Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Natumia fursa hii kukushukuru wewe binafsi na kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenijalia mara yangu ya kwanza kusimama katika Bunge lako hili tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapohapo nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Kwahani kule Zanzibar ambao kwa imani moja wamenileta hapa niwe mwakilishi wao. Walikuwa na simanzi kwa vile wanaona kama wameondokewa na Mbunge mwaminifu, mtiifu na mwenye bidii, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Nawahakikishia kwa nafsi yangu kwamba mimi naweza na nitawapa utumishi uliotukuka na kufuta machozi madogo madogo ambayo walikuwa wanayatoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu na Mawasiliano na kwa kiasi fulani nitajikita zaidi katika kuuchangia Mpango huu wa Miaka Mitano. Nchi yetu kama hii kwa kitendo cha Rais wetu mpendwa kuanzisha reli iendayo kasi kwa kutumia fedha zetu za ndani kwa kipindi hiki ni suala la kumpongeza na kumtakia mafanikio mema katika safari hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilibahatika kidogo kusafiri (mtundu wa kusafiri), ninakona reli kama hii ya Shirika la Reli la Marekani linaitwa Acela inayochukua abiria na mizigo kutoka Washington DC mpaka New York kwa mwendo wa saa nne na nilipanda shirika hilo. Leo nchi kama yetu ya Tanzania hili ni jambo la mfano, Rais wetu mpendwa ameidhinisha zaidi ya shilingi trilioni saba na kuendelea na reli inaendelea. Kwa hiyo, hili ni jambo la kuigwa na huyu ni Rais wa kuombewa dua kila siku kwa madhehebu yote ili aweze kuishi na aweze kutufikisha salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kuchangia kuhusu Shirika la Ndege la ATC. Shirika la Ndege la ATC kila mmoja leo anaona mafanikio yake na limeweza kwa mara ya kwanza katika utawala wa Dkt. John Pombe Magufuli kutoa gawio (dividend) kwa Serikali. Kwa hiyo, hili ni jambo la mfano; amefufua shirika hili na leo lina ndege zaidi ya tisa na nyingine za mizigo ziko mbioni zinakuja. Kwa hiyo, hili ni jambo la mfano katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni ilivyoingia COVID tumeona deterioration ya bidhaa kuja kwetu Tanzania. Shirika la Ndege la Ethiopia limetumia nafasi ya kuchukua mizigo ya wafanyabiashara kuleta Tanzania. Ni jambo la faraja kusikia kwamba ndege ya mizigo inakuja na iko njiani. Kwa hiyo, uchumi wetu utazidi kuhuika kwa kuwa sasa hivi tunatumia ndege yetu wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini si hivyo tu, nadokeza kwamba hivi karibuni shirika hili baada ya hii COVID kuondoka, lina mpango wa kuazisha safari za kuelekea Gatwick pamoja na London, Heathrow. Kwa hiyo, Watanzania hapa watakuwa wanapanda direct flight kutoka Julius Kambarage Nyerere Airport mpaka Gatwick. Kwa hiyo, hili ni jambo la mfano kwa Shirika la Ndege na hizi zote ni juhudi za Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli; hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho katika uchangiaji wangu, natoa ushauri kwamba uvuvi wa Bahari Kuu ambao unachochea uchumi wetu uangalie ofisi za Zanzibar. Hapa katikati utoaji wa leseni ulisababisha ofisi ya Zanzibar kidogo kutikisika. Wavuvi wenye meli walikuwa wengi lakini alibakia mvuvi mmoja tu ndiye aliyepewa leseni. Kwa hiyo, zipo dalili za kuwasaili ikiwa hali imetengemaa na wakati wa utoaji wa leseni za meli za uvuvi wakaangalie kwa makini sana kutoa leseni kwa wakati na fair ili kusudi ile shake ya ofisi isije ikatokea tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa jumla mimi naunga mkono mpango huu kwa asilimia 100 ili mambo yaende.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)