Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pia naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kupata nafasi ya kusimama mbele ya Bunge hili leo na kuweza kutoa mchango wangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano, ambayo ilifanya marekebisho ya Sheria ya Madini mwaka 2017 na tukaja na sheria mpya na kanuni zake ambazo kwa ujumla zimefanya mchango wa kampuni za madini hasa kampuni kubwa ya uchimbaji wa dhahabu pale kwangu Geita GGM kuonekana kwa macho kwa wananchi wa Geita.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia marekebisho hayo ya sheria sasa katika kipindi cha miaka mitatu tu ambayo Bunge hili lilifanya marekebisho, ukifika Geita mjini unaweza ukagundua kwamba marekebisho yale yalikuja katika kipindi sahihi na tayari kuna mabadiliko makubwa na maendeleo makubwa sana ambayo wananchi sasa yanawatoa kwenye mgogoro ambao ulikuwepo awali wa kuona hawa wachimbaji, makampuni makubwa ya madini wanakuja kuchukuwa madini yetu na kutuacha watu maskini, ukifika katika Jimbo langu la Geita Mjini utaona kitu tofauti kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili liliwezekana kwa sababu lilisimamiwa vizuri na naamini katika Mpango huu wa miaka mitano ijayo, yako mambo nataka kuishauri Serikali iendelee kuyafanyia kazi. Kwa mfano, tulipotunga sheria tulizungumza habari ya local content nimsikia Mheshimiwa Rais juzi akisema inafanyika vizuri. Naomba niseme ukweli eneo hili bado halijafanya kazi vizuri, sio kwenye consultation peke yake bado local content katika mazingira ya bidhaa zilizotajwa katika sheria, section 102(2) na (3) tumesema vizuri juu ya bidhaa ambazo hazipatikani Tanzania na tukasema vizuri juu ya namna ambavyo Mtanzania au kampuni ya kitanzania inatakiwa iwe na asilimia ngapi kushirikiana na kampuni ya kigeni ili kuweza kuingiza bidhaa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, bado eneo hili halijasimamiwa vizuri, bado makampuni makubwa yanayo uza bidhaa za gari katika migodi ni makampuni ambayo yamesajiliwa nje na makampuni ambayo yanaleta bidhaa moja kwa moja kutoka nje kuingiza Tanzania. Maana yake ni nini? Kama mgodi matumizi yake makubwa ni kwenye services, maana yake asilimia zaidi ya sitini ya mapato ya mgodi ni kwenye services. Kama mgodi huo una mapato yake ya dola labda milioni 300, sixty percent ya dola milioni 300 ni kwenye gharama za uendeshaji, kama nusu ya hizi zinafanya manunuzi nje, maana yake Serikali inapoteza pesa nyingi sana. Kwa hiyo, ushauri wangu eneo hili lisimamiwe vizuri, ufanyike ukaguzi, sheria ime-provide, imetoa maelekezo migodi hii kila baada ya miezi miwili, kutangaza ni bidhaa gani ambazo inazitaka kutoka nje ili kuruhusu Watanzania waweze kuziingiza. Hata hivyo, bado zimekuwa hazifanyi hivyo na kama zinafanya inafanyika kwa kificho kiasi wafanyabiashara wengi wenye uwezo wanashindwa kupata nafasi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili ya sheria hii tulizungumza habari ya CSSR, inajulikana wazi, kwenye own source tunasema service levy watalipa 0.3 percent, lakini kwenye CSSR sheria imebaki kimya imeacha jambo lile liko wazi; wengine wanasema 0.7, wengine wanasema ni discretion ya investor. Sasa inatufanya tushindwe kuitumia vizuri hii sheria kwa sababu ni vizuri pamoja kwamba pesa hii ni ya mwekezaji iprovide iseme ita-range kutoka asilimia ngapi kwenda asilimia ngapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa kuna shida moja kubwa ambayo naiona pamoja na kusifia tunafanya vizuri sana kwenye mahusiano na mgodi, lakini bado shida tuliyonayo kubwa na ambayo nafikiri Serikali inabidi inatakiwa ifanyie kazi ni kwamba pesa hizi za CSSR zinatumika unakuta gharama zake ni kubwa kuliko gharama halisi ambazo ziko kwenye maeneo ya masoko ambayo tunanunua bidhaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kutoa tu mfano, sisi tunapata CSSR ya bilioni 10, lakini gharama ya CSSR ile unaweza ukakuta mnabishana kuhusu ujenzi wa mradi ambao ungejengwa na halmashauri ungegharimu milioni hamsini, gharama ya ujenzi wa CSSR kwa sababu pesa ni ya kwao utajenga kwa milioni 150. Kwa hiyo nasema bado sheria hii haiweki wazi sana kwanza ni asilimia ngapi hii CSSR ambapo ni kichaka kinajificha, lakini pili ni matumizi ya CSSR, ni vizuri sheria ikasema wazi kwa kuwa ni pesa inakuwa declared kwenye kodi, basi pesa hii isimamiwe na Sheria za Manunuzi za Serikali ambazo tunazifahamu sisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumefanya vizuri sana kwenye utalii kwa miaka takribani minne kabla ya covid na naomba niseme kwamba kipimo kizuri cha mafanikio kwenye jambo hili kimekuja kwenye kuharibiwa na mwaka mmoja baada ya kuingia kwa covid. Tunafanya nini ili tuweze kufanya ya tukio la covid.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia comment juzi hapa, habari ya hasara ya ATCL. Kulipima shirika la ndege changa lenye miaka mitatu kufikiri litapata faida hiyo sio biashara ya nyanya. Shirika la ndege lina-indirect vitu vingi sana ambavyo huwezi kuvipima kama unapeleka nyanya pale Soko la Karikoo kwenda kuuza unatoa gharama na vitu vingine. Kuna vitu vingi sana lazima CAG hapa angesema pamoja na kula hasara hapa lakini limesaidia one, two, three, four, five. Tunataka kuimarisha utalii dunia nzima wanayofanikiwa kwenye utalii wanafanikiwa kwenye mashirika ya ndege. Kwa hiyo maoni yangu kwenye jambo hili, kwanza tuendelee na mpango wa kuliimarisha shirika hili, lakini tujitanue vizuri Zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeona tuna weakness moja, tunasubiri watalii wanaokuja wenyewe au wanaotafutwa na watu. Kiko kitengo kimoja ambacho nchi nyingi kinawapelelea watalii wengi sana hawa wanatumia sana mashirika ya ndege ya ndani cha mikutano lazima pale TTB, Wizara iweke kitengo maalum cha kufanya lobbying, mikutano mingi duniani inatafutwa haiji yenyewe. Wale ndugu zangu wa AICC pale wanasubiri mikutano ije, mikutano ile mikutano ile ya Afrika Mashariki haiwezi ikasababisha nchi hii iweze kuonekana inafanya mikutano. Ni lazima awepo mtu anafanya lobbying na mashirika makubwa duniani yanayoleta mikutano ya watu zaid ya elfu nne na anazunguka duniani kuitafuta hiyo mikutano.

Mheshimiwa Naibu Spika, amesema hapa Mheshimiwa Shangazi, kuna kinaitwa economic diplomacy, ukienda kwenye balozi zetu, nimeenda kwenye balozi karibu nane Tanzania, unakuta staffing ni watu wasiozidi kumi WTO mikutano peke yake iliyoko Ujerumani katika kipindi cha mwaka mmoja inayotangaza utalii iko zaidi ya hamsini, wale walioko pale watu sita, watatu wameweka brochures na vitu vingine kwenye meza na website yao ipo centralized Tanzania hawawezi kuleta watalii na kuongeza watalii Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tukubali kwamba tunatakiwa kama tunazungumzia hao wafanyakazi, tuwa- empower tupeleke watu wawe equipped na knowledge, wapewe pesa wazunguke kwenda kuwatafuta hao watu waje Tanzania vinginevyo tutaendelea kuzungumza habari hii na itaendelea kuwa shida kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo linguine, hapa katikati tulipata tatizo kidogo, tunao utalii wa uwindaji, watalii wa uwindaji ni matajiri sana duniani, lakini kuna gharama kubwa sana ya kuki-manage kitalu, tunayo sheria kila baada ya miaka mingapi unatakiwa kufanya mnada. Sasa unapofanya mnada, unakuta yule amekitunza kile kitalu kwa miaka mingi anaweza asishinde kulingana na mtu mwingine, anayekuja interest yake sio kutunza kile kitalu matokeo yake anapoteza wateja wale wa mwanzo, kitalu kinapoteza thamani na tayari tunandelea kupunguza idadi ya watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu hapa, wale wanaofanya vizuri waendelee kuaminiwa na Serikali, waendee kupewa na waendelee kulindwa. Nasema hivi kwa sababu shida kubwa tuliyonayo tunafikiri unataka uuze vitalu kwa mnada, sawa, utauza vitalu vinne, halafu vitalu sabini viko wazi maana yake nini, ningekuwa mimi ningeweza kuvigawa hata bure vyote, halafu ukataka utoze kodi kutoka kwenye vile vitalu kwa sababu kitendo cha kukaa wazi gharama kubwa ya Serikali ni kuvilinda na kuviendesha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumezungumza hapa mara nyingi kuhusu TRA, nashukuru sana Serikali Sikivu ya CCCM imesikia na imetoa maelekezo. Jambo moja hapa nataka nimshauri Mheshimiwa Waziri wa Fedha, mara zote wanapoona tunazungumzia Habari ya mgogoro wa walipa kodi na TRA inayoweza kula hasara hapa ni Serikali, negotiation itakayokuja ulikuwa unalipa milioni tano na hili ndio jambo ambalo nataka kumshauri lazima tuwe waangalifu tunataka kumpa nani unafuu. Ulikuwa unalipa milioni tano unataka kulipa milioni tatu, wanaweza watu wakatumia vibaya hii loop aliyoisema Mheshimiwa Rais, matokeo yake watu wakawa wana-negotiate wanakwambia nipe milioni mbili halafu hapa tutaandika hela kiasi Fulani, tunapoteza pesa ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nataka kushauri, badala ya kila mwaka huyu mtu anakwenda kukadiriwa kodi ya kulipa TRA kwa nini ukikadiriwa mwaka huu usiachwe miaka mitatu unalipa constant ile ile halafu baadaye utakapo-provide zile audited accounts zako waweze ku- review hesabu. Kitendo cha kila baada ya miezi tisa unaweza kutengeneza hesabu kinafanya mazingira ya kukaa mezani kila mara kuwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele imeshagonga.

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Kengele ya kwanza Mheshimiwa.

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili imeshagonga.

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)