Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa fursa hii ili niweze kuchangia Mpango wa Tatu wa Maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupanga ni taaluma, lakini kwa Taifa letu na kwa Serikali yetu kupanga si tatizo. Mpango huu tulionao ni mzuri sana kuliko mipango mingi sana ya nchi nyingi hapa Afrika, lakini shida tulionao sisi kwenye kupanga ni kutekeleza Mpango tuliouweka.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi sitaongelea mengi isipokuwa nataka nijielekeze eneo moja tu, la Mradi Mkubwa tulionao wa Standard Gauge Railway, tunayoijenga. Standard Gauge Railway tunayoijenga ukijumlisha tu zile njia kilometa zinazojengwa tunatakiwa tujenge kilometa 4,886, hapo naongelea njia tu, siongelei mahala ambapo reli zinapishana. Mpaka sasa tumeshajenga kipande cha Dar es Salaam kuja Morogoro kilometa 300 na tunaendelea na kipande cha Morogoro – Makutupora kilometa 422, lakini vilevile tuko upande ule mwingine wa Isaka na Mwanza kilometa 249.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa aina ya financing ya mradi huu tunavyoindesha tukiendelea nayo tutaujenga Mradi huu wa Standard Gauge kwa nchi nzima kwa miaka 81, miaka 81. Ikiwa miaka mitano tumejenga kilometa 300 ndio ambazo ziko above 90 then kilometa 4,886 tutazijenga kwa miaka 81. Hii katika nchi ambayo inapambana kutafuta maendeleo ni kitu hakikubaliki, ni kitu hakikubaliki. Hivyo vipande nilivyo vitaja ambavyo vinajengwa vimetugharimu takriban trilioni 11. Trilioni 11 ni Idle Investment kwa sababu gani, kwa sababu hatutakamilisha leo ili tuanze kutumia mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachokishauri Serikali yetu iondekane na habari ya Traditional Methods za ku-finance miradi hii mikubwa. Kwanza tunajipa pressure kama Serikali, ya ku-finance mradi huu halafu tunashindwa kupeleka huduma kwa wananchi ambazo ni za kila siku. Kwa hiyo ninachokishauri Wizara ya Fedha waangalie utaratibu wa ku- finance mradi huu Infrastructure Bond. Wamefanya hivyo nchi za wenzetu, ukienda Benin wamefanya, ukienda Tunisia wamefanya. Hii inatupa ahueni ya kutekeleza mradi huu na kuutekeleza kwa wakati. Tunapoendelea kutekeleza mradi huu hivi kidogo kidogo ni hasara kwa Taifa letu, ni vile tu hatui- merge hii hasara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa faida ya wasiofahamu na Watanzania kwa ujumla, tunatakiwa tuitoe reli itoke Dar es Salaam iende mpaka Tabora kwa kupitia Singida, ikifika Tabora iende Isaka Shinyanga mpaka Mwanza, ikitoka Tabora iende Keeza ili tukahudumie Kigali na Burundi, ikitoka hapo Tabora tuipeleke Kaliua kwa ndugu yangu hapa, iende Uvinza mpaka Kigoma tukaihudumie Kongo na tukitoka Kaliua tuje Mpanda mpaka Katema; hiyo ni Reli ya Kati tunayojenga. Bado kuna kipande cha Tanga, Musoma, Arusha kilometa takriban 1,233; na hapo hapo bado kuna kipande cha Mtwara – Mbambabei kilometa 10,092.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ni kitu serious sana, hatuwezi tu kuendesha mradi huu kwa kutumia mapato ya ndani tutawaumiza Watanzania na tunajichelewesha wenyewe kupeleka maendeleo ambayo yanahusu huduma za moja kwa moja za wananchi za kila siku kama vile elimu na afya; na ndio maana kwa mwenendo huu wananchi wa Handeni mpaka sasa hatuja pata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa mradi huu kwa pamoja kutatusaidia sana kama Taifa kwanza kuifungua Bandari yetu ili iongeze mzigo unaopita pale. Kwa sasa hivi tunapitisha tani milioni 17 ukilinganisha na wenzetu wakenya wanapitisha pale Mombasa tani milioni 37. Kukamilika kwa pamoja na kwa wakati mmoja kutatusaidia sana kupata mapato kupitia mradi huu, kwa maana TRA wataweza kukusanya lakini vilevile wananchi wetu uchumi wao unataweza kuwa activated.

Mheshimiwa Naibu Spika, jinsi tunavyojenga kwa vipande vipande hivi na kuchukua muda mrefu kuna maeneo ya nchi yetu yatabaki kuwa-disadvantaged. Kwa mfano kipande hiki cha Mbambabei – Mtwara kitabaki kuwa ni historia tu ikiwa hatutatekeleza mradi wa Liganga na Mchuchuma, viability ya hii reli hapa haipo. Vivyo hivyo kipande kile cha kutoka Tanga kwenda Arusha kwenda Musoma kama hatukuimarisha vile vipaumbele tulivyoweka ukanda ule ikiwemo soda ash pale Lake Natron hakuna viability ya mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lipo bomba linalotoka Uganda Hoima kuja Chongoleani Tanga. Kwa vyovyote vile mafuta yatakapofika Tanga yatahitaji reli hii hii kuyarudisha yakisha kuwa refind. Kwa hiyo Serikali ione umuhimu wa kwenda kukopa kwa kutumia Infrastructure Bond ili tutekeleze mradi huu kwa pamoja kwa mara moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuyasema hayo na baada ya kushauri hilo ni malizie kwa kusema; limezungumzwa hapa asubuhi kidogo lakini halikukaziwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo Sheria ya Bajeti ya mwaka 2015 ambayo inatu-guide kuanzia mwanzo tunapotengeneza bajeti mpaka tunapoitisha bajeti hapa Bungeni, lakini sheria tukishapitisha bajeti hapa wenzetu wa Serikali wanapokwenda kutekeleza bejeti hakuna Sheria ya Monitoring na Evaluation. Kwa maana hiyo tunamuomba hapa Waziri wa Sera Serikali yetu hapa walete Sera. Kwanza wao watunge Sera ya Monitoring na Evaluation ili wailete hapa tuitungie sheria. Ndiyo maana ripoti hii ya CAG ambayo tunakwenda kuijadili ni aibu ni aibu ni aibu ni aibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tusipofika mahala tukatunga sheria hiyo; huwezi; kwa mfano mradi wa bilioni 380 unaotekelezwa, wa maji kule Handeni, unaojengwa kutoa Maji Korogwe kuyaleta Handeni eti ukasimamiwe na Mtendaji wa Kata, usimamiwe na Diwani. Lazima tutunge sheria ikae vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono mpango uliopo mezani, naomba kuwasilisha. Ahsante sana. (Makofi).