Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii kuchangia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Awali ya yote niungane na watanzania wengine wenzangu waliotoa shukrani na pongezi zao kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa hiyo, kwa niaba ya wananchi wa Chakechake, natoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ninatoa ahadi ya kwamba tupo nyuma yake tuna muunga mkono na tutampa kila ushirikiano atakaouhitaji kutoka kwetu Mungu amtie nguvu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili ni shukrani kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuleta hotuba iliyoshiba, iliyosheheni ambayo inaakisi maono ya Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia hotuba ambayo imechukua mtazamo na mwelekeo wa Mheshimiwa Rais mpya aliyekuwa madarakani Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, (Makofi) (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuchangia kwenye mambo mawili kwenye hii hotuba, jambo la kwanza ni structure ya utoaji wa mikopo iliyopo sasa. Moja katika maeneo ambayo tunajisifia sana I feel very proud ni legacy iliyoachwa na Rais Hayati Dkt. Magufuli kwenye ujenzi wa zahanati zaidi ya 1,198 nchi nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa tuna idadi ya zahanati zisizopungua 5,900 Tanzania, hili ni jambo zuri na la kuwa mfano kila mahali, tuna vituo vya afya visivyopungua 666 Tanzania nzima, kwenye uhai wa Mheshimiwa Magufuli kulijengwa vituo vya afya visivyopungua 487 Tanzania nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunachokikosea kama Taifa ni kwenye recruiting ya wafanyakazi au watendaji au wahudumu wa kwenye hivyo vituo vya Afya. Wahudumu walivyo sasa hivi ki-structure tunahitaji ma-clinical officer wengi zaidi na ma-clinical officer ni hawa vijana wenzangu ambao wanasoma diploma za clinical officer kwenye vyuo mbalimbali vya elimu Tanzania ambao ndio hawapati mikopo. Mikopo sera yake ya elimu ya juu, mikopo wanapewa ma-MD ma-medical officers ambao wanaanza degree na kuendelea ambao hao baadae hawataki kwenda kukaa kwenye zahanati na vituo vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hawawezi kwenda kuishi huko vijijini mtu akishakuwa na degree yake yaani hataki kwenda kuanzisha Maisha kwenye zahanati anajiona kama ni kudogo sana kwake. Kwa hiyo, watu ambao tunawahitaji wakae kwenye zahanati zetu hizi zaidi ya 5900 na vituo vya afya zaidi ya 666 ni ma-clinical officer ambao wengi wao wanaanza na hatua ya elimu ya diploma kwenye vyuo vya afya mbalimbali, ambao ndio hawapati mikopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu hapa ni kwamba lazima tutengeneze sera sasa. Aidha tubadilishe au tubadilishe sheria ili hawa watu wakopesheke wapewe mikopo ya elimu ya juu ili wasome wawe wengi wakatusaidie kwenye hizo zahanati zetu. Maana yake tukiwa tunajenga zahanati nyingi lakini mwisho zikiwa zinakosa watendaji hiyo itakuja kuwa kazi bure. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huo ni upande mmoja upande wa pili au jambo langu la pili ambalo nilidhamiria kulichangia ni kwenye sekta ya utalii, wakati nachangia hotuba ya Mheshimiwa Rais aliyekuja kuitoa hapa madarakani Hayati nilitoa mchango wangu kwenye jambo hili, leo nataka niongeze zaidi. Kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi yenye page 303 kwenye page 207 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ilani inampa task kazi ya kuhakikisha anakuza pato la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia utalii kwa kuongeza idadi ya watalii kutoka 500,000 hadi 800,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, ilivyo sasa hivi wastani wa watalii wanaoingia Zanzibar kwa mwezi ni kati ya 40,000 hadi 50,000 statistic niliyonayo hapa kwa Tanzania Bara kwa mwaka 2020 hadi 2021 kumetembelewa na watalii wasiopungua 620,000, maana yake hiyo ni idadi ya watalii wanaoingia Tanzania kwa mwaka mmoja tu kwa Tanzania Bara, ambao ni task aliyopewa Rais wa Zanzibar kwenye Ilani kwa muda wa miaka mitano kuifikia. Sasa ninachotaka kushauri hapa kuna umuhimu tena umuhimu mkubwa wa kufanya kazi kwa ushirikiano baina ya Wizara ya Utalii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wizara ya Utalii ya Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naona huwa haiingii akilini na haiko vizuri ikiwa mgeni anafika Zanzibar anakaa siku saba anaondoka kurudi Ulaya hajafika bara, au anafika bara Ngorongoro anatua KIA ana-spend anaondoka baada ya siku saba hajafika Zanzibar. Wakati anakuja Tanzania ilivyo ni kwamba mifumo na ushirikiano baina ya Taasisi hizi ni kama haupo vizuri kidogo labda kuna zile sentiment za kwamba hizi taasisi sio za Muungano lakini sisi tunafanya kazi kama Taifa tunatakiwa tushirikiane ili kusaidia Taifa hili likipata pato lipate kwa jumla yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nataka kuunga mkono hoja na huo ndio ulikuwa mchango wangu kwenye sehemu mbili ahsante sana naomba kuwasilisha. (Makofi)