Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Waheshimiwa Wabunge wenzangu tumeondokewa na Rais mpendwa Mungu amuweke pema, mwanamme mashine. Tumempata mwanamke mashine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tumpe nguvu, tumuombee dua atimize majukumu yake. Mheshimiwa Rais Samia ameshaanza kuonesha mwanga kufuata nyayo za Mheshimiwa Magufuli, tumsaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Afrika lazima iamke kwenye natural resources ambazo Mungu ametupa katika Bara hili la Afrika. Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema the enclave nature of mining industry can limit the trickle down of benefit unless sovereign government participate fully in managing extract industries, kitu ambacho mara nyingi nchi za Afrika na sisi vilevile bado hatujafikia kiwango kizuri cha ku-manage migodi yetu na natural resources ambazo tunazo. Pamoja na marekebisho ya sheria tuliyofanya ambayo tunapata 16% lakini bado tuna haki ya kumiliki migodi hii kwa 100%, kwa kufanya sisi wenyewe kazi ya ku-extract industries za migodi nchini mwetu Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nilikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kuchunguza madini ya almasi na tumeona wawekezaji wa madini haya hawana ujanja mwingine wowote zaidi ya kutumia madini haya kama dhamana. Serikali yetu inaweza na wao tukatumia madini yetu haya yawe dhamana ya kupatia mtaji na hawa wataalamu tukawakodisha na tukawaajiri na wakawa wafanyakazi wa Serikali. Ni hatari kubwa sana kuacha mali hizi zinaondoka wakati sisi Tanzania hatupati market value ya extract industry ya mining katika nchi yetu. Tunapata pesa kidogo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo dhahabu ni zaidi ya Dola 2,000 tujiulize katika hizo Tanzania tunapata ngapi? Tunachokipata ni kidogo sana, lazima tubadilike na sasa tu- run sisi wenyewe migodi hii. Najua kuna cartel kubwa sana ya multinational companies kutotaka nchi za kiafrika kuendeleza migodi yao wenyewe. Wanataka lazima waje wao wadanganye kwenye masuala ya mengi sana hasa kwenye operation cost.

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima Serikali, najua kuna vitengo katika idara zote ambazo zinaangalia operation cost waongeze umakini na ujuzi. Katika Mgodi wa Mwadui tuligundua mtambo unaandikwa dola milioni 8 kumbe mtambo umenunuliwa kwa shilingi milioni 5 Tanzania hapa hapa. Kwa hiyo, vitu kama hivi vinaongeza operation cost kuwa kubwa na kufanya faida ya Serikali kupungua, lazima tuamke. Pia lazima tuwe na sehemu ya National Revenue Management Schemes such as Stabilizing Funds inflected cost of projects. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tuhakikishe mali ya Tanzania na Afrika kwa ujumla inalindwa na inaendeshwa na Watanzania wenyewe. Siri kubwa ni kuweka dhamana migodi tufanye wenyewe, tusiwape wawekezaji, wao waje na teknolojia tuikodishe, tuwalipe mishahara wabaki kama wafanyakazi wa kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye ATC inajitahidi kutoa huduma na kufanya kazi vizuri. ATC haiwezi kupata faida au kujiendesha kwa ununuzi wa ticket. ATC kama ni national carrier lazima Serikali iwapunguzie baadhi ya operating cost. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndege ya Shirika la Ethiopia hailipi landing fee, parking fee, navigation fee, hailipi gharama nyingi sana wanapunguziwa au kufutiwa ili kuwasaidia wakue. Sasa ATC ina gharamia gharama zote hizi, inafanya kupunguza mapato yao. ATC hii mpya chini ya Mheshimiwa Matindi, 100% mishahara ilikuwa inalipwa na Serikali leo Serikali inatoa only 17%, inaonesha wanaanza kuja na wakianza kusaidiwa watakuwa vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndege hazitakiwi kukaa chini ya ardhi, anayepumzika ni rubani na crew, ndege inaruka twenty-four seven. Sasa kama hatuna viwanja vyenye ubora wa ndege kuruka usiku, Serikali lazima iwekeze. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa Dodoma zimewekwa taa intensity yake haiwi-controlled na Control Tower ambapo siyo jambo la kawaida. Hii inaweza ikaleta madhara wakati wa giza nene taa zisiweze kuwaka vizuri kama Control Tower hawawezi ku-control intensity ya taa zile.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi naomba tuboreshe viwanja vyetu, hapa Dodoma waweke Vertical Approach Slop Indicators (VASI) na ILS ambayo inasaidia hata kwenye mawingu ndege zinatua. Mara nyingi tu ndege za ATC zinarudi sababu zinashindwa kutua. ILS ni chombo ambacho kinaleta usalama kwa abiria, kwenye kiwanja na kwenye ndege. Uwanja wetu huu sasa hivi unapitiwa na watu wengi sana lazima tuboreshe viwanja vyetu kuwe na usalama wa hili shirika letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kuhusu mradi wa DMDP, Mkoa wa Dar es Salaam. Naomba Serikali iendelee kufanya maamuzi, Dar es Salaam 2025 itakuwa na population ya watu milioni 10. Deni lolote ambalo Serikali imelikopa kwa niaba ya Mkoa wa Dar es Salaam linalipika kwa michango na uchumi ambao Dar es Salaam wanao.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine huu ni mwezi wa Ramadhan tende jamani siyo chakula cha Waislamu, tende ni chakula alikula Yesu Kristo na katika vyakula alivyopenda Yesu Kristo ilikuwa tende na mkate wa mana. Ukisoma Wagalatia 5:22-23, chakula cha kwanza ambacho kina spirit tende imetajwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivi sababu Waislamu wako katika mfungo na tende hizi ni sadaka, Serikali ifikirie kutoa ushuru wa tende ili wananchi wa dini zote waweze kula tende. Wakristo wale tende sababu Yesu kala, Waislamu wale tende sababu Mtume Muhammad naye amekula. Kwa sisi Waislamu ni suna na kwa Wakristo ni suna. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mkisema Waziri haruhusiwi kubadilisha sheria tumeanzisha mtindo wa force account. Force account ni uwekezaji au utendaji wa kazi unaofanywa bila kulipa VAT. Kwa hiyo, tende nazo vilevile Waziri aseme tu tunaruhusu, itoke executive order tende ziruhusiwe bila ushuru tupate kula tende, tupate kufuata suna za Mitume wetu waliopita. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na tende hizo ukitizama wana wa Israel walivyotoka kwa farao walivyoingia jangwani ukisoma Exodus 15:27 chakula chao cha kwanza ni tende. Kwa hiyo, naomba Serikali ili nchi iendelee kuwa na neema ruhusuni tende bila ushuru ili Waislamu na Wakristo tule tuweze kupata neema za Mwenyezi Mungu. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye suala la wafanyabiashara, Serikali mmekaa sana na wafanyabiashara…

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili imeshagonga, ahsante sana.

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)