Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuchangia Mpango huu ambao ni dira kubwa, mimi naita ni jahazi litakalotuvusha kama kuna upepo au hakuna upepo kama alivyosema Rais wetu mpendwa, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Wabunge wengi walipokuwa wanachangia walizungumzia habari za markets yaani masoko, kwamba uzalishaji ni mkubwa lakini tuna upungufu wa masoko katika kuuza bidhaa zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri ndugu yangu Mheshimiwa Mwigulu pamoja na Naibu kwamba duniani au Serikali ya Marekani imetoa fursa kwa nchi za kiafrika ambao Mpango huu unaoitwa AGOA (African Growth and Opportunity Act)nadhani katika utawala wa Bush ameamua Afrika iweze kuuza bidhaa zaidi bila ushuru wa aina yoyote. Sasa ni vema zaidi tukajikita na masoko ya nje, nchi yetu ina utajiri wa bidhaa mbalimbali tunazalisha, kuna maparachichi, kuna aina ya bidhaa mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nikifuatilia kwa karibu sana, kila Mbunge anayesimama anasema kwamba soko hatuna bidhaa zinaharibika, kwa hiyo naishauri Serikali kwamba soko la AGOA nalo likapiga hodi Marekani. Hili ni soko zuri na halina ushuru maadamu tu ile bidhaa iliyozalishwa iwe brand yake made in Tanzania na iko katika hali ya ubora. Tusiwe waoga, wakati umefika tutumie fursa za ulimwengu, tutumie madirisha ya ulimwengu kusudi na sisi tuweze kuuza bidhaa zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hayo machache, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja, ipite. Ahsante sana. (Makofi)