Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia katika Mpango huu wa Mwaka Mmoja, lakini pia wa Miaka Mitano inayokuja. Kipekee kabisa nikupongeze kwa namna unavyoendesha Bunge hili, kikao hiki. Hakika unatutendea haki kama Wabunge na tunafurahia uendeshaji wako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu dakika tano ni chache, lakini namuomba Mungu aniongoze ili niweze kuongea vyema kwenye suala la TANESCO, suala la nishati kwa ujumla, lakini pia, suala la TRA. Hakuna changamoto kubwa ninayoipata katika Mkoa wangu wa Songwe kama kusikia umeme umekatika, umeme hauna nguvu, umeme hautoshi, hakika wanavyokuwa wanaelezea wananchi kule huwa inasikitisha sana. Unakuta mwananchi ana ofisi, ofisi yake inategemea umeme. Analipa pango, analipa gharama nyingine zote, lakini mwisho wa siku anachokipata anakuta ni kichache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika kusema hayo nasema gharama za uendeshaji wa umeme katika nchi yetu bado ni za juu. Ukiangalia kwa upande wa TANESCO, ni base katika suala la domestic electricity, gharama inayolipwa kwa kila watt below 75 ni shilingi 100. Gharama inayoenda kulipwa above 75 kilowatts ni 350, hapa sijazungumzia suala la industrial electricity. Tunapoongelea ushindani wa soko na Mheshimiwa wetu Rais amejitanabahisha kuwa sera yake kubwa ni kuifanya nchi ya Tanzania iwe nchi ya viwanda na tunajua viwanda haviwezi kuendelea pasipokuwa na umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiangalia kwa namna gharama hizi za umeme zinavyokuwa na nikiangalia soko la bidhaa zetu tunakotaka kuzipeleka, unakuta wakati mwingine tunawapa wakati mgumu wajasiriamali wetu na wawekezaji kwenye ushindani wa soko katika mataifa mengine. Nitarejea katika mfano mdogo tu wa sukari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niseme kwetu sisi Tunduma hatuna shida sana na sukari kwa sababu, tuko mpakani tunatumia sukari ya Zambia. Wakati mwingine nawaza kwamba, inakuwaje nchi ndogo kama Zambia inatushinda sisi Tanzania kwenye uwekezaji wa sukari mpaka inaanza inafanya supply kwetu katika kanda zetu za mpakani kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sukari Zambia inauzwa Sh.2,000 ukija huku kwetu sukari inaenda hadi Sh.3,000. Sasa unapoongelea shilingi 3,000 na sidhani kama kuna Mtanzania yeyote humu ndani asiyependa kitu cha bei rahisi, hata kama tunasema ni uzalendo hauwezi ukaenda kwa style hiyo kwamba, nafanya uzalendo huku naumia. Kwa hiyo, niombe, niiombe kwanza Bodi ya Sukari itafute namna ya kuifanya biashara ya sukari kama fursa ya kuipatia Serikali pesa. Kama watawekeza vizuri na kama pia watu wa nishati watatuonea huruma kupunguza ghrama za uendeshaji wa viwanda naamini nchi yetu inakoenda itakuwa ni nchi ambayo ina mafanikio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani Zambia nchi ambayo ni ndogo walipe umeme kwa gharama za shilingi 77 kwa domestic, lakini pia kwa business wanalipa shilingi
108.99 wakati hapa Tanzania domestic tu ni shilingi 100 na tena ni shilingi 350 yani kwa wale ambao wanatumia above 75 kilowatts. Kwa hiyo, niiombe Serikali iangalie na itathmini vizuri kwenye suala la nishati ili viwanda vyetu viweze kukua, lakini pia iweze kufanya tathmini vizuri kwa kutafuta mazao ambayo yataweza kupunguza adha kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nirudi kwenye suala la TRA ambalo pia yamekuwa ni malalamiko…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba niishie hapo. (Makofi)