Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa

Hon. Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa. Ofisi au Wizara hii ni muhimu san ana tunajadili bajeti ambayo imebeba hatma ya wengi kwenye nchi yetu. Kwa umuhimu wake ina mafungamano ya karibu san ana Wizara nyingi na Taasisi nyingi za Serikali.

Mheshimiwa Spika, tunapojadili Wizar aya Ofisi ya Rais Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa kuna kilimo humo ndani, kuna afya humo ndani, kuna uvuvi humo ndani, kuna barabara humo ndani, kuna afya na vitu vingi humo ndani. Kimsingi kwa muundo wa Ofisi hii ya Rais Tawala za Miko ana Serikali za Mitaa ndiyo ambayo inashuka mpaka chini kwa wananchi. Kwa hiyo, tunapoizungumzia Serikali kwa mwananchi wa kawaida tunazungumzia Halmashauri za Vijiji, Mtendaji wa Kijiji na Mwenyekiti wa Kijiji ambaye anaangukia katika Wizara hii. Kwa hiyo, tunazungumzia bajeti muhimu sana na utendaji kazi wa Wizara hii pamoja na majukumu yake kama yalivyoainishwa kutoka ukurasa wa tisa mpaka wa 15 inaonesha uzito na dhamana ambayo inaangukia katika Wiara hiyo.

Mheshimiwa Spika, wananchi wetu hawakumbani na Serikali mara kwa mara. Mwananchi wa kawaida kule kijijini anakutana na Seriali pale ambapo anahitaji huduma katika kituo cha afya, katika Ofisi ya Mtendaji Kata, katika Ofisi ya Afisa Elimu Kata ama Mwalimu Mkuu na hawa wote wanaangukia katika Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kule kwetu kwenye majimbo yetu ambako tunatokea, wananchi wana imani kubwa sana na Serikali hii lakini hiyo haiondoi ukweli kwamba kuna nakisi ya imani kwa Serikali za vijiji ama kwa kiingereza tunaweza tukasema kwamba public trust deficit kwa wananchi kitu ambacho kinatuweka kwenye dilemma kwa kiasi kikubwa. Kuna migogoro mingi ya ardhi, viwanja, mashamba yanagawiwa bila kufuata taratibu wala sheria. Kuna changamoto kubwa ya watu kuonewa kule bila kufuata sheria lakini hayo yote ukija kufuatilia kwa makini yanatokana na uwezeshwaji wa hawa watu. Je, wana elimu ya kutosha kulingana na majukumu ambayo wameyaomba? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watu wamechaguliwa katika nafasi zao kama Wenyeviti wa Serikali za Vijiji. Je, wamepata seminar ya jinsi ya kuongoza watu, sheria ambayo inaongoza mamlaka za vijiji na vitu vingine. Kwa hiyo, vitu hivi vinatusababisha katika migogoro mingi ambayo tungeweza kuitatua kama tungeangalia jinsi gani ya kuwawezesha hawa walau kuwapa elimu.

Mheshimiwa Spika, lakini pia hata uwezeshwaji wa posho. Imekuwa shida sana kwa Wenyeviti wetu wa vijiji kwa hiyo naomba wakati tunapitisha bajeti hii tuangalie ni jinsi gani tunaenda kuwaangalia hawa watu ambao ni muhimu sana. Mheshimiwa Chiwelesa amezungumzia kuhusiana na jinsi gani tumejiandaa na wimbi kubwa la watoto ambao ni graduates wa elimu bila malipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka huu watoto ambao wameingi akidato cha kwanza ni 800,872 ukilinganisha na watoto ambao wameingia darasa la kwanza 1,500,000. Sasa udahili wa watoto hawa ambao wanaingi akidato cha kwanza 800,000 haufanani san ana hawa watoto ambao wameingia darasa la kwanza 1,500,000. Kwa hiyo, ni rai yangu kwa Wizara ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kuangalia ni jinsi gani tunajiandaa na hii influx kubwa ya watoto ambao ni zao la elimu bila malipo ambalo linatokea 2022 ambapo ni mwakani tu. Kwa hiyo, tuna bajeti moja tu ya kujadili lakini bajeti ya 2022 tutakuwa na kazi kubwa ya kuangalia watoto hawa wanaenda wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo nilikuwa naomba kutoa rai Ofisi za Vijiji na Kata uendeshaji wake unategemea sana asilimia 20 ya ruzuku ambayo inatoka Serikali Kuu. Lakini wote sisi ni mashahidi vijiji vimekuwa vikihangaika jinsi ya uendeshaji wa ofisi zao lakini hata kata pia na kuna kata ambazo ziko mbali sana kimiundombinu na ofisi za Halmashauri lakini Watendaji hawa Kata, Watendaji wa Vijiji hivi wanaitwa kwenye mikutano inabidi wahangaike watoe hela zao za mifukoni lakini kuna fedha za ruzuku za Serikali Kuu ambayo asilimia 20 inapaswa kwenda lower level.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni rai yangu kwa Ofisi ya Rais TAMISEMI kuangalia namna bora ya kuhakikisha fedha hizi asilimia 20 za ruzuku zinaenda kule katika ngazi za vijiji na kata kurahisisha uendeshaji wa ofisi hizi ili kuondoa manung’uniko kwa watendaji wetu ambao ni muhimu sana katika utekelezaji wa maagizo na maelekezo ya Serikali Kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo nilikuwa naomba niunge mkono hoja ya Wabunge wenzangu ambao wametangulia kuhusiana na suala zima la barabara. Tunazungumzia kuhusiana na suala zima la uzalishaji wa viwandani lakini kimsingi unapozungumzia uzalishaji wa viwandani unazungumzia kilimo na katika majimbo ya pembezoni kama Mikumi, kilimo ndiyo uti wa mgongo na kuna maeneo mengi ya uzalishaji na ninaomba kupitia Bunge lako nitoe mfano wa Kata moja inaitwa Vidunda.

Mheshimiwa Spika, kata hii ni kilometa 5 tu kutoka pale Kidodi ambapo ni barabara kuu lakini ndiyo Kata ambayo inalisha bonde lote la hapa chini Ruaha, Mikumi, Kidodi mpaka Morogoro na Dar es salaam. Kilometa hizi tano huwezi kwenda kwa gari. Tangu nimezaliwa nilikuwa nashuhudia watu wakishusha mizigo na matenga toka enzi hizo mpaka sasa. Hali hii inafanana sana na kata nyingine za pembezoni kama Malolo, Ulening’ombe, lakini kuna kata za chini kama Tindiga ambao ni wazalishaji wakubwa sana wa zao la mpunga. Jan anilirusha clip kwa Mkurugenzi Mkuu wa TARURA na Maafisa wengine wa Wizara ya Ujenzi waone hali ilivyo. Ni umbali wa barabara kilometa mbili haipitiki hata kwa pikipiki, hali ni mbaya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunapozungumzia uchumi wa viwanda tunazungumzia bidhaa za kilimo, unapozungumzia bidhaa za kilimo unazungumzia suala zima la uzalishaji, usafirishaji, na ufikishaji wa mazao sokoni. Unapomnyima barabara mtu ambaye kazi yake kubwa ni kuzalisha kilimo maana yake tunahujumu uchumi wetu sisi wenyewe lakini unapandisha gharama katika uzalishaji na mwisho wa siku unampandishia gharama mlaji. Tunazungumzia hali ni ngumu, hali ni ngumu kimsingi inatokana na gharama ya bidhaa za kilimo masokoni ambayo tungeweza kuipunguza kama tungeweza kuboresha miudombinu. (Makofi)

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Dennis Londo.

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja. Nashukuru. (Makofi)