Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon Toufiq Salim Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. TOUFIQ SALIM TURKY: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, naomba nichukue fursa hii nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan tungali sote salama. Pia tuwatakie rehema waliotutangulia mbele za haki wazee wetu hususan Hayati Rais mpendwa wetu Magufuli.

Mheshimiwa Spika, haijapata kutokea mabadiliko ya Serikali ya namna hii na sisi wananchi na Serikali kwa ujumla, sote tukawa kitu kimoja. Lazima tumshukuru Mwenyezi Mungu Subhanah-Waatalah. Pia na Waheshimiwa wengine tukawa tunajiuliza, Hayati Dkt. Magufuli Waziri Mkuu alimtolea wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli katika kubarikiwa huku, tumebarikiwa kupata kiongozi aliyekuwa mtumishi mtiifu mno. Katika kubadilika kwa Serikali hii, kiungo kikubwa bado kingalipo. Kwa hiyo, tuendeleeni, ilikuwa Bunge hili hili tukampitisha kwa kura zote kabisa, kwa heshima zote kabisa, kwa hiyo, tuendelee kushikamana na Serikali yetu kuhakikisha uchumi wetu unaendelea kuwa mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumwombee sana Rais wetu wa sasa Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, Mwenyezi Mungu ampe hekima, busara na maono (maana viongozi huwa wanapata maono) yale ya kuipeleka Tanzania yetu mbele kama waasisi wa nchi hii walivyokusudia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda sana kuongelea kwa uchache katika suala zima la uwekezaji. Uwekezaji hauwezi kupatikana ndani ya nchi yetu kama elimu hatujaipa kipaumbele. Hivi karibuni nilipata bahati ya kwenda Kenya nikakaa na viongozi wa pale, katika masuala waliyokuwa wanaongelea wakasema Tanzania sisi tunaionea wivu sana, kwa sababu wana rasilimali za kila aina kuliko sisi; lakini sisi tuna rasilimali moja ambayo Afrika nzima hawana, ni rasilimali nguvu watu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, literate level ya Kenya ni 93%. Vile vile elimu yao wanasema ni tofauti na elimu ya watu wengi sana. Afrika watu husoma kwa ku-pass, sisi tunasomesha vijana wetu kwa kufahamu. Mara nyingi sana, ndiyo maana utaona Tanzania hapa tuna ma-degree, wengine wana Masters, wengine Ma-professor, lakini inapokuja katika uelewa na katika suala zima la dunia inavyoenda, exposure ni tofauti. Attitude yetu iko mbali. Ndiyo maana katika suala zima la uwekezaji, watu wanatafuta ma-expatriates. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niliona Wabunge tunavutana sana katika suala la kwa nini tunachukua watu kutoka nje? Hakuna mtu anataka kutoa gharama mara tatu, mara nne, mara tano kuwalipa watu wa nje na wakati Watanzania wapo, lakini bado vijana wetu wako nyuma mno kielimu. Tunafanyaje sasa katika suala hili? Ni lazima turudi tena, tutazame namna gani tunaweza kuwasaidia wanafunzi wetu kuhakikisha wanaendana na matakwa ya dunia ya sasa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Armania ni Eastern Europe Country, sasa hivi kuanzia Darasa la Sita wanafundisha subject ya coding; masuala ya software. Miradi yote karibu sasa hivi watu wanasema tunataka sisi tuwe na mfumo, lakini mifumo yote inatoka nje ya nchi. Hizo ndio ajira za baadaye. Watu duniani wanakadiria, ndani ya miaka 10 ijayo akili zetu zitakuwa hazifanyi tena kazi, itakuwa ni suala zima la artificial intelligence. Vijana wetu tumewatayarisha vipi kuhakikisha ajira za baadaye hatuzikosi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ajira za mwanzo zilikuwa za viwanda, tunatafuta watu wa kulima. Ajira za pili zikaja kuwa ni masuala mazima ya vibarua kwa ajili ya viwanda. Ajira za tatu zimekuja katika kutengeneza viwanda. Ajira zijazo ni namna gani dunia itaenda ki-ICT only; Artificial intelligence? Vijana wetu tuwatayarisheni katika ajira za baadaye. Hizo milioni nane zitakuwa ndoto. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)