Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria ambaye, leo yuko kwenye majukumu mengine, ningependa nami kuupitia na kutoa mchango unaoendana na mawazo ya Waheshimiwa Wabunge ambao walipata nafasi ya kuchangia maeneo mbalimbali. Kwa upande wa sheria Waheshimiwa Wabunge wamechangia maeneo mbalimbali yanayohusu mtazamo wa kurekebisha sheria mbalimbali ili kuendana na wakati tulionao.

Mheshimiwa Spika, na katika hali ya kawaida wengi wa wachangiaji walikuwa wanaonesha kwamba, bado tuna sheria kandamizi ambazo kimsingi Tanzania haina sheria kandamizi. Na hili nalirudia tena na niliwahi kulitoa katika maelezo yangu wakati nikijibu swali, isipokuwa tunazo sheria mbalimbali ambazo zinatakiwa kupitiwa upya kulingana na wakati tunaokwendanao kwa sababu, hizi sheria hatuwezi tukazikosoa tukaziita sheria kandamizi kwasababu, chombo kinachotunga sheria ni Bunge lako tukufu na hivyo haliwezi kubebeshwa mzigo wa kutunga sheria kandamizi kwenye nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wako watu walihoji uhalali wa baadhi ya Watanzania wenzetu waliokamatwa na kuwekwa ndani wakati wa uchaguzi, na inaonekana kwamba haki haijafata mkondo wake, lakini hawa ni wahalifu na wahalifu wanashughulikiwa kwa mujibu wa sheria. Hatuna sababu yoyote kimsingi ya kumuacha mhalifu akitumia kofia ya siasa kutuharibia usalama wa nchi yetu. Kwahiyo hawa tutaendelea kushughulika nao kwasababu wanahitaji kufuata msingi wa sheria ya nchi yetu (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yako maeneo ambayo Waheshimiwa Wabunge waliona ni muhimu sana. Kwa mfano marekebisho ya sheria za mashirika ya Umma ambayo yanaonekana yamepitwa na wakati, kimsingi haya ni mapendekezo ambayo Serikali inayachukua kwa ajili ya kwenda kuyapitia na kuona kama kweli hizi sheria zimepitwa na wakati, kama tunavyoendelea sasa kufanya marekebisho mbalimbali ya sheria katika kuboresha mifumo ya sheria ambayo kimsingi ina mchango mkubwa katika kuleta maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo yale ambayo yameshauriwa tutayachukua na kuyafanyia kazi ili kuboresha. Na Waheshimiwa Wabunge tujue tu kwamba sheria iliyo bora inayokwenda na wakati ni nguzo imara sana katika kujenga uchumi wa nchi yoyote duniani. Kwahiyo kimsingi niseme kwamba tumepokea yale maeneo yote ambayo yameshauriwa na Waheshimiwa Wabunge, tutayafanyia kazi na chombo hiki hiki kitaletewa kwa ajili ya kupitisha sheria ya marekebisho ili tuweze kwenda na wakati na masuala mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, wako Wabunge wengine walizungumzia habari za rushwa. Waheshimiwa Wabunge sisi ndicho chombo ambacho kinaweza kikaondoa rushwa Tanzania. Bahati mbaya sana wakati mwingine sisi wenyewe tukawa hatujanyooka sana katika suala la kuzuia rushwa isiendelee kutendeka nchini.

Mheshimiwa Spika, sisi tukisimama imara sisi ni viongozi wa maeneo madogo madogo sana unaweza ukakuta Halmashauri moja ina Majimbo mawili mpaka matatu lakini sisi huko ndiyo hasa tunakuwa ni chanzo kikubwa sana cha kuji-involve kwenye mikataba ya ovyo ovyo huko kwenye maeneo ya Halmashauri zetu, na wala hatusimamii kuzuia rushwa isitendeke. Lakini linakuja Bungeni sasa linabebwa kama vile kuna mtu mwingine mbadala atakayekwenda kusimamia juu ya kuzuia rushwa zisiendelee.

Mheshimiwa Spika, mimi niwaombe Waheshimiwa Wabunge wenzangu, sisi tuko hapa kusimama kuisemea Serikali lakini sisi vile vile ni wawakilishi wa wananchi, tumetoka huko. Kama ingekuwa Waheshimiwa Mawaziri ni wakuteuliwa tu kutoka kwenye taasisi nyingine labda wangekuwa hawajui miondoko na mienendo iliyopo kwenye maeneo ya majimbo. Lakini ukweli ni kwamba, sisi tukiamua kuondoka kwenye rushwa tukasimama imara kama Waheshimiwa Wabunge, na pale linapotokea jambo la rushwa kwenye Halmashauri yako kwenye Jimbo lako tukakuona umesimama Mbunge unazungumza kwa nguvu zako zote mimi naamini baada ya muda suala la rushwa litakuwa ni hadithi tu.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo haya maboresho ya kusimamia haki ambazo zinasababisha vionjo vya rushwa. Ukweli lazima tushirikiane wote, kwasababu hata kama sheria ikiwepo, hapa iko sheria ya kuzuia rushwa lakini rushwa bado zipo, ni kwasababu miongoni mwetu hatuzisemi hadharani, na matokeo yake tunapokwenda kwenye utekelezaji lawama zinarudi Serikalini na kuonesha kwamba Serikali haisimamii vizuri.

Mheshimiwa Spika, sasa Mbunge wewe ni sehemu ya Serikali; na tusipoteze nafasi kwamba sasa baada ya wananchi kukuchagua wewe ni mtumishi wa Serikali moja kwa moja unadhibiti mambo mbalimbali yanayotokea kwenye halmashauri zetu kwenye maeneo yetu ya kata na ya vijiji. Mimi ningeomba tushirikiane sana kwenye eneo hili. Sheria tu kama sheria hata ingekuwepo ya aina gani bila sisi kuisimamia vizuri bado itakuwa ni kazi bure tu.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo mimi niwaombe Waheshimiwa Wabunge tushirikiane kwenye maeneo haya. Tumeweka taasisi kama TAKUKURU tuna vyombo kama Polisi, lakini bila kupewa ushirikiano watu hawa hawawezi kuliondoa hili tatizo. Sisi ndiyo wengi tunaweza tukafanya ambushi ya kuondoa matatizo yote kwenye maeneo yetu na kimsingi tukaondokana na hii kadhia ya masuala ya rushwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu demokrasia wengi wamesema. Lakini sielewi, nahisi labda kuna watu wanaamini kwamba Tanzania haina demokrasia;

Mheshimiwa Spika, lakini nikuhakikishie, demokrasia ya Tanzania huwezi kuikuta mahali popote, hata Uingereza wenyewe hawana demokrasia hii. Wanatawaliwa na Mfalme huwezi kupata demokrasia ya kweli, demokrasia inatoka kwenye vyombo ambavyo watu wake wanatumia demokrasia ya kuchagua…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana…

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SEHRIA… sisi tunachagua hapa na tunaendelea vizuri kabisa na maisha yetu na wale wanaodai demokrasia kimsingi ebu wajitafiti wao wenyewe kama wana demokrasia ahsante sana. (Makofi)