunguze ili wale ambao tayari wamekwishaathiriwa na huu mfumo tuwarekebishie mambo yao hata kama tutawalipa taratibu lakini haki yao isipotee kila mmoja apate haki yake. (Makofi)

Mimi ni matumaini yangu wizara wamepewa vijana wadogo zangu; na nina hakika watafanyakazi vizuri, Mheshimiwa Mchengerwa na mwenzake nina aamini mtakwenda kutendea haki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na nimemsikia Mheshimiwa Rais, akizungumza suala la haki, jambo hili ni haki ya wafanyakazi ukiacha maslahi yao ya kupandisha mishahara, lakini hata hiki ambacho ni haki yao, nataka kuiomba Serikali ya Chama cha Mapinduzi; chama cha wakulima na wafanyakazi, twendeni tukatende haki kwenye suala la stahiki za hawa wafanyakazi ambao tumewaacha, wananung’unika na msisahau Waheshimiwa Wabunge ndio hawa pia wamesimamia chaguzi zetu. Wamefanya kazi nzuri, wanafanya kazi nzuri ya kuwalea watoto wetu, hebu tusiache haki zao zikapotea.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi leo unaajiriwa, ukiajiriwa kwa teknolojia ya leo, likiingizwa jina lako kwenye kwenye mfumo kuna haja gani tena ya kuanza kuhangaika na taarifa kule chini! Tayari kishaingizwa kwenye mfumo tunajua baada ya muda fulani nitastaafu.

Leo kuna watu wanastaafu wanakaa kule mpaka wanakuwa wanywa gongo! Kwa nini? Kwa sababu hamuwapi haki zao za kuondokea kwenye vituo vyao vya kazi. Kila siku lete document hii, lete document hii, na nikushukuru, Mheshimiwa Naibu Spika asubuhi umelizungumza jambo hili, jambo hili lina umiza, tumeanza kutumia utaratibu wa kuhakiki, utaratibu wa kutaka nyaraka kama kichaka cha kupora haki za watu. Hizi haki zao zisimamiwe wazipate. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa kengele imeshagongwa.

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.