Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii niweze kuchangia mchango wangu. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kuchaguliwa kuwa katika Wizara hii ya TAMISEMI na Naibu Mawaziri wake, wanaofanya kazi vizuri. Sina wasiwasi na viongozi wetu hawa katika Ofisi hii ya Rais TAMISEMI.

Mheshimiwa Spika, moja ya majukumu yatokanayo na mgawanyiko wa majukumu yaani presidential instrument kwa Wizara hii ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI ni kuziwezesha Tawala za Mikoa kuendesha majukumu yake ya kisheria. Kwa kuwa moja ya majukumu hayo ya kisheria ya Serikali zetu za Mitaa yanatakiwa yaendeshwe kwa gharama zinazotolewa katika bajeti na Serikali.

Mheshimiwa Spika, sisi katika Mkoa wetu wa Ruvuma Halmashauri zetu kwa ujumla wake nitatolea mfano mwaka 2019/2020 OC zilizoidhinishwa zilikuwa ni bilioni 20 milioni 255 lakini zilizopokelewa ni asilimia 47, bilioni tisa. OC ndiyo zinazofanya kazi ya kuendesha shughuli za Serikali za Mitaa Kisheria kwa maana ukiondoa mishahara, kwenda kuangalia shughuli za maendeleo, kusimamia n.k. sasa sisi mkoa wetu una square kilometers 67,372. Ukitoka kwa mfano mkoani kwenda mpaka Tunduru ni zaidi ya kilometa 260, kunahitajika magari ya kutosha, kunahitajika fedha za kwenda kugharamia mafuta n.k. ukifika Tunduru kwa mfano kwenda katika eneo la Kusini unatembea zaidi ya kilometa 100 na kidogo. Ukifika Namtumbo kwenda kufika katika Kata ya mwisho unatembea zaidi ya kilometa 200 na kidogo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, fedha za OC za miaka hiyo, 2019 zilikuja asilimia 47. Nasema haya kwa maana ya kwamba ukitazama katika mikoa mingine katika randama kuna wengine sekretarieti ya mkoa imepata zaidi ya asilimia 113. Kwa hiyo, ninachotaka kuiomba Serikali, wanaotoa fedha hizi, wanaofanya disbursement asilimia za ugawaji wa fedha uendane sawa na mikoa yote kuliko kufanya upendeleo mkoa fulani unapata asilimia 47, mkoa mwingine unapata zaidi ya asilimia 100. Kwa hiyo, naomba sana ili twende sambamba disbursement za fedha hizi zinatakiwa lazima zitoke sawasawa. Sitaki kutaja mkoa gani lakini tazameni kwenye randama mtaona tofauti zilizopo. Nimetolea mfano wa eneo langu la Mkoa wa Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, lakini fedha za maendeleo pia angalau tuliidhinishiwa bilioni 30 lakini tukapata bilioni 21 na milioni 600 sawa na asilimia 72. Lakini mpaka bajeti ya mwaka huu 2020/21 mpaka Februari, tumepata asilimia 31 za OC na development asilimia 26.9. Kwa hiyo, bado naamini kabisa sidhani kama tutafikia asilimia 100 mpaka tutakapofika Juni 2020.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka kuomba kwanza Serikali ituongezee ukomo wa bajeti, ituongezee pia zile hela ambazo zinapitishwa kwenye bajeti basi tuzipate kwa asilimia 100 katika mikoa kama ya Kusini ambayo ina mipaka miwili ina kazi kubwa sana katika kuhakikisha kwamba wananchi wake wanasimamiwa na wanapata maendeleo.

Mheshimiwa Spika, sisi katika Wilaya yetu ya Namtumbo ina kilometa za mraba 20,375 tuna watu 240,000 lakini jimbo hilo hilo lina jimbo moja na halmashauri moja lakini utakuta katika mkoa wetu nachukulia mfano, una halmashauri zingine zina square kilometer 6,000, watu ni wengi lakini kilometa za mraba ni ndogo ukilinganisha na eneo letu. Kwa hiyo, inakuwa ngumu sana katika wilaya na halmashauri yetu kusimamia au kwenda kuleta maendeleo ya wananchi kwasababu kilometa za mraba ni kubwa lakini fedha wanazozipata ni kidogo sana kulinganisha na shughuli zilizopo katika wilaya yetu. Lakini ukitazama malengo tunayowekewa na Serikali tunayatimizia kwa asilimia zaidi ya 100. Sisi tuliwekewa lengo la kukusanya bilioni 1.4, tulikusanya bilioni 1.6.