Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Hon. Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nihitimishe hoja ya kutambua na kuenzi mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuanza kusema, hakika kwake mola tumetoka na kwake ni marejeo, Bwana ametoa Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Watanzania tumepata pigo tumelia na uchungu kutokana na mapenzi makubwa tuliyokuwa nayo kwa jemedari wetu aliyetangulia mbele ya haki, iliyobaki ni kumuombea dua ili Mwenyezi Mungu ampumzishe salama huko aliko.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa vile lisilobudi kutendwa naomba Waheshimiwa Wabunge na Watanzania tuendelee na maisha yetu ambayo Mwenyezi Mungu ameturuzuku sisi ambao tuko hapa duniani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutambua na kuenzi mchango wa Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuongea tu, haitosaidia kitu chochote. Kutambua na kuenzi mchango wa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuongea tu haitasaidia chochote. Hivyo basi, niungane na wote waliounga mkono azimio hili kwa lengo la kuendeleza na kudumisha yale yote ambayo tumeyatambua na kukusudia kuyaenzi. Endapo tutafuata njia aliyotuonesha Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli nina imani tutakuwa tumeuenzi mchango wake kwa vitendo.

Mheshimiwa Naibu Spika, namalizia kwa kusema kwamba nina imani kubwa sana na Mheshimiwa Rais wetu, Samia Suluhu Hassan na Makamu wake Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango, kuwa azimio hili litaweza kutekelezeka chini ya uongozi wao mahiri.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nashukuru. Mwenyezi Mungu awajalie afya njema na uwezo wa kumudu majukumu yao katika Taifa letu. Ahsante sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Najma, toa hoja ili niweze kuwahoji Wabunge.

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja.

MHE. ANTHONY P. MAVUNDE: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.