Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana niugane na wenzangu ambao waliosimama katika Bunge lako hili Tukufu kuichangia TAMISEMI na Serikali za Mitaa. Kwa kuzungumzia moja kwa moja, nazungumzia kwenye hoja maana nisemi Mheshimiwa Ummy Mwalimu nimpongeze na nimshukuru sana kwa kuletwa kwenye kamati hii na kwa kweli umeonekana mtu mahiri wa kuja kwenye kamati hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naanza kutangulia kusema kwamba kuna watumishi wengi katika halmashauri ambao hao watumishi wa umma hawajapata stahiki zao kwa kipindi kirefu. Suala hili la watumishi wa umma ambao waliokuwa awajapa stahiki zao toka kipindi cha miaka ile mitano tuliyopita tulikuwa tunazungumzia wastahiki hawa wa umma katika Serikali yetu. Kwa hiyo, napenda kuishauri Serikali yangu ili hawa watumishi waliokuwa wameacha kazi zao wapewe stahiki zao kwa uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile kwa kuzungumzia suala la kuunganisha vikundi vya watu wenye ulemavu au watu wa mahitaji maalum, tumetembelea katika halmashauri katika kamati yangu hii tumewaona vikundi mbalimbali ambavyo vilivyokuwa havijaunganisha kwenye halmashauri zile watu wenye ulemavu ili wakaweza kufanya kazi zao katika vikundi vyao na ile asilimia yao mbili wanayoipata, bado awajakaa kabisa wakaweza kufanya kazi zao.

Mheshimiwa Spika, vilevie napenda kuishauri Serikali waweze kuwapatia mafunzo watu wenye ulemavu ili waweze kujisaidia nakujikwamua kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la mwisho nazungumzia kuhusu TASAF, TASAF kusaidia wananchi wanaonufaika ruzuku za Kaya Maskini, hii TASAF tulikuja tukaitia baraka hapa katika Bunge lako Tukufu na kwa bahati hii TASAF ipo katika halmashauri lakini napenda kusema kwamba ninaishauri Serikali TASAF izidi kufanya kazi zao kwa urefu zaidi ili waweze wale watu wa Kaya Maskini wapate na wao kunufaika, na vilevile wawapatie vikundi mbalimbali katika ndani ya hii TASAF ili na wao waweze kufanya kazi zao vizuri na waweze kujikwamua kiumaskini.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana naomba kuunga hoja mkono asilimia mia moja ahsante sana. (Makofi)