Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JUMA OTHMAN HIJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naanza kuchangia hotuba hii kwa kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuwa miongoni mwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Pili, napenda kuwashukuru wapigakura wangu kwa kuniamini na kunichagua kwa kura nyingi. Natambua imani yao kwangu na nawaahidi kuwatumikia kwa nguvu zangu zote. Tatu, napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Magufuli kwa kuonesha imani na uwezo mkubwa wa kuendesha nchi.
Nne, napenda kumpongeza Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa pamoja na Baraza lote la Mawaziri kwa kuonesha uwezo mkubwa wa kuongoza Wizara zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia hotuba hii ya Elimu, napenda kuchangia maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ada za vyuo binafsi nchini. Serikali imekuwa na nia nzuri ya kuruhusu vyuo binafsi nchini, hili ni jambo zuri na la maana; masikitiko yangu katika hili ni pale inapoonekana baadhi ya vyuo kutoza ada kwa kulipa fedha za kigeni badala ya fedha ya Tanzania. Miongoni mwa vyuo hivyo ni Chuo cha Kampala (Kampala International University) kilichopo Gongo la Mboto Dar es Salaam. Namwomba Mheshimiwa Waziri kuliangalia suala hili na kuweka utaratibu maalum na kuwalazimisha walipishe wanafunzi kwa pesa za Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usimamizi wa utekelezaji wa programu na miradi. Katika kitabu cha hotuba ya Mheshimiwa Waziri, ukurasa wa 67, 109 imeeleza namna inavyoendeleza kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES II). Huu ni mpango mzuri na napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa jambo hili. Napenda kumshauri Mheshimiwa Waziri, katika kutekeleza ujenzi wa majengo haya ya sekondari na hata yale ya primary ni vyema ikazingatia kujenga majengo hayo kwa kuzingatia kuwepo kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum ili na wao waweze kutumia majengo hayo bila ya usumbufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.