Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

Hon. Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2021/2022 – 2025/2026

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwanza kwasababu ni mara yangu ya kwanza tangu tumepata janga kubwa la Taifa kuzungumza hapa nitoe pole kwa Watanzania wote kwa msiba mkubwa tulioupata wa kuondokewa na Mheshimiwa Rais, lakini pia nitoe pole kwa Mheshimiwa Rais mteule Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuondokewa na Mheshimiwa Rais ambaye yeye alikuwa msaidizi wake wa kwanza na wa karibu sana.

Mheshimiwa Spika, lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Rais mteule Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mwanamke wa kwanza Afrika Mashariki kwa kuwa Rais.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Philip Mpango kwa kuteuliwa kwa mujibu wa Katiba kuwa Makamu wa Rais wa Tanzania, lakini pia niwapongeze Waheshimiwa Wabunge kwa kuendelea kuwa pamoja na nchi yetu kutokana na kipindi ambacho tumepitia cha mpito na mambo magumu ambayo tumepitia.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie na nitachangia kwenye Sekta za uzalishaji na nitajikita katika sekta ya kilimo, kwasababu Kilimo ni uti wa mgongo wa Taifa letu na tunajua tumekuwa tukitumia kauli hiyo tangu tunasoma; lakini pia practicability yaani utekelezaji wa maendeleo ya Taifa tunategemea sana kilimo kwa sababu kama tunazungumza Tanzania ya Viwanda na kama mwelekeo wa Serikali maana yake hatuwezi kuzungumza viwanda bila kilimo.

Mheshimiwa Spika, na kwa Waheshimiwa Wabunge wote ambao wamekuwa wana champion hoja ya kilimo, kwabababu utakumbuka hata mzungumzaji aliyepita amezungumza pia kilimo, na ninajua Waheshimiwa Wabunge wengi sisi kama nchi wengi tunajua tunalima kwa namna tofauti tofauti, lakini pia tunajua umuhimu; wake, kama ambavyo Mwenyekiti wa Kamati ametoka kuzungumza. Kwamba tunahitaji malighafi kwa ajili ya viwanda vyetu kwasababu tunategemea malighafi za ndani sasa hauwezi kuzungumza malighafi za ndani bila kuzungumza kilimo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa pekee sana kwa mujibu wa ripoti ya CAG na mambo ambayo amechambua kwenye ripoti yake, ukiangalia mpango wa kwanza na wa pili kwasababu tunazungumza Mpango wa Tatu lakini wakati tuko sasa hivi lazima tukumbuke tulikotoka kwa hiyo, kwenye suala zima la kilimo kuna mambo kadhaa ambayo CAG katika ukaguzi wake ameyaona.

Mheshimiwa Spika, mathalani nitayazungumzia hayo huwezi kuzungumza kilimo bila kuzungumza mbegu, sasa kama Taifa tulikubaliana kwamba tutakuwa na mashamba tisa ya kuzalisha mbegu lakini ukweli ni kwamba kwa mujibu wa ripoti ya CAG mpaka sasa ni shamba moja tu ambalo linafanyakazi mwaka mzima lakini mashamba mengine nane yanategemea msimu wa mvua kwa hiyo yako kwa mujibu wa msimu. Sasa hatuwezi tukazungumza kwamba tunataka tufanye kilimo kiwe sekta ambayo ni stable wakati hatuzungumzi tunapataje mbegu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunahitaji mashamba yote tisa ambayo yametengwa kwaajili ya kuzalisha mbegu nchini yafanye kazi yote mwaka mzima bila kusubiri msimu wa mvua kwasababu ripoti ya CAG inasema tunategemea shamba moja ambalo linafanyakazi mwaka mzima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kwenye nchi ambayo asilimia kubwa tuna water bodies tuna maji kwa asilimia kubwa sana kwenye nchi yetu ardhi ya Tanzania hatuwezi tukawa tunategemea mvua watu wanatushangaa kwasababu kuna vitu tu haviko sawa kwenye scheme za umwagiliaji kwasababu ili uweze kufanya uzalishaji kwa kutumia umwagiliaji lazima utengeneze scheme za umwagiliaji zifanye kazi ili uweze kufanya kilimo especially cha kuzalisha mbegu kwasababu mashamba tisa kama nchi ni mashamba machache sana ambayo tunaweza tukatengeneza utaratibu mzuri na tukayahudumia mwaka mzima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia kama nchi ripoti ya CAG inatuambia ni 39% tu ya pembejeo za kilimo zimegawiwa yaani ugavi kwenye pembejeo za kilimo ni 39% tu. Sasa unategemea Taifa lizalishe malighafi kwaajili ya viwanda vyake kwa Tanzania ya viwanda halafu unafanya ugavi wa pembejeo za kilimo kwa 39% tu. Kuna jambo Wizara na Waheshimiwa Wabunge kuna jambo lazima tukubaliane kwamba kama tumeamua kwamba tunatengeneza Tanzania ya viwanda ni lazima tukubaliane suala zima la kilimo ndiyo msingi na ni lazima wote ikiwezekana tuzungumze kuhusu kilimo. Kwasababu ndiyo tutapata malighafi kwaajili ya viwanda vyetu lakini ndiyo sehemu ambayo itatusaidia sisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwasababu sasa hivi mwenyekiti wa kamati amezungumza kwamba sasa hivi tunalima kilimo cha kujikimu yaani watu wanalima sana ni kwaajili ya kuendeleza maisha kwamba wapate chakula waishi lakini kwa ardhi ukubwa wa ardhi ambao tunao kwenye Taifa letu lakini water bodies ambazo tunazo kwenye Taifa letu, resourcefully ya wasomi na watu ambao wana profession za mambo ya agriculture Taifa letu limebarikiwa sana tunatakiwa tutoke huku tuende sehemu nyingine zaidi kwenye kuboresha kilimo chetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa ripoti ya CAG inatuambia ni 1% tu ya wakulima wamepatiwa mafunzo na mbinu bora za kilimo sasa asilimia moja tu wamepatiwa mafunzo ya mbinu bora za kilimo. Kuna jambo hapa haliko sawa, na hii ni kwa mujibu wa ripoti ya CAG na wapo maana yake watu wanaelewa nini tunachokizungumza. Bahati nzuri nina imani kubwa sana na Mheshimiwa Naibu Waziri pale kwasababu mara nyingi ndiyo tumekuwa tunamuuliza hata yeye maswali na yeye anajibu na anafuatilia Mheshimiwa Hussein Bashe. Kwa hiyo, kwasababu lengo letu ni kujenga na hii nchi ni ya kwetu maana yake hakuna mtu atatoka huku aje kutuambia tunajengaje nchi yetu hapa ni sehemu ambayo ni lazima tuweke nguvu Mheshimiwa Waziri yupo na Mheshimiwa Naibu Waziri pia yupo na Mheshimiwa Naibu Waziri pia yupo tuangalie tunafanyaje kwenye suala zima la kilimo na kimsingi mimi ni wa Singida kwetu tunalima alizeti, na tunalima kweli kweli alizeti kwa hiyo, ni declare interest kwamba mimi pia ni mkulima Pamoja na kwamba tunalima kwa simu. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, lakini pia kwenye upande wa pili nitoe mapendekezo labda nini kifanyike kwaajili ya kuhakikisha kwamba pengine utekelezaji wetu wa mipango ukiangalia mpango wa kwanza na mpango wa pili ni lazima tukubali kwamba kuna sehemu inawezekana haiko sawa ndiyo maana unakuta tunapanga bajeti za sekta za uzalishaji halafu hazitekelezwi kama tunavyopanga kama Bunge linavyopanga.

Mheshimiwa Spika, labda nitoe mapendekezo yafuatayo, pendekezo langu la kwanza napendekeza kuwe kuna sheria maalum kwasababu ni miaka 10 imepita mpango wa kwanza na Mpango wa Pili tunajadili Mpango wa Tatu phase ya mwisho ya miaka mitano ili itimie 15 tunaianza. Kwa hiyo, na nikiangalia hata nikisoma documentation na nini na Waheshimiwa Wabunge ambao ni wazoefu nyinyi mtalizungumza hili vizuri hatuna sheria mpaka sasa hivi ya kusimamia utekelezaji wa mipango ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kama tunakaa tunajadili na tumekuwa tunajadili kuhusu mpango sisi wengine tumekuja juzi siyo wenyeji sana lakini kama tunapanga vitu ambavyo hatuvitungii sheria ya utekelezaji maana yake baadaye tunashindwa kujibana yaani tunashindwa kwamba tutabanana wapi kwasababu kama kutafanyika bajeti reallocation hakuna sheria ya kutu-guide kwamba sasa tumepanga mpango huu tunatumia sheria gani kusimamia utekelezaji wa mipango hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nishauri uletwe muswada wa sheria Bungeni tutunge sheria ya kusimamia utekelezaji wa mipango tunayoipanga kama Wabunge, kwasababu sisi ni watu wazima tuna akili zetu na kuna watu ni wasomi sana hapa na kuna watu wana mawazo mazuri sana lakini hatuna sheria ya kutu-guide kwamba sasa tunatekelezaje mipango tuliyojiwekea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili naweza kushauri ni kwamba sisi kama Wabunge sasa hivi tuko kwenye Bunge la Bajeti tunapanga bajeti na kuna bajeti ambazo tunajua kabisa kwamba Bunge hili ndiyo linatoa muelekeo wa Taifa kwenye masuala la bajeti. Lakini kama tunapanga bajeti za miradi ya maendeleo halafu hazitekelezwi katika kiwango ambacho Bunge limepanga maana yake ni kama vile kuna kukosekana nguvu kwa upande mmoja. Kwa hiyo, nishauri tunapokaa kama bunge tukapanga bajeti zinazokwenda kwenye miradi ya maendeleo tunaomba bajeti zitekelezwe kadri ambavyo Bunge hili limepanga kwasababu hiki ni chombo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hiki ni chombo ambacho kinakaa na tunatumia fedha na tunatumia muda kupanga kwa hiyo hatuwezekani tukiwa tunapanga halafu bajeti hazitekelezwi kama ilivyo na kimsingi sheria ndiyo itatusaidia kwasababu hata bajeti reallocation haitakuwa sana kwasababu kama sheria itatulazimisha kwamba kusifanyike bajeti reallocation especially kwenye miradi mikubwa ya maendeleo ambayo tutajiwekea kufanya kama Taifa.

Mheshimiwa Spika, lakini pia jambo la mwisho naweza kushauri kuwe na uwajibikaji na kimsingi watu wanajitahidi katika kufanya wajibu wao lakini kwenye masuala la fedha kuwe kuna uwajibikaji endapo tunapanga tunapangiana program za kufanya na project za kufanya basi watu kuwe kuna uwajibikaji mkubwa kwenye masuala ya fedha ili kuwe kuna accountability kuwe kuna patriotism ule uzalendo mtu anauona kwamba sasa mimi hili ni jukumu langu kufanya jambo hili.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwasasa nimechangia hapo. (Makofi)