Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala Za Mikoa Na Serikali Za Mitaa

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nami napenda kuchangia kwenye Wizara hii ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ambayo ni wizara muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu. Nitajielekeza sana kwenye elimu na ni dhahiri kwamba kupitia elimu bila ada udahili wa wanafunzi kwa shule za msingi na sekondari umeongezeka, lakini kunakosekana mpango mkakati wa kuhakikisha kwamba kunatolewa elimu bora. Nitaenda kuainisha baadhi ya maeneo. Tumeshuhudia kuwepo kwa uhaba wa Walimu ambazo ni inputs nzuri sana kuhakikisha kwamba tunatoa products au output ya vijana wetu wenye elimu bora. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, uhaba wa Walimu mathalani kwa Mujibu wa BEST 2020, takriban walimu 50,000 kwa shule za msingi. Waliopo 191,000 na kitu na tunaambiwa hapa na waziri amesoma tuna wanafunzi milioni 11. Hasa unaweza ukaona Walimu waliopo wanaweza kukidhi kweli kufundisha kwa ikama inavyosema Mwalimu mmoja angalau kwa wanafunzi 45, unakuta wanaenda zaidi ya hapo. Tunajua kwamba kila mwaka au kila mwezi, kuna ambao wanafariki, wengine wanaacha kazi ya ualimu wanakwenda kwenye kazi zingine na huko nyuma waliondoa wa vyeti fake, lakini replacement katika kuhakikisha kwamba Serikali inakuja na mpango mkakati kuajiri Walimu wa kutosha ili kuweza kutatua changamoto ya Walimu haipo. Unakuta shule moja huko vijijini kuna Walimu sita, wawili, watano, wanafunzi 800 it’s quite unfair. Kwa hiyo hapa, niseme hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika Walimu hao pia ni dhahiri kwamba Walimu pamoja na kwamba wanakuwa na workload kubwa sana, lakini wana mazingira magumu sana, sana. Hawana nyumba, haa kama wamesema wanajenga hapa, lakini Walimu wengi hawana nyumba, lakini mazingira ya kufundishia pia ni magumu, wengine wanakaa kwenye miti, hawana ofisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia hawajapandishwa madaraja na kulipwa mishahara kwa muda mrefu kwa kipindi cha miaka mitano yote, wanatoa wapi motisha. Nikawaza sana, hapo zamani Walimu walikuwa na hardship allowance 150,000 I think, kama yalivyo kwenye upande wa majeshi, tufikirie sasa Walimu ni kada moja muhimu ambayo inaelimisha wanafunzi wetu. Tufikirie kurudisha hii angalau kuweza kuwapa motisha Walimu wetu, tuwape kila mwezi, katikati ya mwezi na wenyewe waweze kupata ile 150,000 ambayo walikuwa wanapata as a flat rate ili kuwapa motisha zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kingine ambacho nazungumzia kama kichocheo cha kuhakikisha tunapata elimu bora; miundombinu ya kujifunzia wanafunzi wetu. Madarasa yameendelea kuwa na uhaba sana. lazima tuje na mpango mkakati, tusikae kwa kusubiria matakamko, maana hapa juzi kati niliona Ubungo huko shule moja sijui inaitwa King’ong’o, ilitokea tafrani fulani wakaandika katika mitandao na nini, hayati akatoa tamko, within a week or two tunaona shule imekamilika. Sasa lazima Wizara ije mpango mkakati iwekeze kuhakikisha inatatua tatizo la madarasa nchi nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukipitia ripoti ya CAG, ameainisha pale kabisa kwamba uhaba wa madarasa out of eleven million or so wanafunzi, zaidi ya wanafunzi milioni tano point something hawana madarasa, kwenye ripoti ya CAG imeonesha. Vile vile hata miundombinu ya vyoo, ripoti ya CAG again nai-quote, imeonesha kabisa kwamba takriban wanafunzi 6,150,000 hawana matundu ya vyoo. Sasa bila hivi unakuta shule zetu zingine zinapelekea kufungwa. Hatuwezi kukaa tukasema tunatoa elimu bora while hatuna mazingira wezeshi kuhakikisha kwamba hii elimu bora inapatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, madawati, bado ni tatizo. Wanafunzi wanakaa kwenye mawe na hii ripoti ya CAG ime- quote walivyofanya ripoti ya ufanisi katika shule hizi, 1.1 wanafunzi wanakosa madawati. Tumesema elimu bila ada lakini unakuta wazazi wanachangishwa sana, anachangishwa kupeleka madawati, anachangishwa ajenge miundombinu ya darasa, ifike kwenye rental, anachangishwa hela ya mlinzi, anachangishwa 1,000 au 2,000 kuweza kulipwa Walimu wa ziada kufundisha wanafunzi wetu. So, it’s a burden, kama nchi lazima tujitoe. Wizara hii ikiamua kujitoa pamoja na Wizara ya Elimu tuwekeze, mbona kwenye uchukuzi tumeweza! Tunawekeza kule trillions of money, hebu sasa tuwekeze kwenye elimu, once and for all tuwe na Walimu wa kutosha, tuwe na madarasa ya kutosha, tuwe na maabara ya kutosha, tuwe na vyoo vya kutosha vyenye umeme, we are in science and technology era, tuwe na umeme kwenye mashule yetu, tuweze kuwa na computer and so called, tuweze kuwa na maji, vinginevyo hatutaweza ku-move popote kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine, kwenye elimu hapo hapo; ukiangalia NECTA kweli kupitia udahili huu, ukiangalia matokeo utasema ufaulu umeongezeka, lakini kiuhalisia ukiangalia tathmini ubora wa elimu unazidi kushuka. Ukiangalia watoto wanaofaulu kwa rank ya Division IV and Division. 0 ni wengi sana. Kuna tathmini imefanyika mathalani for last 10 years, Division 1 – 3 ni only 36%, the rest wanakuwa below that, sasa hatuwezi kukaa hapa tukasema tumejenga madarasa kweli, tume-enroll watu wengi shule ya msingi kupitia elimu bila ada lakini output out of it kama Taifa tunapata nini. Lazima tuangalie hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye quality assurance; udhibiti ubora wa elimu zetu, imekuwa ni kitendawili, bila kuwa na kitengo ambacho kinakuwa well equipped na human resources kwa maana Wadhibiti Ubora, kinakuwa well equipped na bajeti ya kutosha, hatuwezi kuwa na elimu bora. Nimejaribu kuangalia pale kwa mwaka wa fedha 2017/2018, Wadhibiti Ubora by then walikuwa 1,081 tu, mahitajio yalikuwa 1,541, deficit ya 460. Hata hivyo Bunge hili Tukufu limekuwa likipitisha hapa fedha; 2018/2019 tulipitisha 1.5 billion, kwa ajili ya hii Idara ya Udhibiti Ubora, lakini hakuna hata senti tano ambayo ilikwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2020/2021 Bunge lako liliidhinisha billion 25 kwa ajili ya kuimarisha Idara hii ya Udhibiti Ubora, lakini mpaka Machi by then 2020 hakuna hata senti tano imekwenda out of this 25 bilion. Kwa hiyo, tumeidhinisha hapa, nothing is being done, kama hakuna Wadhibiti Ubora wa kwenda kuhakikisha kweli elimu inayotolewa ni bora, tunafanya mark time tu kama Taifa. Kwa hiyo tuhakikishe tunawapeleka Wadhibiti Ubora wa kutosha, tuhakikishe tunaweka bajeti ikipitishwa hapa inaenda, kuhakikisha kwamba wanapata miundombinu imara kwa maana ya magari na kila kitu kwenda kufanya ukaguzi huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, muda unaenda, lakini kingine ambacho nilisema nitagusia, ni hili suala la elimu jumuishi kwenye shule zetu. Limekuwa likiongelewa hapa nashukuru wame-quote, kwa hiyo shule zetu hizi lazima pia tuwe na miundombinu rafiki ambayo inawezesha wenzetu mathalani wenye ulemavu kuhakikisha kwamba na wao wanapata elimu stahiki. Kama tunajua tuna shule na zingine zinachangamana kwa mfano shule ya msingi pale Buhemba Tarime, inachangama na watu wenye ulemavu. Wengine wenye uono hafifu, usikivu na watu wenye ulemavu wa akili, unakuta wapo pale, lakini Serikali haipeleki Walimu wa kutosha, haipeleki miundombinu stahiki kwa hao watu ili na wenyewe waweze kupata elimu kama wenzao wanavyopata. Pia hata miundombinu hii tunayojenga, mathalani kwa watu wengine wenye ulemavu haina zile njia za kupita wao, kuhakikisha kwamba huyu mtu mwenye ulemavu anaweza kuwa-accept. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia katika shule za msingi na sekondari, watoto wa kike wengi wanaacha kwenda shule between four to five days mpaka six days wakiwa wameingia kwenye menstrual period, wanashindwa kuwa na usaidizi mathalani, anashindwa kuwa usaidizi na hili tumelipigia sana kelele Mheshimiwa Ummy Mwalimu anajua tangu akiwa Waziri wa Afya unajua. Tunataka kujua katika ile ruzuku ambayo inakwenda angalau waweze kutenga extra, waweze kuainisha, mathalani katika shule ya msingi wanajua watoto waliofikia umri wa kwenda kwenye hii kitu wako labda 200 au sekondari wako wangapi, waweze kupeleka extra katika hayo. Pia na hao watu wenye ulemavu waweze kuwa wanaongeza ku-catch hiyo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ESTHER N. MATIKO: Dakika mbili Mheshimiwa Spika nimalizie. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, dakika mbili tu. Katika hili la ruzuku ya 10,000 tumekuwa tunashuhudia inabaki 4,000 kama retention ambayo inatakiwa Serikali inunue vitabu, lakini for right four years haijawahi kupeleka hivyo vitabu na ukifanya calculation, nilikuwa nafanya haraka haraka hapa, kwa mwaka wanabakisha over 44 million, kwa miaka mitano karibu milioni 220. Tukienda mashuleni, tunaona bado kuna uhaba wa vitabu kwa hawa wanafunzi. Kwa hiyo kama Serikali wakibakisha hizo fedha wanaona ni ngumu kupeleka, bora ziende kule, Mwalimu husika aweze kuwajibika kuweza kununua hivyo vitabu kuliko kubaki huko Serikalini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)