Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kuchangia kuhusu mtaala wa elimu ya msingi katika ukurasa VIII. Serikali imekiri kuwepo na mtaala uliokuwa ukitumika mwaka 1997. Je, Serikali inaweza kuleta nakala ya mtaala huo hapa Bungeni, kwani nimeutafuta bila mafanikio wakati ni mali ya umma?
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, malengo ya maendeleo ya milenia ya mwaka 2002, yaliyotajwa katika ukurasa wa pili yalizingatiwa vipi katika kutayarisha mtaala wa elimu ya msingi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, inakuwaje Mashirika ya Dini yanahusishwa katika tathmini ya mtaala wa elimu ya msingi, lakini sio katika kutathimini mtaala wa elimu ya awali na Serikali za Mitaa kuhusishwa katika tathmini ya mtaala wa elimu ya awali lakini sio katika mtaala wa elimu ya msingi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, malengo ya elimu ya Tanzania katika mtaala wa elimu ya msingi, ukurasa nne ni tofauti na yale yaliyoainishwa katika mtaala wa elimu ya awali katika ykurasa wa tatu na nne, kulikoni?