Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuchangia Mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwa kazi kubwa na nzuri iliyokwishafanya kufikisha maji vijijini. Kazi imeshaanza na inaendelea na mwenye macho haambiwi tazama maana kazi kubwa inaendelea kufanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tumejaliwa kuwa na vyanzo vingi vya maji, ikiwa ni pamoja na maziwa, mito mikubwa pamoja na mito midogo midogo. Kwa kutumia fursa hizo nashauri tutumie vyanzo hivyo tulivyojaliwa na Mwenyezi Mungu kuhakikisha tunafikisha maji vijijini. Maji ni uhai, maji ni kila kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake wengi vijijini wamejiajiri katika shughuli za kilimo. Hivyo basi, maji yakifikishwa vijijini watapata nafasi ya kwenda kushughulika na shughuli nyingine za kuzalisha mali na kuchangia kipato chao na pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukishindwa kufikisha maji vijijini wananchi wengi wakiwemo wanawake wataweza kupata magonjwa ya matumbo na tutaweza kutumia pesa nyingi kwa ajili ya kununulia dawa. Tukifikisha maji vijijini tutaweza kuepusha magonjwa na pesa zitaweza kwenda kufanya shughuli zingine badala ya kwenda kununua dawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kushauri kuhusu kilimo cha umwagiliaji. Kwa kutumia vyanzo hivyo hivyo vya maji tuendelee kuimarisha kilimo cha umwagiliaji. Ipo miradi ya maji ambayo ilianzishwa, tunaomba miradi hiyo iendelezwe na iweze kukamilika na mingine mipya iweze kuanzishwa ili kwa kutumia maji tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu tuweze kunufaika kwa kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, wananchi wengi wamehamasika kulima michikichi na wamehasika haswa na imepelekea wananchi wengi kulima kilimo hiki. Naiomba Serikali iendelee kutusaidia mbegu. Kwa awamu ya kwanza tumeshapata mbegu za kutosha, tunaomba sasa Serikali iendelee kuongeza mbegu ili wananchi wale ambao tayari wameshahamasika waweze kulima kilimo cha michikichi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kila anapopata nafasi anafika Kigoma. Tunakushukuru sana kwa kuweza kuuangalia Mkoa wa Kigoma na kuweza kufanya zao la mchikichi liwe zao mkakati. Kwa juhudi ambazo umeendelea kutuonesha na sisi tutaendelea kukuunga mkono kuhamasisha wananchi waendelee kulima zao hilo la mchikichi hatimaye tuweze kupata mazao ya mchikichi tuachane na kuagiza mafuta nje, tuweze kutumia mafuta tunayozalisha wenyewe. Pesa za kigeni tunazotumia kuagiza mafuta nje zibakie kwetu na kuweza kufanya shughuli nyingine za maendeleo. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)