Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Hon. Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kutambua na Kuenzi Mchango wa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa Utumishi wake Uliotukuka Pamoja na Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MHE. ANTHONY P. MAVUNDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa zawadi ya maisha ya Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambaye kupitia uongozi wake ametuachia mbegu ya ujasiri, mbegu ya kuipenda nchi yetu, mbegu ya uzalendo, mbegu ya kujiamini na mbegu ya kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika uongozi wa Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, nchi yetu imeshuhudia maendeleo makubwa na miradi mingi mikubwa ikitekelezwa ambayo tunaamini kabisa kwamba itakwenda kuleta tija kwa Mtanzania na kulifanya Taifa letu liendee kusonga mbele. Mheshimiwa Hayati Rais Dkt. Magufuli alifanya kazi yake kwa kumtanguliza Mungu na ametuachia hilo kama funzo sisi viongozi katika kazi zote ambazo tunazifanya, tumweke Mungu mbele ili tuweze kufikia malengo na mafanikio. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunamkumbuka sana Hayati Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli kwa kazi kubwa ambayo ameifanya katika nchi yetu ya Tanzania na kwa sisi hapa Dodoma kama ambavyo ilikuwa ada ya Azimio la mwaka 1973 la Makao Makuu, Hayati Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli alitekeleza kwa vitendo. Katika viongozi wote waliopita kila mmoja alifanya kwa sehemu yake, lakini tumeshuhudia chini ya uongozi wake, Makao Makuu ya Serikali yakiwa hapa Dodoma na Dodoma imebadilika hivi sasa, maendeleo yanakuja kwa kasi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashuhudia miundombinu mingi sana ikikamilika ndani ya Dodoma na kuifanya Dodoma kuendelea kuwa kati ya sehemu ambazo zinakua kwa kasi sana hapa nchini. Hii ni kazi kubwa na alama ambayo Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli ametuachia na tutaendelea kumkumbuka katika hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa kazi ambayo ameifanya katika nchi yetu ya Tanzania na hasa katika kuwaamini vijana, ametujengea heshima kubwa sana vijana wengi wa Kitanzania kuamini kwamba wana uwezo wa kufanya kazi na kazi ambayo inaweza kuonekana na watu ambayo inaweza kuonekana na watu kuithamini. Ni kiongozi ambaye aliamini katika vijana akawapa nafasi na kwa asilimia kubwa vijana hao wamelitendea vyema Taifa hili, hivyo tunamshukuru sana kwa heshima hiyo kubwa. (Makofi)

Mheshimwia Naibu Spika, pia kazi hii kubwa yote iliyofanywa na Hayati Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, tumempata mama yetu ambaye anakwenda kuiendeleza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye tunaamini kabisa atakwenda kuyasimamia yale ambayo Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli aliyaanzisha na kuyaendeleza kwa kasi kubwa zaidi. Imani yetu ni kwamba nchi yetu iko katika mikono salama. Wale wote waliokuwa wanadhani kwamba sasa mpira umerudi kwa goal keeper, hivi sasa kazi inaendelea pale pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona kazi ambayo ameianza siku chache zilizopita, Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan inaonyesha ni namna gani Tanzania ile ile ambayo kila mmoja alikuwa anaiota inaendelea. Nitoe rai kwa Watanzania nasi Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumuunga mkono Mheshimiwa Rais katika kazi hii ngumu kabisa na tunaamini kabisa Mwenyezi Mungu atamsimamia ili tuipeleke Tanzania kule ambako kila mmoja anataka Tanzania yetu iende. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kila mmoja anaamini katika uadilifu na uchapaji kazi wa mama yetu Mheshimiwa Suluhu Hasssan. Ni Imani yetu kwamba nchi yetu ya Tanzania kupitia uongozi wake itaendelea kung’ara na basi yale yote ambayo yalifanywa akiwa na Hayati Mheshimiwa Dkt. Magufuli, huu ndiyo mwendelezo wake mzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, imani kubwa sana ambayo tunayo kwa akina mama naye akiwa Makamu wa Rais ambaye alipita kwenye kipindi kilichopita, tunaamini ataifanya kazi hii vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Naunga mkono maazimio yote mawili. Ahsante sana.