Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia Mpango wetu huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia nia na lengo la Mpango wetu huu ni kuendelea kukuza uchumi, kupambana na umaskini na ku-maintain hali ya nchi kuendelea kuwa nchi ya kipato cha kati lakini kuelekea kwenye higher middle income. Hii ina maana Mpango una malengo ya kuleta ustawi wa watu wake na kuongeza kipato cha chini na uchumi wa jamii na kuleta ajira zilizo rasmi na zisizo rasmi. Ili kuleta ustawi mimi nashauri Mpango uende sambamba na utekelezaji wa miradi ya utoaji huduma iliyokusudiwa katika Mpango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa imefanyika katika Mpango uliokwisha. Serikali imewekeza kwa wingi sana kwenye miradi mkakati au naweza nikasema product capacity project kubwa, reli, umeme, viwanja vya ndege, barabara na kadhalika. Katika eneo hili la umeme imewekeza sana, leo tunao umeme vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwekezaji yeyote anayewekeza anatakiwa lazima pia afahamu anatakiwa apate kile alichowekeza na Serikali imewekeza umeme ili kusaidia shughuli za kiuchumi kuanzia chini. Hapa nashauri Mpango uangalie uwezekano wa ku-trickle down economic activities katika maeneo ya vijijini kwetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wakulima tunalima lakini kazi yetu tukishalima mara moja tunauza basi, watu wanakaa wanasubiri mwaka unafika. Sasa umeme umefika vijijini, Mpango lazima uangalie kuhamasisha sekta binafsi kuona uwezekano wa kuleta viwanda vidogo kule vijijini lakini pia wale wawekezaji wengine waliokuwepo hapa kuona uwezekano wa kuanzisha viwanda vya kuwekeza kule vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namfahamu kijana ambaye anatambulika na SIDO, NYUMBU pia wanamtumia, amesoma Urusi na Uchina, yeye ana-assemble viwanda vidogo vya kutengeneza mafuta haya ya michikichi na pia anatengeneza viwanda vidogo vya kutengeneza sabuni. Ushauri wangu Serikali iwe na mpango wa kushawishi makampuni makubwa yanayoweza kuingiza viwanda vidogo kwenye vijiji vyetu ili wanaozalisha alizeti wakachakata alizeti, wanaozalisha mpunga wakakoboa mpungu. Hii itasaidia kuwa na activities za mwaka mzima pale, wa kuchakata mpunga, pumba za mpunga zitatumika kuchomea tofali; unga wa pumba za mpunga utaingia katika viwanda vya chakula cha mifugo na pia tutaendelea kuuza mali ambayo imeongezewa thamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lazima tuuangalie jinsi gani ya kupata wawekezaji wakubwa wanaoweza kuingiza viwanda hivi vidogo. China kuna viwanda vidogo na vya kati ambavyo vinauzwa kuanzia Dola 3,500 mpaka China. Sasa tukiweza mazingira mazuri kwa wafanyabiashara wa sekta binafsi wakaweza ku-import hizi tukapeleka huko vijijini, tukaondoa mentality ya sasa hivi ya kijijini mtu akistaafu, mtu akiwa mwalimu au mtumishi wa Serikali, akikopa ananunua pikipiki ndiyo anafanya biashara, kwa hiyo, biashara yake ni ya service. Sasa tutoe mentality zile wawekeze kwenye viwanda vidogo hivi vya uzalishaji ambavyo vitaajiri vijana wetu waliokuwepo kule vijijini na tutaongeza thamani ya mazao tuliyonayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili naomba nizungumzie ustawi wa shughuli zetu za kiuchumi, kilimo na mifugo. Leo kuna mifugo 33,000,000 na inasambaa tu na inasumbuana na wakulima lakini sasa hivi imefikia mahali inasumbua pia Hifadhi za Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alielekeza katika hotuba yake humu Bungeni kwamba watatenga hekta milioni 6 kwa ajili ya kuweka blocks za wafugaji ili waweze kufanya shughuli zao vizuri na wasiteswe, hili ni jambo zuri kabisa. Naomba sana hili lifanyike kwa sababu wafugaji wanaingiliana sana na wakulima. Leo hii sisi kwetu Namtumbo wafugaji waliondolewa Morogoro wameingia Namtumbo sasa hawana mahali maalum, wako ndani ya hifadhi na wako ndani na wakulima.

(Hapa kengele iligonga kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mpango utenge ardhi kwa ajili ya hawa wafugaji ili kuleta ustawi katika maeneo yetu. (Makofi)