Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa nafasi hii lakini nimshukuru sana Waziri kwa kuleta Mpango huu. Nimeupitia Mpango huu ni mzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nishukuru kwa miradi mikubwa ambayo tumeiwekeza kwa miaka mitano. Huo ndiyo mwelekeo sahihi wa nchi, lazima tuwe na capital investment. Kama tunataka hili Taifa baadaye liwe lenye heshima lazima tuanze kuwekeza sasa hivi kwenye miradi ya muda mrefu; miradi ya umeme, barabara, reli na ununuzi wa ndege. Bila kufanya hivyo litakuwa taifa lenye aibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite kwenye tatizo la ajira kwa vijana wetu wanaomaliza vyuo vikuu. Watu wengi wameongelea kero mbalimbali upande wa elimu kwamba elimu yetu ni mbovu na kadhalika. Mimi naomba niwatoe mashaka kwamba ingekuwa mbovu mimi leo nisingekuwa Daktari hapa wa Policy, ingekuwa mbovu Mwigulu leo asingekuwa Daktari pale wa Uchumi. Nadhani kuna maeneo ambayo sisi kama wataalam tunahitaji kuishauri Serikali, ni case by case na tusi-generalize. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimepitia Mpango huu kwa kweli naomba niseme tunahitaji kuja na chapter ya pekee ni jinsi gani tunakwenda kutatua tatizo la ajira kwa vijana wetu waliomaliza vyuo vikuu. Mimi naomba nijikite kwa vijana waliomaliza vyuo vikuu tu kwa ngazi ya cheti, diploma na digrii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Dodoma na nimefundisha Chuo cha Mipango, nina vijana wangu ninaowafahamu wamemaliza wana miaka 8 bado wapo mtaani. Wanaoathirika zaidi ni watoto wa maskini ambao hawapo aggressive, hawajui wapi pa kuanzia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashauri nini Serikali? Kwanza, natambua kuna program ndani ya Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inaendeshwa na ndugu zetu wa TAESA, wengi tumepiga kelele hapa kwamba vijana wanamaliza vyuo hawana uwezo, huwezi kupata uwezo chuoni, uwezo tunaupata kwa kupitia on job training. Kule tunafundisha theory lakini lazima tuje na programu ambayo itawahamisha wale vijana kutoka kwenye theory kwenda kwenye practice na ndiyo kitu ambacho Ofisi ya Waziri Mkuu wamefanya kupitia program hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamefanya nini? Wamechukua vijana kama internship program wamewaweka pale kwa mwaka mmoja wakawapa token ya 150,000 then wakawasaidia kuwa-groom, wanawapitisha kwenye zile life skills, interpersonal skills, communication skills, computer skills na kadhalika, aki-graduate pale wanam-link na job seekers au wale supplier wanaotaka watu kwa ajili ya kuwaajiri. Hiki ndiyo kitu ambacho mimi nashauri huu Mpango ujikite kwamba tuendeleze ile program ambayo imeshaanza, financing yake ambayo bado ipo weak vijana wanapomaliza vyuo wajiunge pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nataka tuje na Sera ya Internship. Tuna vijana wengi wapo mtaani tunalalamika kwenye vituo vya afya hakuna watoa huduma wa afya, tunalalalmika kwenye sekondari hakuna walimu lakini tuna vijana wengi mtaani. Ile program ambayo Waziri alikuja nayo wanawapa shilingi 150,000 kwa mwezi kwa nini tusiifanye hiyo program tuajiri vijana wale tuwaweke kwenye health facilities, tuwalipe shilingi 150,000. Kwanza itakuwa tumewapunguzia stress ya maisha, tumepunguza stress ya wazazi kuwatunza na tumepunguza stress ya watoto wa kike kuolewa tukawaweka pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji kuja na hiyo program kwenye huu Mpango kwamba sasa internship program iwe compulsory, tutengeneze sera na sheria kijana yeyote akishamaliza ile miaka mitatu anakuwa mainstreamed kwenye internship program. Akishamaliza pale, hapa sasa uhusiano kati ya TAESA na Sekretarieti ya Ajira, nitashangaa kuona Sekretarieti ya Ajira unamuacha kijana ambaye Mheshimiwa Waziri amem-groom mwaka mzima kupitia internship program unaenda kumchukua mtu hajapita kwenye program hiyo. Tunapiga kelele vijana hawana skills, hizo skills tutazijenga kwa kupitia internship program na Sekretarieti ya Ajira sasa fanyeni kazi na TAESA ili kuhakikisha kwamba vijana wanaokuja kule hatutakuwa na malalamiko hawawezi kujieleza, tayari tumeshawa-groom kwa mwaka mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine hili ni la Wizara tofauti. Tunapoenda kutumia hii program ya internship, nataka tuje na kitu kinaitwa policy maximum, hebu sisi kama nchi tujiwekee ukomo wa kisera, kijana asikae zaidi ya miaka miwili tangu amemaliza chuo. Tunajisikia aibu vijana wanakaa miaka mitano mtaani wanatembea na vyeti, sisi wenyewe tumewafundisha, tumewekeza na tunataka warudishe zile kodi. Hebu tuje na sera ambayo nimei-propose tuweke kiwango cha ukomo kwamba sasa Viwanda, Uwekezaji na watu wengine ambao sisi ndiyo creators wa kazi tukae pamoja tutengeneze modeling ya vitu gani ambavyo tunahitaji kuvifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kitu kimoja, kwa mfano, kwenye huu Mpango sijaona zile ajira milioni 8 ambazo tumeahidi tunaendaje kuzifikia? Tunahitaji kufanya modeling mwaka wa kwanza tutahitaji kufikia labda watu milioni mbili, mwaka wa pili milioni 3. Halafu pia tunawapataje hawa, ni kutoka private sector au public sector? Hicho kitu natamani kifanywe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni Mfuko wa Kuchochea Ajira kwa Vijana. Nashukuru Mheshimiwa Waziri ameliweka vizuri kwenye Mpango wake na namuunga mkono lakini naomba niboreshe kwenye ….

T A A R I F A

MBUNGE FULANI: Taarifa.

SPIKA: Taarifa, nimekuona Mheshimiwa.

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mchangiaji kwamba vijana wanaomaliza vyuo vikuu akiona zizi la ng’ombe, akiona kinyesi anakimbia, akiona banda la kuku anakimbia. Vijana hawa wanaomaliza chuo kikuu hawajapata mahali popote pale pakwenda ku- practice hata kama ni kilimo kidogo. Shule zetu kuanzia sekondari tumeondoa mashamba darasa, hakuna mahala ambapo mwanafunzi anaenda ku-practice.

Mheshimiwa Mwenyekiti, graduate anawazungumzia mchangiaji hawajawahi ku-practice hivyo vitu kuanzia wanaanza darasa la kwanza mpaka wanamaliza hiyo degree. Mimi napigiwa simu kama Mbunge, Mheshimiwa Mbunge tunaomba utusaidie kazi, nawauliza kazi gani? Wanasema kazi yoyote hata kufagiafagia. Hii inaonesha kwamba mpaka anamaliza chuo kikuu haja-define exactly na kile kinachofanyika nyumbani kwake ufugaji na kilimo haoni kama ni kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimpatie taarifa mwalimu ambaye amefundisha chuo kikuu muda mrefu kwamba watoto kwa upande wa ku-practice vitu ambavyo tunataka viendeleze taifa kwenye kilimo hawa graduates hawajapata fursa hiyo na ni weupe kabisa. Ukimwambia chips kuku anakimbilia kuila ila mchakato wa kupatikana kwa mayai na viazi hataki kusikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mzungumzaji. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana. Mheshimiwa Dkt. Chaya muda wako ulishapita, nilikuvumilia tu.

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi. (Makofi)