Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, awali ya yote nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa sababu ni siku yangu ya kwanza kuchangia katika Bunge lako tukufu, lakini vilevile niwashukuru sana wananchi wa Jimbo la Karatu kwa kunichagua kwa kura nyingi na hatimaye nikawa jimbo la Karatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nikishukuru chama changu Chama cha Mapinduzi kwa kuniamini na mimi kupeperusha bendera na hatimaye nikawa Mbunge wa jimbo la Karatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme mchango wangu utajikita katika maeneo ya kilimo kama walivyoongea Wabunge walio wengi katika ukumbi huu, lakini vilevile katika jimbo la Karatu sisi ni wakulima, tunalima mazao ya kitunguu, mahindi na mbaazi, lakini ushauri wangu ni nini kwa Serikali na Wabunge walio wengi hapa wameongea kwamba katika eneo hili la kilimo Wabunge wengi wamechangia kwamba suala hili la kilimo kuwekwa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo langu la Karatu imetokea mara nyingi sana katika Wizara ya Kilimo kwamba sasa kipindi chakula kikiwa kidogo ndani ya nchi wanasema mazao yetu tusipeleke nchi za nje, lakini wakati huo mkulima huyo amelima kwa shida, wakati huo mkulima huyo wa Jimbo la Karatu na wa nchi ya Tanzania amelima kwa mikopo ya benki na kila kitu, lakini wakati huo Wizara ya Kilimo inasema tusipeleke mazao yetu nje ya nchi kwa sababu ndani ya nchi hii kuna uhaba wa chakula. Sasa ninataka kujua, hivi ni kazi ya wakulima wa Tanzania kulisha watu waliokuwa mjini ambao wanakaa kwenye baridi na wakati huo sisi tufanye kazi ya kulisha walioko mjini kwamba sasa tusiuze mazao yetu nje kana kwamba ndani ya nchi hii ya Tanzania kuna shida ya chakula. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi kwa nini mazao yetu tusiuze yakaisha kabisa baadae tukaagiza chakula kutoka nje kikaja ndani ya Tanzania kama tunavyoagiza mafuta yanaisha ndani ya nchi hii na baadae tunaagiza nje ya nchi ili kwamba watu wetu waweze kupata pesa katika eneo hili la kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kilimo katika Jimbo langu la Karatu tunalima kilimo cha aina mbili; kuna kilimo cha mvua na kuna cha umwagiliaji na sisi pale tuna tarafa nne katika Jimbo la Karatu lakini Tarafa ya Eyasi inalima kilimo cha umwagiliaji lakini tarafa nyingine zinalima kilimo hiki cha mvua na kule kwenye Jimbo langu la Karatu ukiwa unalima kilimo kile cha mvua unaweza kupata gunia tano kwa hekari mpaka gunia kumi, lakini unapolima kilimo kile cha umwagiliaji unaweza kupata gunia 30 mpaka gunia 40. Sasa ushauri wangu ni nini kwa Wizara hii ya Kilimo? Kwamba Wizara ya Kilimo ijikite katika mito na kutengeneza scheme namna ya umwagiliaji ili wananchi na wakulima walio wengi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waweze kupata mtiririko wa umwagiliaji ili waweze kutoka kwenye gunia tano mpaka kumi waende kwenye gunia 30 mpaka gunia 40 na huu ushahidi ninao katika Jimbo langu la Karatu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaishauri Serikali katika Wizara hii ya Kilimo; waache kufungua mipaka ya nchi hii kwa muda, waweze kuacha mipaka kwa miezi yote 12 ili wakulima hawa waweze kwenda kutafuta soko kwenye maeneo mengine nje ya nchi hii ili waweze kufaidi kilimo wanacholima kwa shida, kwa jasho, wasiendelee kuambiwa kwamba sasa hawawezi kuuza mazao haya ndani ya nchi hii ya Tanzania wakati huo Serikali haijandaa mpango mzuri wa kununua mazao ya wakulima, na wakati huo kama naweza kupata soko kule Kenya na nikaweza kuuza gunia kwa shilingi 200,000 kwa nini Serikali ndani ya nchi hii ya Tanzania wasiweze kununua gunia kwa hiyo shilingi 200,000 ambayo mimi mkulima naweza kupeleka mazao yangu katika nchi jirani ya Kenya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imeshaonekana mara nyingi magari ya watu yakitaifishwa katika mipaka ya Namanga, Kilimanjaro na maeneo mengi sana ya nchi hii kwamba sasa wakati huo mpaka ukifungwa unaweza kukosa gari yako au unaweza ukakosa mazao yako, wakati huo Serikali ikidai ndani ya nchi hii kuna upungufu wa chakula. Mimi naamini siyo kazi ya mkulima wa Tanzania kulisha wananchi wa Tanzania, ni kazi ya Serikali kulisha Watanzania na kujua kwamba chakula kinatosheleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende katika Wizara ya Maji; katika Jimbo langu la Karatu kuna Mradi wa World Bank ambao una takribani miaka kumi sasa haujaweza kukamilika. Lakini vilevile najua kuna Naibu Waziri wa Maji mwezi wa 12 aliweza kutembelea Jimbo la Karatu wakati huo Jimbo hilo la Karatu kuna mradi wa maji yeye alivyokuja mradi uliweza kutoa maji, lakini baada yayeye kuondoka mradi ule haujaweza kutoa tena maji. Lakini vilevile mradi wa aina hii uko kwenye Kijiji cha Getamo, uko Umbang, uko Endanyewe, uko Buger na Khusumai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika eneo la TRA Wabunge wengi waliongea; katika Jimbo langu la Karatu TRA wameweza kushindwana na wafanyabiashara walio wengi kwa sababu Jimbo la Karatu asilimia kubwa liko kwenye suala la kiutalii. Lakini vilevile hawa watu wa TRA kwa Jimbo la Karatu wamekwenda mbali zaidi, wamekwenda kuwahoji wakulima wa Tarafa ya Eyasi na mimi nikiwepo, kwamba utengeneze mehesabu ya miaka mitatu iliyopita ili uweze kutengeneza hesabu na kuwapelekea watu wa TRA. Sasa kwa Jimbo langu la Karatu inaonekana kwamba hawa watu wa TRA wamekwenda sasa mbali zaidi kwenda kuwahoji wakulima wanaolima kitunguu katika Tarafa ya Eyasi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.(Makofi)