Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Mohammed Maulid Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. MOHAMMED MAULID ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi kwa mara ya kwanza kabisa niweze kuongea kwenye Bunge lako Tukufu. Kwanza kabisa naomba niwashukuru wananchi wa Jimbo la Kiembesamaki, pamoja na Chama changu Cha Mapinduzi kwa kuniwezesha na kuniamini kuwa Mbunge katika jimbo hilo ili niweze kuwatumikia wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu katika hili utajikita katika mambo matatu; kwanza kilimo, pili viwanda na tatu barabara. Imeelezwa hapa kwamba zaidi ya asilimia 66 ya Watanzania wanategemea kuendesha maisha yao ya kila siku kwenye kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, imeelezwa vilevile katika Mpango huu kwamba kiasi cha viwanda 8,477 vimeanzishwa ili kuchochea ajira kadhaa zilizokusudiwa katika nchi. Mchango wangu upo kwenye suala la tatu la barabara. Mambo haya matatu yaani barabara, kilimo na viwanda vinakwenda sambamba, kama kimoja kikiwa kimetetereka vingine viwili havitakwenda sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara zetu vijijini haziko katika hali nzuri, wasiwasi wangu sijui kama viwanda hivi vitafanya kazi vizuri wakati malighafi au raw materials zinatoka vijijini.

Kwa hiyo, basi niungane na Wabunge wengine waliochangia kwamba TARURA iongezwe fedha ili na wao waweze kuzitengeneza barabara hizi ili huu mzunguko ambao tunauzungumzia hapa uweze kuwa vizuri, otherwise viwanda hivi vitashindwa kufanya kazi kama tulivyotoka huko nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani mchango wangu kwa leo ni huo tu. Ahsante sana. (Makofi)