Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mara nyingine nishukuru kiti chako kwa kunipa nafasi hii ya kuzungumza mbele ya Bunge lako Tukufu likiwa limeketi kama kamati. Kimsingi kwa sababu muda hautoshi, naomba nijielekeze zaidi kwenye sekta ya utalii. Sekta ya Utalii katika nchi yetu bado hatujaitendea haki, kwa sababu pamoja na kwamba tuna vivutio vingi vya asili, lakini bado tumeshindwa kuhakikisha kwamba sehemu kubwa ya vijana wetu hasa ambao wanaweza wakaenda kwenye elimu ya kati ama vyuo vyetu vya VETA wakapata elimu ambayo inaweza kuwasaidia kujikita katika tasnia ya utalii na kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi nimepata nafasi ama bahati ya kuishi kwenye nchi mbalimbali zinazotegemea sana utalii. Gharama ya utalii kwetu ni kubwa mno na hata tafiti zinaonesha kwamba kati ya watalii mia moja ambao wanatembelea Tanzania ni 20 tu ambao wanarudi. Idadi hii ndogo mno, ni lazima sasa kama Serikali tujikite kutafuta sababu kwa nini watalii hawa mia hawarudi wote ama hawawi mabalozi kwa wengine kwa ajili ya kuvutia vivutio vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo naomba kujikita ni eneo la kilimo; tumekuwa na slogan nyingi; kilimo kwanza, kilimo uti wa mgongo, lakini kimsingi Mtanzania hahitaji hizi kauli mbiu, kilimo kwake ndio kila kitu, amezaliwa anategemea kilimo, amesomeshwa na kilimo, anaishi kwa kilimo, haitaji mtu kumpa kauli mbiu, anahitaji mazingira rafiki ya yeye kujikita kwenye kilimo. Mazingira ambayo tumemwekea sasa hivi si rafiki. Naomba nitumie mfano wa wakulima wa miwa katika Bonde la Kilombero, nilizungumza mwanzo kwamba kati ya tani 900,000 ambazo mkulima wa miwa anazalisha pale Kilombero, ni tani 600,000 tu ambazo zinaweza kununuliwa na kiwanda pekee cha Ilovo, tani 300,000 zinaharibikia mashambani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mazingira hayo bado tunasema miwa ni zao la kimkakati, lakini ni zao la kimkakati hakuna mazingira wezeshi ya kuhakikisha kwamba mkulima wa miwa ana soko la uhakika. Matokeo yake sasa hivi watu wamekata tamaa, pendekezo langu naomba Serikali iwe inaagiza sukari kwa sababu jukumu la kuagiza deficit anaachiwa mzalishaji ambaye ndiye mwenye jukumu la kuhakikisha ananunua miwa ya kulima; na kwa kuwa sukari ya kuagiza ni bei rahisi ukilinganisha na sukari ya kuzalisha; mzalishaji huyo wa sukari badala ya kum-encourage mkulima kuzalisha amekuwa kikwazo kwake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, naomba Serikali ihakikishe kwamba inaenda kumsimamia Ilovo kukamilisha upanuzi wa kiwanda ili kuhakikisha kwamba mkulima ana soko la uhakika…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa kengele imegonga.

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante. (Makofi)