Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, natanguliza shukrani zangu za awali kwa wote walioandaa hotuba hii ya Wizara ya Elimu na hasa Mheshimiwa Waziri wa Elimu na Naibu Waziri.
Matatizo ya Jimbo langu la Bunda Vijijini; moja ni kutoa kibali cha ufunguzi wa sekondari ya (High School) ya Makongoro (Makongoro High School). Tunahitaji msaada wa Wizara, wananchi wamejenga vyumba vya madarasa, mabweni na jengo la utawala, tunahitaji shilingi 72,000,000 ili kumaliza ujenzi wa high school hii. Tunaomba msaada ili kupunguza makali ya michango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili ni upungufu wa walimu wa sayansi, (kemia, fizikia, biolojia na hesabu). Zaidi ya sekondari 30 wanahitajika walimu 30.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni matatizo ya mazingira ya vyoo. Zaidi ya shule za msingi 40, zina matatizo ya vyoo vibovu vya shule na tatizo la maji shuleni, hivyo naomba Wizara ya Elimu kupitia mashirika yake ya kutoa huduma za msingi na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na tatizo la vyoo magonjwa ya watoto shuleni yameongezeka sana, (typhoid, kuhara, U.T.I). Naomba msaada wa suala hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namba nne, matatizo ya maabara, madarasa na nyumba za walimu. Wizara iangalie namna ya kusaidia Jimbo hili jipya.