Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya tele na kuweza kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Kibiti, nawaahidi sitowaangusha, naomba ushirikiano kutoka kwao, Hapa Kazi Tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia hotuba hii ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi. Kwanza nampongeza Waziri mwenye dhamana, Mheshimiwa Profesa Joyce Lazaro Ndalichako pamoja na Watendaji wake wote wa Wizara husika kwa kazi yao nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mitaala ya masomo haiendani na changamoto ya maisha ya kila siku. Napenda kuishauri Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi kufikiria kurudisha mitaala kama ilivyokuwa zamani ya sayansi kilimona sayansi kimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Rais wetu mpendwa, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kutekeleza ahadi yake ya elimu Bure. Katika Jimbo langu la Kibiti wazazi wameitikia kauli hii kwa kupeleka watoto wengi kuandikishwa katika shule zangu za msingi. Japokuwa zipo changamoto, naamini huu ni mwanzo tu yote yataisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishauri Serikali yangu sikivu inayoongozwa na Chama cha Mapinduzi kulipa madeni yote ya Walimu, kuwapandisha madaraja kwa wakati, kuwalipa madai yao ya likizo, kuwalipa posho ya mazingira magumu kama kwenye Jimbo la maeneo ya Kibiti, Delta, Mfisini, Mbwera, Kiongoroni, Maparoni na kadhalika
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimba za utotoni. Napenda kumshauri Waziri wangu mchapakazi wa Wizara hii kuangalia suala hili kwa umakini. Moja, aboreshe mazingira ya shule na yawe karibu na makazi ya wananchi.
Pili, mtoto akipata ujauzito baada ya kujifungua apewe kipaumbele cha kurejeshwa tena shuleni. Tatu, kuhakikisha tunajega mabweni ya kutosha katika shule zetu za sekondari zote za kata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuyapongeza mashirika ambayo si ya Kiserikali jinsi yanavyochangia sekta hii ya elimu. Nalishukuru shirika la CAMFED jinsi linavyotusaidia kwenye suala hili la elimu katika Jimbo langu la Kibiti na wananchi wote tunawaunga mkono.