Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napongeza Mawaziri na Watendaji wote katika Wizara kwa kuwasilisha hotuba ya makisio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ubora wa elimu na ualimu. Tumeshuhudia zaidi ya miaka kumi mitaala mingi ikifanyiwa mabadiliko ambayo yameleta shida kwa wananchi kwani ubora wake umeshuka ukilinganisha na miaka ya nyuma. Vilevile kozi ya ualimu imekuwa haizingatii viwango hasa vyuo vya watu binafsi. Walimu katika shule za Serikali na binafsi hawazingatii taratibu na kanuni katika utendaji hivyo Wizara iangalie namna ya kuboresha kanuni ziendane na wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi. Katika hotuba ya Waziri hakutaja Chuo cha Maendeleo ya Wananchi cha Msaginya kilichopo Halmashauri ya Wilaya Nsimbo, Mkoa wa Katavi. Taarifa za hivi karibuni ni kuwa kimehamishwa toka Wizara ya Afya. Chuo hiki kina matatizo mengi kuanzia rasilimali watu, miundombinu na madeni ya wakandarasi ambao wamesimama kazi kwa sababu hawajalipwa. Hivyo tunaomba Wizara ifanye malipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mafunzo kwa vitendo. Katika kuongeza ujuzi wa wanafunzi, tunashauri Wizara iboreshe mwongozo wa mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa kuanzia mwaka wa kwanza kushiriki mafunzo haya ili kuwajengea uwezo mzuri wa kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Mikopo. Wizara inahitaji kuboresha utendaji wa Bodi ya Mikopo na hasa kuwawekea malengo kwa kukusanya madeni toka kwa wanafunzi ambao wanadaiwa. Pia muda wa kulipa upunguzwe tena kwa kuwa fedha inahitajika kusaidia wengine na kuondoa mzigo kwa Serikali kutoa fedha kila mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mitihara elimu ya juu. Ili kuboresha elimu ya vyuo vikuu nchini tunashauri Wizara itoe mwongozo juu ya mitahara (course outline) zenye kuendana na hali ya sasa na pia ziwe zenye ubora na kufanana ili shahada, stashahada zipate ubora duniani.
kusahihisha uwe unashirikisha mtu zaidi ya mmoja (panel) kuondoa rushwa za aina mbalimbali kwa wanafunzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ruzuku vyuo binafsi vya ufundi. Tunashauri Serikali iangalie namna ya kutoa ruzuku kwa vyuo binafsi vya ufundi ili kuviwezesha kutoa elimu bora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.