Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi kuchangia hoja katika Serikali za Mitaa, sehemu ya kwanza napenda kuchangia ni uhamisho wa watumishi wa Serikali za Mitaa kumekuwa na matatizo sana la watumishi wa Serikali za Mitaa kuhama kwa suala kubwa hili la kubadilishana hilo suala limekuwa kizungumkuti.

Mheshimiwa Spika, kuna mtu ambaye nilikuwa namshughulikia kabisa mwenyewe aliniomba document zake nizishughulikie nimeangaika nazo muda mrefu karibu miaka miwili bila mafanikio na huyo mtu alishapata mtu wa kubadilishana naye na kulikuwa na nyaraka zote ambazo zilikuwa zinatakiwa kwa ajili yakubadilishana.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa kila siku naenda Mtumba kila baada ya siku mbili tatu lakini nikifika kule naambiwa document hazipo natoa kopi zingine naacha, nikika siku mbili nikienda tena naambiwa hizo document hazipo natoa copy nyingine naziacha pale, nimefuatilia hiyo issue karibu miaka miwili mpaka ilipofika kipindi cha kwenda kwenye kampeni nikaacha nikamwambia yule binti aje mwenyewe kibaya zaidi alivyokuja mwenyewe ndio yalitokea mambo ya ajabu sana.

Mheshimiwa Spika, baada ya kufuatilia pale aliandikiwa barua feki ya uhamisho yule binti yangu alitaka kufukuzwa kazi alipokwenda kuripoti sehemu ambayo anatakiwa kwenda kuripoti walipofuatilia ile barua ilionekana ni feki. Kwa kweli matatizo yalikuwa makubwa sana, ikabidi niingilie kati yale mambo yakaisha akarudi kwenye kituo chake kilekile cha kwanza. Kwa hiyo, tunaomba TAMISEMI iangalie kitengo hicho cha uhamisho mambo yanayofanyika ni mabaya naya aibu sana tunaomba kuwaomba mjitahidi kurekebisha hapo Serikali yetu Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni eneo la watumishi wa afya na walimu kuna maeneo mengi katika mkoa wetu ya Lindi ni sehemu ambazo sio rafiki sana kwa kuishi, ni sehemu zenye mazingira magumu. Watumishi wanakwenda pale kwenda kuchukuwa cheki namba baada ya muda wanatafuta uhamisho kuhama kwenda sehemu nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunaomba kuna watumishi vijana ambao wamemaliza chuo wako kwenye maeneo yale wameomba nafasi za kazi naomba wapewe kipaumbele wale vijana kuliko mkiwachukuwa watu ambao wanatoka maeneo ya mbali wanafika pale kuchukuwa cheki namba wanaondoka mfano halisi ni Wilaya ya Liwale, Nachingwea huko Kilimarondo kuna shida sana za watumishi na sehemu nyingi.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya tunacho kikubwa kizuri cha Kilimarondo lakini inakatisha tamaa watumishi wako 12 pale wanafanya operation zote wana huduma nyingi zote afya lakini hali ni ngumu. Kwanza hata jokofu lile la theatre hawana, hawana vifaa tiba, watumishi ni wachache. Na pia kuna hospitali zetu za wilaya kuna Hospitali ya Wilaya Nachingwea, ina hali mbaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hospitali ile ya Nachingwea haina vifaa tiba muhimu kwa mfano kuna wodi ya wazazi iliyopo pale haina kifaa hata kimoja ni jengo tu lipo pale mapambo lakini hakuna kifaa tiba kwenye ile theatre na theatre kubwa iliyopo katika Wilaya ile ya Nachingwea haina hata zile taa hakuna hata washing machine vitanda ni vya kizamani vimechakaa sana, tunaomba Waziri husika atupie macho hospitali za Mkoa wa Lindi zaidi zile zilizopo pembezoni na Vituo vya Afya ili waweze kusaidia wananchi wa kule wapate huduma stahiki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine ambalo tunaliomba kwako kwa hawa watumishi ambao wanakwenda kwenye sehemu mazingira magumu tunaomba iweke posho kwa watu wale ahsante naomba kuchangia hoja. (Makofi)