Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri na Watendaji wote wa Wizara hii kwa hotuba yake nzuri na naunga mkono.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Wanging‟ombe haina shule kidato cha tano na sita pamoja na shule za Mount Kipegere, Makoga, Wamihe na Wanging‟ombe kukidhi vigezo vyote vya kuanza masomo ya high level. Naomba Waziri alitolee maamuzi yanayostahili. Pia shule za Philip Mangula, Maria Nyerere, Mt. Kipegere, Makinga, Wanike, Wanging‟ombe, Igachunya, Luduga, Saji, zinayo mabweni na hivyo zipandishwe hadhi ya kuwa shule za bweni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Wanging‟ombe ina upungufu mkubwa wa Walimu katika shule za msingi na sekondari. Kwa upande wa elimu ya sekondari hatuna Walimu wa hisabati na masomo ya sayansi. Naomba Wizara hii ituangalie kwa jicho la huruma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujengewa Chuo cha Ufundi cha VETA eneo la Soliwaya - Wanging‟ombe kwani hatuna hata chuo kimoja kwenye Wilaya hii ya Wanging‟ombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu ya awali kwa shule nyingi imekosa Walimu wa kufundisha kutokana na upungufu wa Walimu. Tatizo hili limetokana na hivi sasa wazazi kuacha kuchangia kuwalipa Walimu hawa kwa hiyo, Serikali ione maana ya kuelimisha kuhusu uchangiaji kwa maeneo yenye mahitaji kama hili la upungufu wa Walimu na hasa elimu ya awali.