Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa fursa hii ya kuweza kunipatia kuchangia katika Mpango huu wa Tatu wa miaka Mitano. Nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa mpango mzuri uliojikita kutoka kwenye document takriban kumi na moja ambazo amezi-refer, ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025, ikiwemo Agenda 2063 ya Afrika, lakini na nyingine nyingi mpaka hizo document kumi.

Mheshimiwa Spika, binafsi mimi nitajikita katika maeneo mawili tu kwa sababu ya muda. Eneo la kwanza ni la elimu, ambalo liliguswa na mchangiaji wa kwanza au wa pili wa siku ya leo.

Mheshimiwa Spika, ukurasa naamba 25 wa mpango huu unaonyesha kwamba mwaka 2014 Tume ya Mipango ilifanya utafiti wa soko la ajira na ikaja na majibu kwamba ujuzi wa wale watu ambao wanapata elimu ndani ya nchi hii ulionekana ni pungufu kulingana na mahitaji ya waajiri. Maana yake waajiri kwenye viwanda, kilimo na sehemu zingine. Ukaja na mapendekezo kwamba tunatakiwa tuwekeze, kwenye mpango huo huo, wanasema tuwekeze mara tano ya uwekezaji uliokuwepo mwaka 2014 ili kuweza ku-fill hiyo gape ambayo inaonekana kwenye elimu tuliyonayo.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi nishauri; ukurasa namba 73 umekuja na majibu kwenye mpango huu huu. Kwamba tunatakiwa tuguse elimu ya msingi kwa kitu kinaitwa SATU (Sayansi Teknolojia na Ufundi); yaani wanategemea kwenye SATU tuguse hiyo primary; lakini tuguse kitu ya T and M kwenye elimu ya vyuo vikuu kwenye mpango huu. Lakini elimu tuliyonayo sasa ni competence-based education; ambapo competence-based education tunatakiwa tunapotengeneza mitaala yetu tuwe makini.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, ninategemea kabisa kama tulitakiwa kujaza huo udhaifu ulioonekana hapo tunatakiwa hawa waajiri na mazingira yetu ya kazi yahusike, tujue ni competence gani tunahitaji kwenye watu wetu. Kwa mfano, tunamuhitaji mtu ambaye atakwenda kulima maana yake competence ni kilimo; sasa ile principal outcome ya hiyo curriculum tunategemea ituletee mtu ambaye atakuwa na elimu ya kilimo, halafu twende kwenye hizo enabling kwamba tunakwenda kumu-enable nini ili aje ya hiyo principal outcomes.

Mheshimiwa Spika, sasa ninaona kabisa kuna mahali fulani Wizara ya Elimu huenda inachukua kumbukumbu za knowledge based na kutengeneza curriculum na hatimaye ndiyo sababu hatuwapati hao ambao tunawahitaji. Kwa sababu kama tunahitahi na tunaujua mwisho wetu tunashindwaje kutengeneza process ya katikati ili tuwapate hao wataalam? Kwa hiyo niishauri Wizara ya Elimu waangalie competence gani tunahitaji kwenye eneo hili, baadaye waende kwenye principal outcome waende sub-enabling na mwisho wa siku tutakuwa tunaweza kupata ability ambazo tunazihitaji kwa watu wetu. Tutapata hicho tunachohitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini niguse viwanda. Mimi niseme tu ni-declare interest, mimi ni mhandisi; tunatatizo kwenye viwanda vyetu. Ukisoma kwenye document ya Mheshimiwa Waziri ya mpango huu ukurasa namba 68 unaonesha tutakuwa na viwanda vya ku-process; lakini umeonyesha mambo mawili kwenye ukurasa wa 68. Unaonesha kwamba ni lazima tuwe na mali ambazo tunaziuza nje ambazo zipo- process. Lakini ya pili ulionesha kuwa lazima kuwe na political will, kuwe na utashi wa kisiasa wa kufunga mikataba ambayo ina faida kwa nchi, kwenye ukurasa wa 68; ni document hii ambayo ninaizungumzia hapa.

Mheshimiwa Spika, sasa shida ninayoiona tunapoenda ku-process kwenye viwanda vyetu; kwa mfano viwanda vya alizeti, hakuna kiwanda cha alizeti kinachota double refined oil nchi nzima, tunatoa semi refined kila mahali, na haya ndiyo mafuta ambayo kila Mtanzania amekula. Kuna mahali fulani hata ukimuona mtu anachangangia anachemka unajua hii ni semi refined ilimu- affect tangu utoto mpaka leo ndiyo sababu anahemuka. Kwa hiyo kuna mahali ambapo tunatakiwa sasa tutengeneze double refined ili watu wetu wale mafuta yaliyosafi (quality food) lakini tunachotengeneza ni semi refund na watu wote wanakula semi refined.

Mheshimiwa Spika, lakini niseme, tunatakiwa tuongeze ujuzi kama tulivyosema. Kuna njia mbili ya kutengeneza mafuta kwanza ni press; yaani ku-press you press by hydraulic au you press by expeller machines kuna machine kumal, kuna machine za VIP zinafanya hiyo pressing. Hiyo teknolojia ya zamani, teknolojia ya sasa ambayo itatutolea mafuta mengi ni solvent extraction ambayo nchi nzima hakuna mahali ambapo tunafanya solvent extraction tunafanya pressing tu. Na ili u-press mafuta kutoka kwenye mbegu zetu lazima utumie motor kubwa na gharama yake inakuwa kubwa. Kwenye solvent unatumia chemicals tutaenda kufanya double refine tutakuwa na mafuta yaliyo safi. Nchi nzima sasa ina mafuta yanatoka Uturuki wanatumia solvent extraction, kwa nini sisi tusiingie kwenye teknolojia hiyo ili tuweze kupata mafuta?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kuna habari ya gape ya ujuzi ambayo tunatakiwa kwenye viwanda na biashara sasa waangalie gape hiyo mahali gani kwenye uhandisi tunaiondoa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzunguzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga hoja. (Makofi)