Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Abdullah Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa zawadi hii. Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, Muumba wa Mbingu na Ardhi kwa kutujalia uhai, afya na ustawi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hii ni mara yangu ya kwanza toka tulivyoingia Bungeni kuongea ndani ya Bunge hili Tukufu, napenda vilevile kuwashukuru wannachi wa Jimbo la Mahonda pamoja na chama changu cha CCM kwa kunipa ridhaa na kuniingiza hapa mjengoni niwe mwakilishi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais, Mwenyekiti wetu wa Taifa, kwa uamuzi, ujasiri na umahiri wake mkubwa katika kuongoza nchi hii kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Sina haja ya kuyazungumza yote aliyoyafanya, walionitangulia, Mheshimiwa Askofu Gwajima na Mheshimiwa Polepole wameyasema yote ya msingi kabisa ambayo yamefanyika katika hii miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite katika maeneo matatu. Eneo la kwanza huu Mpango umekamilika na umefanyika kwa kiwango cha hali ya juu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu kugusia maeneo ambayo nahisi hayajawekewa mkazo mkubwa ambayo ni haya matatu. La kwanza, mchango wa diaspora katika uchumi wetu; la pili, dhana ya Tanzania kuwa logistics na transit hub; na la tatu, ushiriki wa Watanzania kwenye uwekezaji wa rasilimali zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, diaspora ina mchango mkubwa sana katika chumi za nchi. Kuna study ambayo nimeitazama ya mwaka 2018, katika nchi nne; Nigeria, Kenya, Uganda na sisi Tanzania. Mwaka 2018, fedha zinazotoka kwenye diaspora kuingia Nigeria, zilikuwa Dola bilioni 23.6 sawa na asilimia 6.1 ya GDP ya Nigeria. Kwa ule mwaka diaspora ili-contribute fedha nyingi kushinda export ya mafuta. Nigeria ndiyo nchi ya nne ulimwenguni kwa ku-export mafuta. Hata hivyo, Wanaijeria waliokuwa nje wameleta fedha zaidi ya mara mbili ya export yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kenya mwaka 2018, contribution ya diaspora ni Dola bilioni 2.72 sawa na 3% ya GDP yao. Uganda mwaka 2018 imeingiza Dola bilioni 1.24 sawa na asilimia 4.5 ya GDP ya Uganda. Mwaka huo huo Tanzania tumeingiza Dola milioni 430, sawa na 0.8% ya GDP yetu. Bayana kabisa, sisi kama Tanzania hatujalea hii sekta muhimu ambayo inaweza kuwa mchango mkubwa sana katika maendeleo yetu na katika Mpango wetu wa Miaka Mitano. Hii sekta ni lazima ilelewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna haki fulani fulani ambazo zinakuwa vichochezi. Kwa mfano, Mkenya mwenye passport ya nchi nyingine hadhibitiwi kununua ardhi. Halikadhalika na Uganda, lakini Tanzania huwezi. Sasa naiomba Serikali iyatazame haya, tuweze kuwapa hawa incentives ili sekta hii, hawa watu, Watanzania wameamua kuishi nje, washiriki na watusaidie katika mchango wa uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, tumejenga miundombinu mikubwa sana katika sekta ya transport; SGR, barabara nyingi, tumeboresha bandari na nyingine tunaziongeza; dhamira yetu siyo tu kuiendesha Tanzania bali kusaidia nchi zilizokuwa jirani. Tanzania inapakana na nchi tisa. Mbili tu kati ya hizo tisa zina access ya bahari ya hindi. Mbili tu; Kenya na Msumbiji. Saba hazina; na zote hizo saba, kuna advantage kubwa sana kwa wao kupitisha mizigo yao kwetu. Uganda, Rwanda, Burundi, Congo, Malawi, Zambia, wote wana advantage kubwa na ndiyo distance fupi, hupiti katika nchi nyingine. Ikitoka baharini inapita Tanzania, inaingia kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, advantages zote strategically tunazo. Kwa nini hawazitumii? Mambo magumu yote Serikali ya Awamu ya Tano imeyafanya. Upungufu wetu ni katika yale mambo mepesi (soft skills). Yapi hayo? Customer service; urasimu. Civil service kwa kijeshijeshi badala ya kuwa kirafiki na kibiashara. Haya mambo mepesi lakini thamani yake ni kubwa mno. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwashauri Mawaziri wa sekta, hilo jambo walitazame kwa macho makini ili tukuze uchumi na mpango wetu utimie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, ni ushiriki wa Watanzania kwenye uwekezaji. Serikali hii kwa nia njema kabisa inataka Watanzania tumiliki rasilimali zetu zilizokuwa kubwa. Sheria zilizopitishwa kwenye Extractive Industry; madini, oil and gas, sasa Tanzania ina hisa asilimia 16 katika kila investment kubwa ya namna hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vitu vinaitwa mutual farms au collective investment schemes. Hii ni mifuko tu; maneno makubwa tu haya ya Kiingereza, lakini ni mifuko ya kuwachangisha sekta binafsi washiriki kwenye miradi ya mkakati. Kunakuwa na mfuko maalum, mnasema pengine Kabanga Nickel, mahesabu yake haya; Kabanga Nickel tunajua ina idadi gani? Faida yake ni hii. Nyie mnaotaka kuchangia na mkawa na hisa, karibuni. Hiyo ndiyo njia sahihi ya kuongeza ownership.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa badala ya 16 tu ile ya Serikali peke yake, Watanzania sisi katika sekta binafsi, pamoja na wale wa diaspora walioko nje, wanaweza waka-invest tuka-own zaidi na ile fedha ya faida ikawa repatriated kwenda nje ikabaki hapa hapa.

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)