Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nakushukuru nichukue nafasi hii kwanza kumpa pongeza kwa kupata nafasi hii nzito, lakini tunaamini Mwenyezi Mungu atamuongoza na atamsaidia katika kazi zake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa Waziri kwa vile umeingia sasa wataalam halmashauri zetu nikisema wa nchi nzima wanahitaji wapewe training, training za innovation, training za teknolojia, training ambazo wataifanya Tanzania iweze ku-score zaidi kwenye human development index tunaboresha huduma za afya tunaboresha huduma za elimu lakini lazima kuwe na training za ziada ili waweze kufanyakazi vizuri na kuivusha nchi hii iwe sasa iende katika kutambulika katika HDI.

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kumpongeza Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam jipya yeye pamoja na Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam kwa kazi nzuri wanayoifanya na kuweza kukusanya mapato kwa 98% kwa mwaka takriban billion 60. Hakuna halmashauri yoyote katika nchi hii inayokusanya bilioni 60 kwa mwaka kama Jiji jipya la Dar es Salaam la Ilala ambalo lina Majimbo matatu ya Segerea, Ilala na Ukonga.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jiji hili bado barabara zetu ni mbaya nimesema kwenye swali lile la muda uliopita sitaki kuchukua muda mwingi kwenye suala la barabara. Tunalo tatizo kubwa sana tumerudishiwa kukusanya property tax, property tax hii tunarudishiwa kukusanya si mali yetu tunakusanya lakini mapato haya yanakwenda Serikali Kuu ambalo ni jambo zuri lakini gharama za kukusanya hatulipwi kuna running cost za mafuta, kuna running cost manpower, kuna running cost hela nyingi sana ambazo tunatakiwa tuzipate nimuombe Mheshimiwa Waziri hili alitazame ili tuweze kulipwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hilo jiji lilivyovunjwa halmashauri ya Manispaa ya Ilala ilikabidhiwa miradi yote na mali zote za Jiji la Dar es Salaam ambazo ziko katika paramita za Jiji jipya la Dar es Salaam parking fee ambayo ni halali ya kukusanywa na Jiji la Dar es Salaam tunagombania na TARURA, TARURA wanataka na sisi tunataka nikuombe tu Mheshimiwa Waziri uone umuhimu TARURA wakichukua hizi pesa hawazirudishi kuboresha hizi barabara. Kwa vile hawaboreshi barabara ni bora tuzikusanye sisi ili tuwape watengeneze barabara za Mkoa mpya wa Dar es Salaam kwa maeneo ambayo pesa hizi zinakusanywa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe sana Mheshimiwa Waziri ulitazame hili na mapambano ambayo tunapambana sasa hivi katika Jiji la Dar es Salaam kuhusu mapato. Mapato ya Jiji la Dar es Salaam Jipya kwa mwezi kwenye fee ya parking 1.1 billion shillings ni hela nyingi sana. Sasa hii ni halali ya wakazi wa Dar es Salaam si halali ya TARURA.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri nikuombe lingine TARURA wanafanyakazi vizuri sana wana wataalamu wazuri CO wao mzuri ma-engineer wazuri lakini hawana pesa. Pesa wanazopewa na Serikali wanapewa pesa za maintenance. hawapewi pesa za kutengeneza barabara nimeona kwenye vitabu sasa hivi kuna pesa zimetoka za maendeleo. Lakini naomba u-revisit na Hayati Rais Magufuli alitoa agizo siku alipokuja kufungua soko la Kisutu Jiji jipya la Dar es Salaam lipewe pesa zaidi za barabara ili uchumi ukue na tuweze kusaidia maeneo mengine nje ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Waziri pamoja na Serikali kwa ujumla, Waziri wa Fedha yuko hapa, fee ya ada ya simu, miaka yote tunapigania mapato ya simu, Ethiopia miradi mikubwa inaendeshwa na ada na tozo katika simu. Tukitoza shilingi 50 tuna-card holders wa simcard Tanzania sasa hivi zaidi ya milioni 52, tuchukue watu wachache milioni 30; only thirty milioni wale ambao wataweza kulipa shilingi 50 kwa siku we end up getting bilioni 540. Tutafute vyanzo vipya, TRA msidumae tu kukamata Bharesa, Mohamed Dewji, sijui Enterprises nani, tafuteni vyanzo vipya, there is a lot money kwenye simu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukitizama hii sintofahamu ya bando ambapo tumechukua kama mwezi mzima au wiki tatu fedha zimepotea. Hebu TCRA fanyeni forensic audit kwenye evarage users per kila mtu mtizame shilingi ngapi ambazo makampuni hayo yamechukua ili muweze kuwadai zirudi katika Mfuko wa Serikali na zilete maendeleo katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe masuala ya wananchi kulipa ada ya ziada ya simu ni uzalendo. Leo hatuandiki barua, hatuna gharama ya stamp, leo mtu yuko Mwanza anauliza soko la Pugu la ng’ombe ni shilingi ngapi, leo mtu yuko Mwanza anauliza soko la samaki ni shilingi ngapi, hii ni nafasi nzuri tuwe na kodi ya uzalendo. Tukisema shilingi 50 kwa watu milioni 30 tunaenda kupata bilioni 540. Tukisema tukiweka shilingi 100 kwa siku tunapata trilioni moja na bilioni themanini. Haya ni mapato ambayo yatasaidia kuchochea maendeleo ya nchi yetu na maendeleo ya Dar es Salaam na majimbo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali lazima ije sasa na mikakati ya kuboresha miundombinu. Nimeuliza swali hapa lakini naendelea kusisitiza kwa vile nina muda umuhimu wa kuboresha miundombinu ya Mkoa wa Dar es Salaam. Kibamba, Ukonga, Ilala, Segerea miundombinu ni mibovu, kuna maeneo hayapitiki katikati mjini. Leo tumeoneshwa wabunifu ambao wameshinda tuzo za Afrika, wanapokuja kupewa hizi zawadi, wale wanaokuja na hizi zawadi wanashangaa barabara za wabunifu Tanzania. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Serikali ione umuhimu wa kuboresha miundombinu hii. Fedha zipo, tubadilishe aina na namna gani ya kutafuta kodi za Watanzania. Fedha ziko nyingi sana tubadilishe mfumo wa kukusanya kodi ili sasa mapato haya yaweze kupatikana kwa wingi sana na yaweze kusaidia Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa DMDP II, ni mradi muhimu sana kwa Taifa na kwa Dar es Salaam. Mradi huu haupo Dar es Salaam tu, uko nchi nzima. Dar es Salaam inatajwa sana kwa sababu kwa sababu ni D inaanza na Dar es Salaam na mradi huu upo kwenye umwagiliaji, Kilimo, kuboresha masuala mengine ya utalii na vitu vingine. Kwa hiyo, naomba sana tuendelee kuboresha miundombinu tupate maendeleo katika Taifa letu. Tuboreshe Dar es Salaam, tuijenge Dar es Salaam ili iweze kusaidia mikoa mingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, biashara Dar es Salaam zimekufa, wafanyabiashara wa Dar es Salaam wanaondoka wanakwenda nchi zingine kufanya biashara sababu wanashindwa kupita kwenye barabara katikati ya mji. Jimbo la Ilala lina wakazi wengi wanasema wa chache ni kweli lakini kuanzia asubuhi saa kumi na moja mpaka saa tatu usiku tunaudumia watu milioni mbili katika kieneo kile, utaona uchumi ambao unaweza ukawa generated kwa watu wale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pengine nimkumbushe Mheshimiwa Waziri a-train watu wake katika innovation na teknolojia mpya waweze kuwa na uelewa mkubwa kwenye mambo ya afya, elimu na katika mambo mengine.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)