Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA; Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii nichangie kidogo kwenye hii bajeti ya Ofisi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa dakika ni chache sana na mimi nitaongea machache mengi wengi wameshazungumza. Kwanza, naunga mkono hoja asilimia 100.

Mheshimiwa Spika, naomba kama mimi binafsi au mtu wa maadili nitoe ushauri kidogo. Kuna madeni mengi ambayo yamekuwa yakizungumzwa; madeni ya wakandarasi mbalimbali ambayo yanaongezeka kila siku kwenye sekta ya ujenzi waangalie namna gani watapunguza madeni haya kwa sababu kila siku kuna shida lakini Ofisi ya Waziri Mkuu inafanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, nilisema nitatoa ushauri wa kimaadili kidogo. Ni vizuri kumsema mtu akiwa yupo ili aweze kujibu lakini unapomsema mtu hayupo na hawezi kujibu kunakuwa na mashaka na ndimi mbili huwa si nzuri. Nchi sasa hivi imetulia sana huko nje maana yake wananchi wana imani na Serikali iliyopo ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan. Sasa wanaanza kutokea baadhi ya Waheshimiwa wenzetu kuponda vitu ambavyo vilifanywa katika awamu iliyopita, si vizuri. Kama kitu ulikisifia jana, leo ukaanza tena kukiponda wananchi wanachanganyikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, miradi yote hii iliyoanzishwa ndiyo ilitufanya Wabunge wengi turudi leo humu Bungeni nikiwemo na mimi. Unafahamu kwamba Tabora Mjini haijawahi kurudisha Mbunge mara mbili ni mimi niliyesimama hapa Mwakasaka, ni kwa sababu ya mafanikio ya Awamu iliyopita chini ya Mheshimiwa Hayati Dkt. Magufuli pamoja na Mheshimiwa Mama Samia. Miradi ile ile iliyotupitisha leo tunapoanza kuiponda tunawachanganya wananchi.

Mheshimiwa Spika, tusiwe na ndimi mbili na hata kwenye Biblia sijafahamu ni kitabu gani lakini nadhani ni Mithali, Mwenyezi Mungu anasema kheri uwe moto au baridi, ukiwa uvuguvugu utatapikwa maana yake huna msimamo. Tuwe na msimamo, wananchi wana imani na Serikali iliyopo ya Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, tusiwachanganye kwenye miradi ambayo inaendelea. Bahati nzuri Mheshimiwa Samia ana uwezo mkubwa, miradi hii itaendelea na tuna imani kabisa kwamba nchi yetu itasonga mbele. Tuache kuwachanganya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi yangu ni machache tu, naunga mkono hoja. (Makofi)