Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru lakini pia nimshukuru Mwenyezi Mungu aliyenipa afya njema hadi siku ya leo nikapata fursa ya kutoa mchango huu.

Mheshimiwa Spika, mimi nijielekeze moja kwa moja kwenye sekta ya kilimo. Unapozungumzia sekta ya kilimo kwenye taifa letu unazungumgumzia sekta muhimu sana, hasa ukizingatia zaidi ya Watanzania asilimia 65 wanashughulika na sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, unapozungumzia kilimo kuna mambo ya msingi hapa ya kuzingatia. Jambo la kwanza ni suala zima la utafiti, jambo la pili ni pembejeo na la tatu ni masoko; lakini wanavyokwenda kwenye masoko utagusa kidogo na masuala ya viwanda.

Mheshimiwa Spika, tunavyozungumzia tafiti mimi najiuliza maswali mengi sana hapa. Tumekuwa tuzijenga hoja za tafiti kwenye kilimo. Hatuna changamoto ya tafiti, tuna vyuo ambavyo vipo hapa kama vile Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) ni maelekezo tu. Wenzetu Japan kule wana mfumo mmoja ambao wanasema Public Private Academia. Maana yake nini, kuna umuhimu wa wasomi kufanya tafitil; tungetumia vyuo vikuu vyetu hivi kufanya tafiti, hamna haja ya fedha eneo hilo. Wape maelekezo SUA wafanye tafiti kwenye kilimo tuwekeze tupate kilimo chenye tija kwa taifa letu. (Makofi.

Mheshimiwa Spika, eneo lingine nimezungumzia suala la pembejeo. Bado kuna changamoto kubwa ya pembejeo lakini kubwa zaidi ni masoko.

Mheshimiwa Spika, nirudi kwenye zao hili la kimkakati la mpunga. Ukizungumzia Mkoa wa Morogoro hasa Jimbo la Mlimba, sisi katika taifa hili tunalisha zao la mpunga. Hata hivyo tuna changamoto ya kuuza mpunga nje ya nchi, lakini hatuwezi kuuza mpunga mpaka tuuchakate mpunga. Kwa hiyo naiomba Wizara ya Kilimo itusaidie. Jimbo la Mlimba tungeweza kufanikiwa sana kama tungewekeza viwanda vya kuchakata mpunga tupate mchele, mchele uwekwe kwenye fungashio actually uwe branded na upelekwe nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa najaribu kuona hapa wenzetu Japan wanaagiza chakula cha mwaka mzima, nilisema hapa awali, Zimbabwe wamekuwa wadau wakubwa wakiuza chakula nje ya nchi, na sisi tunaweza kufanya hilo; kwa hiyo tuongeze jitihada za utafiti kwenye kilimo, pembejeo lakini pia na viwanda pamoja na suala zima la masoko.

Mheshimiwa Spika, eneo lingine ambalo ninataka niliguse ni eneo la viwanda. Eneo hili nitagusa wizara mbili, Wizara ya Ulinzi lakini pia na Wizara ya Viwanda na Biashara. Naomba kama kuna Waheshimiwa Mawaziri na Manaibu Mawaziri mnisikilize kidogo.

Mheshimiwa Spika, katika safari ya maisha yangu mnamo mwaka 2002 niliwahi pita pale Nyumbu. Nyumbu pale kuna Shirika la Nyumbu la Taifa. Shirika la Nyumbu la Taifa, yaani Nyumbu Automobile Engineering, mimi nimekaa pale miezi minne; nchi hii ni Tajiri. Kama Shirika la Nyumbu likatumika vizuri hatuwezi kuagiza magari Japan. Pale Shirika la Nyumbu linavifaa vyote lina foundry zote, linafanya hata iron processing. Kuna Electrical Furnace ambayo kazi yake ni kuchakata chuma. Wana-pattern shop, wana-foundry shop, wana kila kitu. Mheshimiwa Baba wa Taifa alianzisha shirika hili ili tuweze kupata magari ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kama tunafikiri kuna eneo la kuwekeza ili tupate fedha ni Shirika la Nyumbu. Kwa hiyo Waziri wa Ulinzi na Waziri wa Viwanda mtusaidie kufufua Shirika la Nyumbu ili Watanzania tusinunue magari nje ya nchi tununue ndani ya nchi yetu. Labda niseme tu, kwenye uchumi mtanisaidia. Suala la mauzo nje ya nchi na kuagiza bidhaa nje ya nchi; Mheshimiwa Waziri wa Fedha kaka yangu Mheshimiwa Mwigulu Nchemba naomba unisikilize eneo hili. Kwenye uchumi kuna masuala tunazungumzia kuna jambo la export na import nchi yeyote yenye uchumi imara lazima izalishe na kuuza sana nje ya nchi. Ukiona mnaagiza sana kuliko kuuza nje ya nchi maana yake nini, ukikokotoa pale, kuagiza bidhaa nje ya nchi idadi ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi ikiwa kubwa kuliko idadi ya bidhaa tunazonunua unapata favorable balance of payment, favorable balance of payment, maana yake unapata jibu chanya na siyo hasi, eneo hili wachumi watanielewa kidogo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tukiendelea kuagiza sana kuliko kuuza bidhaa nje ya nchi bado tutaendelea na uchumi ambao unatusababishia kuwa unfavourable balance of payment na mwisho wa siku nchi yetu itapata tatizo la capital flight. Capital flight kwenye uchumi maana yake unavyoagiza bidhaa nje ya nchi unachukua pesa ya ndani ya nchi kwenda kubadilisha na pesa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: …ya nje ya nchi yaani dola maana yake nini ndani ya nchi hiyo utapata changamoto ya balance of payment.

Mheshimiwa Naibu Spika; naomba nimalizie kwa jambo moja, dada yangu hapa Mheshimiwa Halima Mdee amezungumza jambo ambalo Mungu anisaidie Roho Mtakatifu anishukie wakati namalizia tu. Kwanza nianze na lugha za kejeli, lugha za kuudhi.

Mheshimiwa Spika, sisi wengine ni vijana pia na bado hata umri wa busara haujafika, tuna hofu sana. Tunasihi, na mimi niseme tu kwa dhati, namuonya, aache lugha za kejeli ndani ya Bunge hili, aache lugha za kejeli ndani ya Bunge hili namuonya tu, hamna njuka hapa, njuka maana yake nini? kwa hiyo namuonya kwenye eneo hili.

Mheshimiwa Spika, lakini pia amezungumzia suala zima ya ATCL, unapotosha. Uchumi wowote duniani unapozungumzia usafirishaji inamaanisha kuwa ni huduma, it’s just a service, ni huduma tu, ku-facilitate maeneo mengine ya uchumi kama utalii, kilimo na maeneo mengine. Anakuja hapa anatudanganya, anadanganya Watanzania hapa tunampigia makofi hapa. Lugha za kuudhi nakuonya. (Makofi/Kicheko)