Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii inahitaji kufanya marekebisho ya msingi katika mfumo wetu wa elimu na mafunzo nchini.
Naomba Mheshimiwa Waziri asome kwa makini sana Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii, Hotuba ya Kambi ya Upinzani kwa Wizara hii na ripoti ya Profesa Mchome ya mwaka 2013 kufuatia mass failure ya watoto wetu katika mitihani ya Form IV mwaka 2012. Naamini hizi zote zitamsaidia katika kazi nzito iliyo mbele yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba Mheshimiwa Waziri alipitie upya suala au sakata la TCU na wanafunzi wa Chuo cha St. Joseph. Kwa kiasi kikubwa tatizo liko katika utaratibu ambao Serikali imeuweka. Mabaraza yetu ya NACTE, NECTA na TCU yanatakiwa yafanye kazi zao kwa kuzingatia mipaka yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiutaratibu vyuo viilivyo chini ya NACTE vinadahili wanafunzi waliopata minimum ya D nne (4) katika mtihani wa form four kwa kozi ya NTA 4 katika chuo chochote. Wanafunzi waliofukuzwa St. Joseph College wamekidhi hili. Tatizo liko wapi? Kupata diploma watasoma miaka mitatu na wakiendelea mpaka digrii watalazimika kusoma miaka mitano, hili ndilo walilokuwa wanafanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia kusema Mheshimiwa Waziri apitie kwa makini taasisi zilizo chini ya Wizara yake ili kuitendea haki nchi yetu na hasa vijana wetu. Lazima iwepo nidhamu na utaratibu maalum kwa taasisi zetu wakati wanatekeleza majukumu yao. Pamoja na nidhamu, uadilifu ni muhimu zaidi. Vijana wetu wengi wameharibiwa maisha yao au ndoto zao kwa maamuzi ya NECTA kwa miaka mingi na sasa tunashuhudia hili la TCU.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.