Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ili niweze kuchangia. Awali ya yote niungane na Waheshimiwa Wabunge kumpongeza Mheshimiwa Ummy kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa TAMISEMI, naamini kwa kushirikiana na Naibu Mawaziri wachapakazi kazi itafanyika vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na eneo la mapato ya halmashauri na katika eneo hili nizungumzie suala la ushuru wa huduma (service levy) ambayo ilikuwa ikilipwa na makampuni ya simu makubwa haya ya Vodacom, Airtel na tiGO. Kwa kipindi kirefu kulikuwa na shida kubwa kwamba, hizi kampuni kubwa za simu ushuru wa huduma (service levy) ulikuwa unalipwa kwa halmashauri moja tu ya Kinondoni pamoja na kwamba, hizi kampuni za simu zilikuwa zinazalisha mapato kutoka maeneo yote nchi nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, kulikuwa na tatizo kubwa kwamba, hizi kampuni za simu zilikuwa zinapata mapato kutoka Mbeya, Mwanza, Muleba, nchi nzima, lakini ushuru wa huduma ulikuwa unalipwa kwa halmashauri moja tu ya Kinondoni kwa sababu, eti makao makuu ya kampuni hizi yalikuwa yako Kinondoni na kwamba, sheria ilikuwa inasema hivyo. Ambayo ilikuwa ni very unfair kwamba, kampuni ina- generate mapato kutoka halmashauri zote na halmashauri hizo zinastahili kupata ushuru wa huduma (service levy) lakini ilikuwa inalipwa kwa Manispaa moja tu ya Kinondoni kwa sababu, makao makuu yalikuwa pale, hii ilikuwa ni very unfair. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana Waheshimiwa Wabunge tulijenga hoja na tukapitisha sheria kuanzia mwezi uliopita ambao unaendelea mpaka sasa kwamba, sasa hizi kampuni badala ya kuilipa Kinondoni kwa sababu, Kinondoni ilikuwa inanufaika inapata mpaka bilioni sita kwa mwaka wakati halmashauri nyingine hazipati hata shilingi, kwamba, badala ya hizi kampuni kulipa ushuru wa huduma kwenye halmashauri moja basi walipe ushuru wa huduma TAMISEMI, halafu TAMISEMI isimamie kuhakikisha inagawanya huu ushuru wa huduma ili halmashauri zote Tanzania ambazo na zenyewe zina minara ya simu zinazalisha mapato, zipate ushuru huu wa huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulisema kwamba, baada ya kampuni hizi kupeleka ushuru wao wa huduma TAMISEMI, TAMISEMI iwasiliane na TCRA ili TCRA iwape mchanganuo kwa sababu, TCRA inajua kwamba, hizi kampuni zimepata kiasi gani kutoka Mbeya, Mwanza au Nzega, ili kila halmashauri ipate stahiki yake ya ushuru wa huduma kwa mujibu wa mapato iliyo-generate kwenye halmashauri hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimefuatilia nimeona kwamba, ni kweli kampuni za simu sasa hivi zinapeleka ushuru wa huduma TAMISEMI, lakini TAMISEMI wanachofanya wanagawanya equal, kwamba, kuna Mamlaka za Serikali za Mitaa 185 kwa hiyo, wakipata yale mapato wanagawanya tu equally kwa 185 bila kujali mapato yaliyozalishwa katika eneo husika, ambayo haikuwa sheria tuliyopitisha. Kwa hiyo, niwaombe TAMISEMI sasa kwamba, hizi kampuni kubwa za simu zikishaleta ushuru wao wa huduma pale TAMISEMI, TAMISEMI iwasiliane na TCRA ili TCRA iwape mchanganuo kwamba, Mbeya wanastahili kiasi gani, Muleba wanastahili kiasi gani, Nzega wanastahili kiasi gani, Handeni wanastahili kiasi gani, Same wanastahili kiasi gani, ili kila halmashauri ipate stahili yake husika sahihi na wala sio kugawa equally. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivi kwa sababu, naona sasa hivi TAMISEMI pengine wanaogopa kazi au vipi wakilipwa hayo mapato kutoka hizi kampuni za simu wao wanagawanya tu equally, kwa hiyo, kila hlmashauri inapata milioni 10 au ngapi basi, wakati halikuwa lengo la sheria tuliyopitisha. Naomba TAMISEMI wafanye kazi ili kila halmashauri ipate stahiki yao. Nina uhakika mapato ya kampuni ya simu ya Mbeya hayawezi kuwa sawa na mapato ya kampuni ya simu ya Muleba. Mapato ya kampuni ya simu yanayokuwa generated Tanga hayawezi kuwa sawa na mapato ya kampuni ya simu yanayokuwa generated Nzega, kwa hiyo, lazima kazi ifanyike TAMISEMI wawasiliane na TCRA ili kila halmashauri ipate stahiki yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni TARURA, Waheshimiwa Wabunge wengi wameongea. Nataka niongezee tu hapo kwamba, kwa nini Wabunge wengi wanataka TARURA iwezeshwe ili iweze kuimarisha barabara, hasa za vijijini ni kwa sababu, barabara za vijijini zina impact, zinaathiri sekta nyingine za maisha kwa kiwango kikubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wengi wameongea, nilitaka kiongezee tu hapo kwamba kwanini Wabunge wengi wanataka TARURA iwezeshwe ili iweze kuimarisha barabara za vijijini ni kwa sababu barabara za vijijini zina impact, zinaathiri sekta nyingine za maisha kwa kiwango kikubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za vijijini wote tunafahamu kwamba watu wetu wengi wanaoishi maeneo ya vijijini shughuli yako kuu ni kilimo, na ili kilimo kibadilishe maisha yako maana yake ni bei ya mazao iwe nzuri, na hauwezi kupata bei nzuri ya mazao ukiwa maeneo ya kijijini kule Mashambani kama barabara ya kuyatoa mazao kule shambani na kuyafikisha sokoni itakuwa mbaya. Kwa hiyo, tunapozungumzia TARURA ipewe fedha iimarishe barabara za Vijijini tunazungumzia bei ya mazao na hali nzuri ya wakulima kule vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za vijijini zina athari kwa huduma nyingine kama Afya na Elimu, sisi maeneo ya kwetu kule maeneo ya kwa mfano Jimboni kwangu kule Bulende, Itumbili Siliaza wakati wa masika barabara hazipitiki kabisa, kwa hiyo hata wanafunzi hawawezi kwenda shule, kwahiyo tunazungumzia barabara lakini maana yake ni kwamba barabara hii TARURA wasipowezeshwa wakaifanya ipitike ina-impact inaathiri kwenye elimu kwasababu hata watoto hawawezi kwenda shule kwasababu mito inajaa, mabonde yanajaa watoto hawaweze kupita, kwa hiyo ni barabara lakini ni barabara ambayo ina-impact kwenye Elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unapokuwa na barabara vijijini kwenye vitongoji hazipitiki maana yake hata huduma ya Afya inaathirika kwa kiwango kikubwa tunasema akinamama wajifungulie zahanati wajifungulie kwenye vituo vya Afya kuna maeneo mengine wakati wa masika huwezi hata kupita kutoka kwenye kitongoji unachoishi kwenda kwenye zahanati, kwasababu barabara inakatika kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo ni barabara, ukiitazama unaona barabara lakini maana ni huduma ya Afya ina-impact kwasababu mwananchi, huyu mama mjamzito ambaye anatakiwa akajifungulie kwenye kituo cha Afya hawezi kufika ku-access kituo cha Afya au zahanati.

Kwa hiyo, tunaposema barabara za vijijini ziwe improved maana yake ni maisha bora ya wakulima kwa maana ya bei nzuri ya mazao maana yake watoto waweze kwenda shule, maana yake ku-improve elimu, maana yake hao wananchi waende wa-access wafike kwenye vituo vya afya na zahanati maana yake kui-mprove afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho ni kwamba huu mwaka wa fedha tunaokwenda kuumalizia ambayo imebaki miezi miwili halmashauri yangu ya Nzega iliidhinishiwa nilioni moja kwa ajili ya kujenga jengo jipya la Halmashauri kwasababu baada ya agizo la kwamba halmashauri za vijijini zilizokuwa mijini zihame sisi Nzega tulihama kutoka Nzega Mjini tukaenda Ndala, sasa kule Ndala tulipo sasa tunakaa kwenye madarasa ya Shule ya Sekondari ya Ndala pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, maana yake ni kwamba tunazuia hata ile shule sasa ishindwe kuandikisha wanafunzi kwasababu ndizo ofisi za halmashauri sasa hivi tupo madarasani. Sasa hiyo bilioni moja ambayo iliidhinishwa Mheshimiwa Waziri nikuomba kama kuna uwezekano lifanyike lolote linalowezekana tupate hiyo, tuanza kujenga ofisi. Ofisi tuliyokuwanayo pale mjini tumewaachia Halmashauri ya Mji, kwa hiyo tunakaa madarasani kwa hiyo kukaa kwetu madarasani tunazuia hata wanafunzi wasiweze kupata elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana hili kama Mheshimiwa Naibu Waziri ufanya kila linalowezekana hii miezi miwili iliyobaki hii bilioni moja tuliyoidhinishiwa iweze kutoka, Hamashauri ya Nzega tuhame kwenye madarasa, tupate jengo letu tuanze kufanya kazi. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, Baada ya kusema hayo naunga mkono asilimia 100, ahsante sana. (Makofi)