Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia. Kwanza ningependa kutoa mchango wangu kwenye eneo la kilimo na biashara. Mpango huu ni mzuri, lakini unachangamoto hasa kwenye eneo hilo la kilimo na biashara ambalo ni eneo muhimu sana kwa uchumi wa nchi. Nianze kwanza ku-declare interest hata mimi ni mkulima wa chai kwa sababu nitachangia kwenye eneo la chai. Mpango huu kwa eneo la kilimo kwa maelezo ya Waziri mwenyewe haujaonyesha mafanikio makubwa kwa eneo la kilimo, ukuaji wa uchumi eneo la kilimo umekuwa mdogo na tunasema mchango wa kilimo kwenye pato la Taifa umekuwa mdogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo ambalo naliona kwamba linaweza likaleta mabadiliko makubwa ni eneo la chai. Zao la chai kwa ujumla wake na sekta ya kilimo kwa ujumla wake imekuwa chini kwa sababu moja kubwa, uwekezaji katika eneo la chai umekuwa mdogo, uwekezaji upande wa Serikali lakini hata uwekezaji kwa upande wa watu binafsi. Kwa hiyo ipo haja ya kuongeza kwa kiasi kikubwa sana uwekezaji kwa namna nyingi na nitazitaja hata chache tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo kubwa ni kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya wakulima wa maeneo ya chai. Ukiangalia kwa undani kabisa utaona wazi kabisa utaona wazi kabisa wakulima wetu wa chai hasa wadogo wadogo bado wana-struggle sana kuzalisha chai yao. Kule kwenye maeneo ya Njombe kuna viwanda vikubwa vya chai kama kumi na tisa. Viwanda hivyo vyote vinakuwa own na watu wa nje, wakulima wetu bado wanafanya njia za kizamani za kulima na hawawezi kutoa mchango mkubwa. Ni vizuri sasa Serikali ikajikita zaidi huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia eneo ambalo unaliona lazima tuongeze uwekezaji, ni eneo la ugani. Katika global average wakulima 400 wanatakiwa wahudumiwe na Mgani mmoja, lakini kwetu sisi hapa ni wakulima 1,100. Ukienda kwenye upande wa miundombinu ya umwagiliaji bado tuko nyuma sana, hatuwezi kwenda na kilimo ambacho tunategemea mvua hasa kwenye mazao ya chai na mazao ya avocado. Kwa hiyo tuna kila sababu, Tanzania mpaka leo kwa eneo lililolimwa kwa mwaka 2019, karibu hekta 13,000,000 ni asilimia 20 tu ambayo ina umwagiliaji kama hekta laki nane. Tunatakiwa twende juu zaidi na zaidi ili tuweze kuona tija kwenye eneo la kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima tu fungamanishe hii sekta ya kilimo ya process na eneo la Nyanda za Juu Kusini Njombe ikiwemo, ni eneo lenye potential kubwa sana ya kuwa game changer kwenye kilimo kama tutafanya uwekezaji mkubwa na tutaita uwekezaji. Hata hivyo, tukumbuke tuna wawekezaji kule wana-struggle kwa sababu ya tozo nyingi sana ambazo kwa kweli pamoja na jitihada za Serikali na tumeona kwenye kitabu hapa, lakini tozo bado ni nyingi sana. Kwenye chai peke yake kuna tozo zaidi 19.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitabu na kwenye hotuba ya Rais na kwenye Mpango tunakwenda kwenye kilimo cha biashara maana yake kilimo cha biashara unakuwa competitive ukilinganisha na wenzako. Tuwaangalie Kenya kilimo chao chai, tozo ziko mbili tu; Uganda wana tozo moja; sisi tuna 13. Twende kwenye avocado na matunda matunda tuna tozo karibu 45; pamoja na kazi nzuri ya serikali bado jitihada zinatakiwa zifanyike. Nafahamu kuna blue print inaendelea, lakini kwa kweli impact kwa wakulima bado ni kubwa na negative.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee eneo la wakulima ambalo ni la viwanda sasa hivi vya chai vilivyopo. Nipende kusema wana mchango wao mkubwa, lakini wanaweza wakachanga Zaidi. Kuna mmiliki mwenye viwanda vya chai ametoka Kenya anaitwa DL, sasa hivi anashindwa hata kulipa mishahara, anashindwa kulipa pension, ni miezi 12 wafanyakazi hata pensions zao hazijalipwa, wafanyakazi wana maisha magumu, wakulima wana maisha magumu, wana mwaga chai. mahindi ukikosa mwekezaji au ukikosa mnunuzi utaweka ghalani, utauza mwaka unaofuata, lakini chai ukikosa mnunuzi unamwaga. Kwa watu ambao wanaisha maisha magumu wanatafuta mitaji kwa shida, wanalima chai, wana kila haki ya kuhakikisha kwamba wanasaidiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la mwekezaji huyu ni moja, amenunua viwanda vya chai lakini hajakamilisha process nzima ya ku-transfer viwanda vya chai na sababu kubwa tunaambiwa ni TRA kwamba wanasema kuna capital gain tax haijalipwa, lakini anayelipa capital gain tax ni yule aliyeuza. Kwa hiyo huyu anashindwa kwenda kukopa, anashindwa kwendelea, anashindwa kuchukua chai, watu wanamwaga chai yao, lakini kosa siyo lake. Sasa kama tunataka mpango huu na tunataka chai iweze kwenda kuzalishwa zaidi na malengo ya Serikali ni kufanya chai kama zao la mkakati liweze kuingia na pesa za kigeni; tuwaangalie wawekezaji hawa, hata huyu mmoja ambaye ana viwanda karibu zaidi ya vinne na anaajiri zaidi ya watu 2,000 na anasaidia kwa kutoa mbolea, kwa kutoa madawa kwa kulima wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye moja lingine la avocado, avocado it is not be a big business, avocado can be a big changer, tunaita green gold, kwa kweli tunatakiwa tujipange vizuri na naomba sana Serikali tunapozungumzia miundombinu wenzeshi, lazima tuangalie zao hili. Kwenye mazao ya mbao naomba niseme na nimalizie kwa kusema, wakulima na wafanyabiashara wa Njombe wana hali mbaya sana, kwa sababu tunahitaji mahusiano mazuri kati yao na TRA, tunapokwenda siyo kuzuri kwa maana watu wanaona hakuna faida ya kulima misitu, wamelima misitu hawawezi kuiuza, hawawezi kupata faida, ni jambo tunatakiwa tulitiliee maanani na Waziri wa Fedha ameshaandikiwa ili atoe nafasi kwa hawa Watanzania, wafanyabiashara wa Njombe waweze kukaa na TRA kuona namna gani wata-improve.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)