Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Natambua tunajadili Mpango huu wakati dunia inapita kwenye mtikisiko mkubwa wa COVID-19. Nimeangalia ripoti ya World Bank, ukuaji wa kibiashara kidunia ulikuwa umeshakua mpaka kufikia asilimia 64 lakini baada ya COVID- 19, biashara ya dunia ime-drop mpaka asilimia 37 ya pato la dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kusema haya, nataka niiombe Serikali, kwa sababu wataalam wa kiuchumi wamefananisha anguko hili na lililotokea wakati wa Vita ya Pili ya Dunia, nataka tunapojadili hotuba hii ya Mpango basi tuonyeshe reflection kubwa sana na gonjwa hili la COVID-19 ili tuweze kuchangia ndani ya changamoto hii tusiwe tofauti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze kutekeleza Mpango tunahitaji fedha ya kutosha. Nimeona Mheshimiwa Mpango na baadhi ya Wabunge wakitoa malalamiko kwa namna ambavyo kumekuwa na malalamiko makubwa sana kwenye ukusanyaji wa kodi, tunahitaji fedha ili kuweza kutekeleza Mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tujiulize ni kwa nini tunakusanya kiasi kidogo cha kodi ukilinganisha na nchi nyingine nyingi lakini pia kuna kilio kikubwa kuhusu mzigo wa kodi. Tanzania tunakusanya kodi asilimia 13 ya pato la Taifa. Nimefanya research kidogo Lesotho wanakusanya asilimia 29 ya pato la Taifa; Kenya wanakusanya asilimia 20 ya pato la Taifa; South Africa wanakusanya asilimia 28 ya pato la Taifa; ukienda Burkina Faso wanakusanya asilimia 18 ya pato la Taifa; Namibia asilimia 30; Zimbabwe asilimia 21.1; Mozambique asilimia 23 na Zambia asilimia 15.2. Tanzania tunakusanya asilimia 13 ya pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini sababu? Hii inathibitisha kuna udhaifu mkubwa sana kwenye sayansi ya kukusanya kodi. Namwomba Mheshimiwa Mpango anapokuja kuhitimisha hapa atuambie ni kwa nini kuna malalamiko na kelele nyingi kwenye ukusanyaji wa kodi na wakati tunakusanya asilimia 13 tu ya pato la Taifa ukilinganisha na nchi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijielekeze kwenye hoja yangu ya msingi kabisa ya zao la alizeti. Kuhusiana na kilimo cha zao la alizeti kama nchi tunatia kichefuchefu. Naomba niseme hivi, kuna mtu mmoja aliwahi kusema Afrika miujiza haitakuja kufika mwisho na mimi ninaungana naye. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia zaidi ya asilimia 60 ya ardhi inayofaa kwa kilimo duniani inapatikana Afrika lakini kila mwaka Afrika tunatoa zaidi ya dola bilioni 27 tunaangiza vyakula kutoka nje. Kwenye muujiza huu, Tanzania hatuko nyuma, kila mwaka nchi ya Tanzania tunaagiza mafuta zaidi ya dola milioni 280. Tunatumia wastani wa dola milioni 280 kuagiza mafuta ya kula kwa pesa za kigeni badala ya pesa za kigeni kuingia ndani kupitia zao la alizeti kwa kuuza mafuta, tunatumia fedha za kigeni kuagiza mafuta kutoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefanya study ndogo sana kwenye zao la alizeti ambalo limekuwa recognized na WHO kwamba ni zao linalotoa mafuta bora kabisa, inaonyesha kwamba karibu nusu ya eneo la Tanzania linafaa kwa ajili ya zao la alizeti. Mfano, Simiyu, Shinyanga, Singida, Iringa, Morogoro na kwingineko wanaweza kulima alizeti. Cha ajabu tunazalisha tani laki nane peke yake kwenye zao la alizeti, kiasi hiki hakifiki hata 0.1 percent ya kiasi cha mbegu za alizeti kinachozaliwa dunia nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka haraka nitoe mfano wa nchi kama Ukraine, nchi ambayo inaongoza kwa kilimo cha alizeti na uzalishaji wa mafuta. Nchi ya Ukraine inazalisha takribani tani milioni 16.5 kwa mwaka lakini wanalima kwenye square meter za mraba 20,000. Ukisema square meter za mraba 20,000 ni sawasawa na nusu ya Mkoa wa Singida maana Mkoa wa Singida ni square meter za mraba 48,000. Sisi Tanzania tunauza mafuta, kahawa, chai, almasi, tunapata dola bilioni 5 kwa mwaka na wakati Ukraine hiyo dola bilioni tano wameipata kwa kuuza mafuta ya alizeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka haraka nimalizie, kama Ukraine wanafanikiwa, kama Ukraine wanaweza kulima zao hili na kupata manufaa sisi tunashindwa nini? Namwomba Waziri wa Viwanda na Biashara, Waziri wa Uwekezaji, Waziri wa Kilimo hebu wakae chini na kutafakari, umizeni vichwa acheni kumbwelambwela.

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia galoni ya lita tano ya mafuta ya kula inauzwa Sh.28,000, wananchi wanalia, wananchi wanateseka. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MBUNGE FULANI: Taarifa.

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kidogo niwape solution, nataka niwasaidie hawa…

MWENYEKTI: Muda wako umeisha, ahsante sana Mheshimiwa Jesca Kishoa. (Makofi)