Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, natanguliza pongezi kwa kuteuliwa kwake Mheshimiwa Waziri na hongera kwa uwasilishaji mzuri, naomba nizungumzie mambo machache yafuatayo:-
Kwanza, Serikali ilitoa waraka wa responsibility allowance, lakini mpaka sasa haijaanza kutekelezwa ili kuwawezesha viongozi wetu kwenye Idara ya Elimu.
Pili, kumekuwa na tatizo kubwa sana la madeni ya walimu, Serikali lazima ije na Mpango wa kukomesha madeni ya walimu.
Naomba soko huria la vitabu lidhibitiwe kuendana na mitaala ya elimu. Nashauri kuwe na formality moja nchi nzima ya vitabu.