Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii na naomba nimpongeza waziri kwa hotuba yake nzuri na kimsingi ni kwamba ni mpongeze pia mtangulizi wake kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa miaka mitano.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka mitano iliyokwisha, Jimbo langu la Geita Mjini, lilijenga shule mpya za sekondari 13. Na likajenga shule mpya za msingi 13, maana yake tulipata shule mpya 26. Lakini katika kipindi chote hicho, mgao wa walimu ajira mpya umekuwa mdogo sana. naipongeza Serikali kwa kuziba mapengo ya walimu waliostaafu hizi ajira 6,000 ambazo imesema itatangaza hivi karibuni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kama Jimbo langu peke yangu lina shule 26 na sasa hivi najenga shule zingine nane maana yake ni kwamba walimu wanaokuja hawawezi kwenda kumaliza tatizo la walimu katika halmashauri zetu. Niiombe Serikali kwa sababu tulikuwa na hizi ajira 6,000 lakini tuna ajira zingine ambazo zilikuwa zimetangazwa na zikaacha kuajiriwa ni vizuri Serikali ikaajiri walimu wa kutosha katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, madhara ya kutokuwa na walimu kwenye shule ni makubwa sana. Huku juu ambako tunakwena watoto wanakwenda Chuo Kikuu, wanashindanishwa kwa ufaulu na ufaulu wao hauangalii historia kwamba huyu mtoto kwa bahati mbaya hakupata elimu ya kutosha kutokana na uhaba wa walimu alipokuwa sekondari. Na hata wakati mwingine, mikopo inaangalia aliyefaulu vizuri sana, sasa utaangalia shule ambayo ina walimu wanne na ina Watoto 600 ametoa mfano hapa Mheshimiwa Mbunge asubuhi, ipo kata yangu mimi form one walioanza mwaka huu wapo 850, lakini shule nzima ina walimu 32, na wanafunzi wengine wapo zaidi ya 2,000 utaona shule hii kama wanafunzi hawa wataendelea kufika form 4 na baadaye waende Chuo Kikuu hata kama watafaulu, hawataweza kushindana na wale ambao walikuwa kwenye shule yenye walimu wa kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna Watoto wana adhibiwa huko Chuo Kikuu kwa kuoneokana hawakufaulu vizuri lakini kwasababu ya mapungufu waliyoyapata walipokuwa sekondari. Niombe sana, wizara ituletee walimu wa kutosha. Kinachofanyika sasa tunaongeza idadi ya shule, tunaongeza idadi ya wanafunzi, tuna-deal na quantity na hakuna quality ya Watoto wanaomaliza shule. Tunaweza kufikiri tunafanikiwa lakini kimsingi tunapeleka kundi kubwa la watu ambao hawakupata elimu ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa spika, tatizo hili lipo pia kwenye afya, tumejenga zahanati mpya 24. Zahanati 24, zahanati unakwenda unakuta nurse peke yake. Mwaka juzi na mwaka jana tuliajiri madaktari, nikaamini sasa Serikali inakuja kuajiri hizi kada za kati ma-clinical officer na ma-nurse hawa katikati, lakini hizi kada zimekuwa zinaajiriwa taratibu sana matokeo yake sasa tuna zahanati nyingi tunajenga kila Kijiji, lakini zahanati ina mhudumu mmoja na huyo mhudumu akiugua zahanati inafungwa. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Waziri, najua hizi zinasimamiwa na TAMISEMI lakini inawezekana wanaoratibu ajira hizi wakawa ni wengine lakini uwepo tunahamasisha wananchi kujenga ni vizuri wakapata huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa kwenye mradi ambao ulikuwa unaitwa LGSP mradi huu ulikwisha na tukapata mradi mwingine unaitwa TACTICS wamesema wenzangu hapa. Taarifa tulizonazo ni kwamba fedha hizi tayari zipo, kinachotakiwa ni Serikali kutoa commitment ili pesa ziweze kutoka. Mazungumzo ya fedha hizi yalianza tangu mwaka jana tumeshirikishwa na wale wataalam waliokuwa wanakuja, ikaaminika zingesainiwa kabla ya bajeti hii haijapita, sasa tunaona mwaka wa fedha unaisha, hii miji 45 anbayo inahitaji pesa hizi ni muhimu sana Serikali ikatoa commitment ili tukaweza kupata fedha hizi zikaenda kusaidia watu wa TARURA.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, pale kwangu pale Geita Mjini barabara zote ni mbovu lakini mradi huu ukianza utachukua sehemu kubwa ya barabara za pale mjini na TARURA wata-deal na barabara zingine sehemu za vijijini. Hatujui ni kwa nini mradi huu unachelewa kuanza kwasababu wanaotoa fedha hizi walishatoa, fedha ziko Serikalini, Serikali inatakiwa kufanya commitment tu fedha ziweze kutumika. Miji 45 Tanzania itapata fedha.

Mheshimiwa Spika, tatizo kubwa ambalo tunalo hapa ni kuchelewa sana kufanya maamuzi. Kwa sababu tungechelewa kutafuta fedha, tumeshatafuta fedha tumepata, kufanya maamuzi ya kuzitumia fedha tunachelewa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, TARURA ilichukua ma-engineer wote kwenye halmashauri, Tanzania nzima ma-engineer waliopo kwenye halmshauri ni 84. Halmashauri tulizonazo ni 180 na kitu, kwa hiyo utagundua kuna upungufu wa ma- engineer 100. Lakini niombe, kwenye majeshi yetu huko hasa Jeshi la Ulinzi la Wananchi kuna ma-engineer kuna ma- engineer wamejaa. Badala ya kutuletea washauri wa Mgambo ambao hawana taaluma wachukue washauri wa mgambo ma-engineer wawapeleke kwenye halmashauri huko, kwenye wilaya tunaweza tukawaazima kwenye miradi.

Mheshimiwa Spika, amesema Mheshimiwa mmoja hapa, tunatumia force account, ubaya wa force account hakuna retention kwa hiyo inapotokea mradi ule umekosewa usitegemee kuna mtu atakuja kurekebisha, kwa hiyo lazima ufanyike kwa usahihi tangu mwanzo. Tunajenga majengo makubwa milioni 500, milioni 400 hakuna engineer waliopo ni ma-technician. Niiombe sana wizara, kama kuajiri itashindikana vipo vyombo vina ma-engineer waazime walete hao watu wafanye kazi kule hii ndo maana ya Serikali moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitoa ushauri kwenye TARURA. TARURA walipoundwa ilionekana kama chombo fulani hivi kinajitegemea, na matokeo yake kikajikuta huku halmashauri ni kama halmashauri hawahusiki. Kabla ya TARURA, Mkurugenzi alikuwa na uwezo wa barabara ikiharibika anatumia fedha zake kwenda kurekebisha barabara kwasababu kuna emergence. Leo mkurugenzi hawezi kwanini! kwasababu TARURA ni ka chombo fulani kanachojitegemea. Mimi nikuombe Mheshimiwa waziri, pitia upya muundo wa jambo hili, kama ni lazima hawa watu wapo halmashauri pale warudishwe halmashauri waendelee kuwa na pesa zao lakini warudishwe halmashauri waweze kushiriki, kusimamia na Madiwani na Kukaguliwa.

Mheshimiwa Naibu spika, Hii itawawezesha halmashauri wanapotoa fedha waweze kuamini kwamba tunawapa wenzetu. Leo mkurugenzi akitaka ripoti lazima aombe, Madiwani wakitaka taarifa lazima waombe, na huyu meneja wa TARURA wa wilaya ni kama karani kazi zote zinafanywa mkoani. Aliyeko pale hawezi kufanya chochote. Mheshimiwa hii imekata mawasiliano kabisa ya wawakilishi wa wananchi na matatizo ya barabara na unajua sehemu kubwa ya kura za Madiwani na Wabunge ziko kwenye barabara. Kwa hiyo nikuombe sana Mheshimiwa utazame upya huu muundo.

Mheshimiwa Spika, Kamati yetu ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ilipitia bajeti za mikoa, tumegundua kwenye asilimia 10 tumetunga sheria nzuri sana ya asilimia 10. Halmashauri nyingi zimetimiza agizo hilo, shida iliyopo hakuna ufuatiliaji wa kutosha wa fedha zilizokopeshwa, lakini hakuna utaalam wa kutosha kwenye halmshauri wa ku- manage fund kubwa.

Nataka kutoa tu mfano, Halmashauri ya Mji wa Geita inakusanya takriban shilingi bilioni mpaka bilioni 8, shilingi bilioni nane kwa mwaka. Fedha hizi ni nyingi sana, matokeo yake unatenga milioni 8 kwa miaka mitano unazungumzia takriban shilining bilioni 4, shilingi bilioni 4 tuliagiza kwenye Kamati zifunguliwe akaunti maalum zisiende kwenye general account maana yake kwa miaka mitano tuna 20 bilion. Lakini halmashauri zote, mikoa yote iliyokuja kuhojiwa hakuna continuation ya akaunti ya mwaka uliyopita na mwaka mwingine. Maana yake fedha hizi hazijulijani zikowapi? (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Constantine J. Kanyasu muda huu, malizia sentensi mbili, tatu.

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, ombi langu kwa kuwa tulisema halmashauri zifungue akaunti inayojitegemea, tunachotarajia sasa akaunti hii itakuwa inakuwa at time five years tutakuta kuna 20 bilion, kuna 10 bilion na halmashauri zitaacha kusubiri makusanyo ya mwezi kukopesha wananchi. Lakini kwa sasa fedha hizi zinapotea, hazijulikani ziko wapi, wanaokuja wanakuja na hesabu za mwaka jana hawaji na collection ya mwaka wala haijulikani wana shilingi ngapi. Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika. Ahsante sana. (Makofi)